Tanzania inabidi ijifunze namna ya kuendesha nchi na kuleta maendeleo kwa muda mfupi kutoka China

inabidi tujifunze mambo mbalimbali ya faida kutoka Chiina
Huko kujifunza ndiyo mlango mwingine wa ufisadi. Tangu tupate uhuru wametumwa wataalamu nchi mbalimbali duniani kwenda kujifunza lkn hakuna jipya.

*Unakumbuka ishu za Kilimo Kwanza?
*Ubakumbuka ishu za BRN ?
*Unakumbuka maandalizi ya uchumi wa gesi ya kule Mtwara?

Pesa ilipigwa ktk haya mazingaombwe na nyimbo nyingi ziliimbwa kwamba Sasa umaskini wa nchi kwisha kabisa
 
Uko sahihi mkuu . Tufanye nini kukomboa taifa letu ?

Maana kilimo kwanza chali, serikali ya viwanda chali hatueleweki tupo upande gani ?
 
Wazo lako ni zuri kuhusu tozo kuwa na “mfuko wake” .
 
Ulifeli kwa sababu nyie ni mazezeta sio ujamaa wala ubepari utakao faulu kwenu mazezeta msiokuwa hata na punje ya akili timamu.
Ubepari ni mzuri ila unazaa gepu kubwa sana baina ya walionacho na wasionacho!

Ujumaa ni mzuri kwani unapunguza matabaka ya alienacho na asionacho yaani gepu linakuwa si kubwa ni la ahueni.

Zaidi ya 80% ya watanzania ni masikini. Tulikuwa millioni 60 sijajua kwa sensa ya sasa hivi idadi itakuwa ni ya kiasi gani.

Ikiwa zaidi ya 80% ya 60,000,000 ni masikini itakuwa ni bora zaidi ikatafutwa namna ya kuwainua hawa wote kwa wakati mmoja.

Pengine itafutwe namna ya kukuza uchumi. Pengine itafutwa namna ya kukuzwa uchumi wa raia wote kwa pamoja.

Sijajua ila ni pengine! Nimewaza tu!
 
Wakati mwengine nafikiri inatubidi baadhi ya desturi ziwekwe chini kwa mfano: Tamaduni zetu kumkosoa mkubwa hata kama kwa staha utakumbwa na tatizo.

Nachelea kusema ila viongozi wenye mamlaka ni tatizo kuu! Ukijaribu kuweka mambo sawa ni tatizo.

Nakumbuka baba yangu aligawa mabati kwenye shule fulani baada ya kuona mazingira ya hiyo shule hayapo vizuri, mbunge wa hilo jimbo akahisi Mzee anajiandaa ili achukue kiti chake.
 
Sahihi tukisema tufuate ubepari 100% watu watalia humu TZ inabidi tuchanganye mazuri ya Ubepari + Ujamaa.
 
Sahihi tukisema tufuate ubepari 100% watu watalia humu TZ inabidi tuchanganye mazuri ya Ubepari + Ujamaa.View attachment 2351228
Yap! Nakuunga mkono.

Uzuri tupo ndani ya zama ambazo manufaa na kufeli kwa mifumo kupo wazi. Ni zama za ushahidi ya mifumo ipi inafaa kuendesha nchi kwa muktadha wa maendeleo ya raia mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Yaani kila kitu kipo mbele yetu tumeshuhudia na tunashuhudia. Hivyo, kusonga mbele au kujididimiza yatabakia ni maamuzi ya nchi yenyewe binafsi.

Tatizo tuna viongozi wajinga. Na ujinga ni mbaya na ndiyo maana ikasemwa; ni bora uwe na adui aliye serious kuliko rafiki aliyemjinga.
 

Unafikiri Kuna mtu angelalamika kama huduma za afya, elimu na jamii Kwa ujumla zingeboreshwa? Shida ni pale unakamuliwa tozo na Bado inabidi ukalipie huduma za muhimu huku mnashuhudia tozo zinavyotafunwa bila huruma.

Huduma zingekua nzuri hata wakate nusu ya mshahara achilia mbali hivyo vi tozo, hakuna mtu angepiga kelele.
 
Tatizo la Tanzania ni wananchi wala sio viongoz. Huwez kubadilisha mtu ambae hajaamua mwenyewe kubadilika. Discipline ya watu wa Asia na cc kifo na usingiz.
 
SAsa mbona mnalalamika chumba kujengwa kwa milioni 11
 
Kweli kabisa.
 
Magufuli alikua anajaribu kuwashtua kidogo watu wafanye kazi lakini kilichomkuta sisi wote ni mashahidi.
 
Tatizo la Tanzania ni wananchi wala sio viongoz. Huwez kubadilisha mtu ambae hajaamua mwenyewe kubadilika. Discipline ya watu wa Asia na cc kifo na usingiz.
Kweli mkuu, kuna shida mahali juu yetu Mao Zedong anaonekana ni dikteta Ila kuna kitu aliwa jenga wachina kilicho kuwa na manufaa sana na ndio maana hata alipoiacha China baada ya kufa na kuingia Deng Xiaoping hakupata shida Sana kuwa badilisha wachina bali aliongoze vichache tu na nchi ikapepea kwenda mbele shida yetu inaanzia awamu ya kwanza kabisa kuna kitu Mwalimu haku kazia kwetu kitu amabacho watawala wa mwanzo wa nchi za mashariki mwa Asia walifanya baada ya kupata Uhuru wao.
 
Nawaza inbox; Hivi kwanini nchi hii tusimtafute expart aje awe raisi na ikiwezakana aje pia na baraza la mawaziri kwa japo miaka 10 tungefika mbaali sana.

Hiyo niliwahi kuandika hapa.

Yaani tuingie makubaliano na consultant firm waje na management Yao Kila kitu sie tubaki kufanya mambo mengine.

Mkataba uainishe hadidu rejea, maendeleo Gani na Kwa kiwango kipi tunataka, baada ya hapo wao watasimamia ukusanyaji wa mapato, mipango ya maendeleo, uwekezaji, huduma za kijamii n.k

Hatutakuja Tena na bajeti ya ma Vieite ya wabunge na mawaziri ( Consultant itakua juu yake na atabana matumizi apate faida) huku alileta tija Kwa taifa.
 
Nenda Korea Kaskazini kwenye ujamaa ulione gap la kutisha zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…