Tanzania haijapate Mwinjilisti Mwingine mwenye nguvu kitaifa kama Moses Kulola sababu aliondoka bila kukabidhi mtu kipawa alichokuwa nacho

Tanzania haijapate Mwinjilisti Mwingine mwenye nguvu kitaifa kama Moses Kulola sababu aliondoka bila kukabidhi mtu kipawa alichokuwa nacho

Niseme tu, nyakati zimebadilika sana. Leo hii hata kama angekuwepo Moses Kulola bado angepata taabu sana kuhubiri aina yake ya Injili. Baada ya kuja uchafuzi wa Injili ya wasaka afya na mafanikio, masikio ya watu wote, wapagani, Waislamu kwa Wakristo wameelekeza mioyo yao huko. Ndio maana utaona wafuasi wengi wa akina kuhani Musa, Mwamposa nk ni Waumini wa imani tofauti. Wahubiri wanaofuata maagizo ya Kristo kwa kuhubiri toba wapi ila hawawezi kuwa na mega churches, ni makusanyiko madogo mno. Matapeli wa Injili ndio wanawake, sawa sawa na Kristo alivyosema itakuwa nyakati za mwisho.

Hivyo hoja sio Kulola kutokabidhi kipawa kwa sababu afanyaye hivyo ni Roho Mtakatifu wala si mwanadamu. Tatizo hapa ni watu kupenda mafundisho ya uongo. Nakumbuka kwenye uchaguzi wa mwisho kabla ya kifo chake kulikuwa na njama za maaskofu kumng'oa Kulola. Sasa ndio uone uasi ulianzia humo humo ndani, na hao waliotaka kumng'oa ndio wameshika kijiti hii leo. Kutwa kucha mahakamani kwa kesi za wizi na kugombania madaraka. Vipofu wanawezaje kuwaongoza vipofu wenzao?
Moses injili yake haikuwa kushawishi akili
Kama leo mahubiri yake yalijikita kwenye kwenda Jehanamu kwa wenye dhambi na unyakuo watu waliokoka kibao

Akihubiri Habari xs Jehanamu neno linafanyika live kwa msikilizaji anaona Jehanamu live bila chenga na yeye akipelekwa ndio maana wengi walikimbia mbio kuokoka akihubiri unyakuo watakaoenda na kuachwa mtu atakaeachwa anapata maono live akiachwa watu wakinyakuliwa akiita kuokoka ili mtu asiachwe unyakuo watu walikuwa kama wehu wanakimbia mbele wengine mabosi maofisini
Sasa hivi mahubiri ya kiinjilisti yanawinda akili sio roho ndio maana matokeo madogo.

Sasa hivi wahubiri Jehanamu na unyakuo .hawapo

Moses alijikita maeneo hayo mawili tu ns watu walikoma walijua kiyama hiki hapa walikiona live bila chenga

Akihubiri mwenye dhambi utaachwa siku.ya unyakuo au utaenda Jehanamu alikuwa hatanii lazima Jehanamu uione live hapo hapo mkutanoni na maono ya kuachwa unyakuo ukija ujiaona bila chenga.Alikuwa.akihubiri dakika chache tu ila huo muziki wake mwenye dhambi lazima akimbie mbio kwenda madhabahuni hata kabla kuitwa akilia mno akilia kujali elimu yake au cheo chake

Aliamini kuwa neno lazima lifanyike mwili akihubiri Jehanamu mtu lazima aone Jehanamu akihubiri unyakuo mtu lazima aone live ns yeye anafall wapi?
Sasa hivi uinjilisti unawinda akili tu

Akilia kwa watakaoenda jehanamu mkutano wote unatungua kilio sababu Jehanamu kwao inakuwa live

Sasa hivi porojo nyingi zinahubiriwa injili za ku convince akili na kushawishi kujiunga na kadini ketu

Mtume Paulo alisema wazi nilipokuja kwenu sikuja na injili.ya ushawishi wa akili bali.katils udhihirisho wa nguvu za Mungu sio porojo.za ushawishi wa akili xa manipulation xa kisaikolojia za ku.manipulate human brain
 
Kulola alikuwa na nguvu KWA sababu wao ndio waanzilishi wa injili ya uamsho nchini
 
Nasali kwake Mwamposya huduma yake ni ya maombi na Maombezi sio Uinjilisti
Yupo Mwalim Mwakasege!

Kila Mtumishi anahudumu kadri ya Kipaji ambacho Mungu kampa, Wapo Wainjilisti Wazuri sana, lakini hawana Huduma ya Unabii!!!

Dunia ya leo Watu wanataka Majibu ya Matatizo yao, Kwa vile Mungu ndo anasamehe Dhambi!!

Binadamu huna haja ya kuhukumu!

Mimi nikiona Mtumishi wa Mungu ambaye Mungu anamtumia kusaidia watu, Nafurahi Moyoni na kumtukuza Mungu!!!
 
Leta historia ya Moses Kulola hapa na maswahibu aliyokutana nayo mtumishi tujifunze...


Maana kule kawe mtume alipitia maswahibu ya kuuza matenga ili anunue raba mtoni.
Alipigwa na askari ambae SAwa na mwanae ndio ikawa chanzo cha kifo chake. Alifungwa sababu ya injili.
 
Huyo Moses Kulola kuja kumshinda Diana Bundala kwenye uinjilist May be aende direct mbingun kusoma gospel ndo aje ashindane. Yule mama ni shindikanaa coz yeye mbingun anaendaga daily
 
Huyo Moses Kulola kuja kumshinda Diana Bundala kwenye uinjilist May be aende direct mbingun kusoma gospel ndo aje ashindane. Yule mama ni shindikanaa coz yeye mbingun anaendaga daily
[emoji23][emoji23]
 
Wengi sasa hivi wamekua ni wafanya biashara nawaita "wajasiliadini" kazi kuuza maji ya upako mafuta, sabuni, mara dawa za meno za upako na takataka zingine nyingi, makanisa machache yamebaki kuisema ile kweli ya Mungu na kuambia watu watubu dhambi zao
Na wasingetokea kama ilivyo tabiriwa, biblia Ingekuwa ni kitabu cha uongo
 
Na pia hautamsikia mwamposa akisema watu watubu dhambi, nakubaliana na
mleta maada,na si mwamposa tu siku hizi mafundisho ya Toba yamepotea sana , Kila mtu anazungumzia miujiza na mafanikio ya kimwili zaid
Mtu elimu hana connection hana anaambiwa toa sadaka ya kujimaliza kesho utapigiwa simu na mtu usiyemjua utapewa pesa usizozitegemea na lenyewe kama zuzu linaitikia amen amen!

Tanzania hii itokee siku hela zitoke kusikojulikana?hivi tu zinatafutwa kwa force hazionekani halafu utegemee kuitikia amen na kushinda Kanisani ndo zitakuja?stupid kabisa acha waendelee kuibiwa
 
Back
Top Bottom