Tanzania haijapate Mwinjilisti Mwingine mwenye nguvu kitaifa kama Moses Kulola sababu aliondoka bila kukabidhi mtu kipawa alichokuwa nacho

Tanzania haijapate Mwinjilisti Mwingine mwenye nguvu kitaifa kama Moses Kulola sababu aliondoka bila kukabidhi mtu kipawa alichokuwa nacho

Mimi nashauri walioko Karibu Na Mwamposa wambambie apunguze bei ya yake Maji yake !

Shilingi 1,000/- kwa chupa moja ni bei kubwa sana.

Auze shilingi 500/- kwa chupa.

Yeye si ananunua at large quantities kwa hiyo anapata “trade discount “

Kama anayatengeneza mwenyewe Pia bei iwe hiyo.

Afanye kama Kwa Bwana.

Nazani leo sio kufanya faida bali huduma zaidi.

Mbona maji “brands” nyingine wanauza bei ya shilingi 500/- sembuse kwenye huduma ya kiMungu?! Si inapaswa kuwa nafuu zaidi ilimradi awe ana braak even au kutengeneza faida kidogo!

Naomba mumfikishie huo ushauri.
Hiyo ni biashara mzee tena serikali ilitakiwa ikusanye Kodi yake pale
 
Humjui BULUDOZA wewe?



Hivi Kwanini ajiita hilo jina ?

Lilianzaje?

Mimi naona kama ni kujikweza, Mbona Mitume wale wa kanisa la kwanza hawakuwa na hizo mambo ya majisifu?

Sema wanyakyusa bana ! Namfikiria Lusekelo naye huwa anapenda kujisifu yeye anajiitaga katapila sijui nani vile?!

Natamani angekuwa humbled ingependeza zaidi na Utukufu wote atazidi kupewa Bwana!
 
Kifupi Kwa uinjilisti ni kidogo mno tu kufikia viwango vya akina Moses Kulola,Billy Graham au Renhard Bonke vya kujikita tu kwenye injili ya kuleta wokovu tu watu watubu dhambi na kuacha
Watu wazito sana hawa umewataja mkuu, japo mimi si mtu wa dini lakini nawaheshimu sana hawa watu, enzi hizo wazazi wangu walipata wokovu kwenye mkutano wa Reinhard Bonke.(nilikuwa mdogo, wazazi ndo waliniambia) ile injili ilibadilisha sana maisha yao.

Kipindi nakua naikumbuka sana mikutano ya Moses Kulola tukiwa na familia hakika alikuwa na wito wa kweli kwa Mungu.
 
Uzi una makandokando, anayeongelewa ni Muinjilisti na sio mchungaji Wala muombezi
 
Viongozi wote wakubwa wenye vipawa vikubwa kwenye Biblia kabla kuondoka duniani walikabidhi vipawa vyao kwa watu wengine specific.Musa alikabidhi kwa Joshua na Eliya alikabidhi kwa Elisha na baada ya kukabidhiwa wakabidhiwa walifanya maajabu makubwa

Moses Kulola alikuwa Mwinjilisti akihubiri.maelfu walikimbia kutubu dhambi na kuziacha kwenye mikutano yake kama ilivyokuwa kwa Yohana Mbatizaji Yerusalemu na Yudea yote walikwenda kwake kutubu dhambi. Tofauti na sasa wengi huenda kwa ajili ya maombi na maombezi tu mambo ya kutubu dhambi hawana mpango nayo.Yohana mbatizaji alikuwa na huduma kuu ya kutubisha watu dhambi zao na kuacha hajawahi ponya mtu wala muujiza wowote Billy.Graham pia alikuwa na kipawa hicho cha kuleta mamilioni kutubu dhambi na kuziacha

Moses Kulola pia anafahamika zaidi kwa kuwaleta wengi kutubu dhambi na kuziacha kwa Tanzania

Lakini kutokana na Mateso makali aliyopitia mikononi mwa Kanisa na magerezani huko na kwa mataifa wasiojali Injilli alihangaika na mateso yake akasahau kukabidhi kazi yake kwa mwingine awe kama yeye na zaidi siku zake za kuondoka duniani zilipofika.Hivyo kuliacha Taifa la Tanzania njia panda halina Mwinjilisti mwenye nguvu kama yeye mleta watu wengi wautubu dhambi na kuziacha. Kaliacha taifa njia panda limejaa huduma za maombi na maombezi na uchungaji Kila mtu anataka kuwa mchungaji au kiongozi wa huduma ya maombi na maombezi Uinjilisti hawataki

Vyombo makanisa mengi yamekuwa matapeli huombq kuwa yanahitaji kwa ajili ya injili uongo mtupu wanahitaji vyombo kwa ajili ya kwaya tu kanisani hakuna cha uijilisti wala nini

.Katika huduma zisizopendwa tena ni Uinjilisti wakati wa kipindi chake yeye Moses Kulola alikuwa role model watu wengi walipenda sana Uinjilisti kuliko uchungaji au huduma za maombi na maombezi

Leo ni Ijumaa kuu tunapokumbuka mateso Yesu alipata tukumbuke pia mateso Moses Kulola alipitia na vizuri kila aliyehusika kumtesa kwa mawazo,kwa maneno au vitendo awe mtu binafsi au taasisi au kikundi kwa siri au kwa wazi au kwa kumuwazia au kumsema vibaya aombe msamaha kwa Mungu Ijumaa kuu hii na kuomba rehema za Mungu asamehe alete mwingine kama Moses Kulola.Sioni Nchi ku move forward kwa nguvu sana kwenye Uinjilisti kama kanisa halitafanya toba kwa madhira iliyompitisha Moses Kulola


Na kama Taifa tuombe Rehema za Mungu kama taifa tuhurumiwe sababu sio vizuri sana mtumishi mwenye nguvu kama yule kufia kwenye nchi yetu kwa mateso aliyopata ndani ya nchi.Nchi twaweza laanika kwa kuwajibika kwa kifo chake sababu alifia kwetu kwa mateso
Damu yake iko nchini kwetu Bugando ,Mwanza ,Tanzania

Nawatakia Ijumaa kuu njema
Hiyo sio kazi ya Kulola. Kama Kulola alipewa na mtoaji basi mtoaji huyo huyo ndiye mwenye huo wajibu wa kujua jinsi ya kuvuna mavuno yake.
 
Matunda ya idadi ya wanaookoka mikutano yake

Biblia inatamka wazi mtawatambua kwa matunda yao

Mwinjilisti hapimwi kwa jina kujiita Mwinjilisti Moses aliketa maefu kwa kanisa kupitia huduma yake

Uinjilisti sio cheo ni kazi
Ulipima vipi kuwa waliookoka Ni kweli wameokoka kwa Kristo?
Au kwa macho ya Rohoni!
[emoji1787][emoji1787]

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nashauri walioko Karibu Na Mwamposa wambambie apunguze bei ya yake Maji yake !

Shilingi 1,000/- kwa chupa moja ni bei kubwa sana.

Auze shilingi 500/- kwa chupa.

Yeye si ananunua at large quantities kwa hiyo anapata “trade discount “

Kama anayatengeneza mwenyewe Pia bei iwe hiyo.

Afanye kama Kwa Bwana.

Nazani leo sio kufanya faida bali huduma zaidi.

Mbona maji “brands” nyingine wanauza bei ya shilingi 500/- sembuse kwenye huduma ya kiMungu?! Si inapaswa kuwa nafuu zaidi ilimradi awe ana braak even au kutengeneza faida kidogo!

Naomba mumfikishie huo ushauri.
Atoe Bure, gharama za uandaaji wa maji Ni sadaka za waumini?
Kwani sadaka anazopewa anataka anunue magari mangapi?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Hivi Kwanini ajiita hilo jina ?

Lilianzaje?

Mimi naona kama ni kujikweza, Mbona Mitume wale wa kanisa la kwanza hawakuwa na hizo mambo ya majisifu?

Sema wanyakyusa bana ! Namfikiria Lusekelo naye huwa anapenda kujisifu yeye anajiitaga katapila sijui nani vile?!

Natamani angekuwa humbled ingependeza zaidi na Utukufu wote atazidi kupewa Bwana!
Lusekelo ni Mnyakyusa au Mkinga?
 
Huyo Moses Kulola kuja kumshinda Diana Bundala kwenye uinjilist May be aende direct mbingun kusoma gospel ndo aje ashindane. Yule mama ni shindikanaa coz yeye mbingun anaendaga daily
Diana Bundala anafanya uinjilisti gani?. Maana hamuamini Yesu.
 
Uinjilist ndio kufanya kitu gani?? na uchungaji ni kitu gani??
Uinjilsiti ni kupeleka habari njema kwa wasioamini au waliopo dhambini, wakati mchungaji ni kuchunga wale walioamini wasirudi nyuma dhambini
 
Nadhani mwinjilisti wa kwanza wa kilokole aliitwa Harris Kapiga miaka 1928, wakaja akina Andrea shimba, baadae miaka ya 1960 ndio wakaja wainjilisti Moses Kulola, Lazaro na Kiwia.
 
Back
Top Bottom