Tanzania inatarajiwa kuingia mkataba na Kampuni ya DP World ya Dubai kuendeleza bandari ya Dar es Salaam
Kwani CARDLESS ana maoni gani? Maana asubuhi alikuwa anatuchamba humu wale wote ambao hatujasomea uchumi.

Kwa hiyo hao akina Msukuma na Lusinde ndiyo wachumi wenye sifa ya kuliongelea hilo sakata, au!!
 
Kweli CCM mmeishiwa mbinu suala nyeti kama hili mnatuletea msukuma na lusinde kubwabwaja kuhusu suala la bandari, nimeshangaa kwerkweri.

Mnaona watanzania ni wajinga wajinga katika mambo ya msingi , binafsi nimekasirika na kusikitika sana baada ya kuona hayo. Yaanii lusinde na msukuma watu convice sisi kuhusu suala la bandari?
shame on you
Badilisha andika Bandari! Kabla ya kuandika acha mihemuko spelling error kibao
 
"Black people are not complete human beings because they don't have good brain to govern the society as white people are. They are still under the process of becoming the complete human beings". Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
Nimeipenda hii aisee [emoji848][emoji848]
 
Mtake msitake lazima Mwarabu apate hii tenda! Kwani Mchina alishapigwa chini au mnataka mnyaturu!!!
 
"Black people are not complete human beings because they don't have good brain to govern the society as white people are. They are still under the process of becoming the complete human beings". Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
We do not pretend like other Whites that we like Blacks. The fact that, Blacks look like human beings and act like human beings do not necessarily make them sensible human beings. Hedgehogs are not porcupines and lizards are not crocodiles simply because they look alike.

Pretending is cursed sin.
 
Kukusomesha wewe mpaka ukafika hatua ya kuweka maoni yako humu yakasomwa na umma wa watanzania.
Hizi ndiyo mentality za wazee wa kule kweusi 1960s,mnadhani kila mtu alikula shayiri shuleni, na kupewa wino wa kuandika. Mnadhani kila mtu kasomeshwa.

Wazazi wetu wametoka jasho kutulipia Ada. Wazazi wetu walishindwa hata kununua bati moja ili sisi tusome.

Kwamba mikataba ikija na terms za kipumbavu tusaini tu kwasababu anaendesha bandari ya London na Southampton kule Uingereza.

Terms za London na za kwetu zinafanana?

Mnawaandalia Waarabu na vizazi vyao maisha mazuri kwa miaka 100 huku vizazi vya kitanzania vinataabika kwa miaka 100.

Nchi ya wapuuzi Hii!
 
Hizi ndiyo mentality za wazee wa kule kweusi 1960s,mnadhani kila mtu alikula shayiri shuleni, na kupewa wino wa kuandika. Mnadhani kila mtu kasomeshwa.

Wazazi wetu wametoka jasho kutulipia Ada. Wazazi wetu walishindwa hata kununua bati moja ili sisi tusome.

Kwamba mikataba ikija na terms za kipumbavu tusaini tu kwasababu anaendesha bandari ya London na Southampton kule Uingereza.

Terms za London na za kwetu zinafanana?

Mnawaandalia Waarabu na vizazi vyao maisha mazuri kwa miaka 100 huku vizazi vya kitanzania vinataabika kwa miaka 100.

Nchi ya wapuuzi Hii!
Wanaosaini wanatafuta pesa ya kodi itakayosomesha watoto wako leo na kesho. Pesa itakayolipia bima za raia walipa kodi kwa miaka mingi ijayo.

Hakuna serikali yenye nia ya makusudi ya kuuza rasilimali za taifa, haipo serikali hiyo.

Ni uboreshaji wa uzalishaji, ni utafutaji wa pato zaidi kwa njia za kodi, pia ni uongezaji wa ufanisi kwa ujumla, unaoendana na mahitaji ya muda.

Tujue kwanza kwa kina nini kinachokusudiwa na kwanini ndio tuwe na uhalali wa kupiga makelele mitandaoni.
 
Uchumi wa Dubai kutegemea bandari Ni hisia!.

Bandari ya Bagamoyo kumeza mizigo inayopitia Dubai na Dubai kukosa mapato Ni hisia!

Hivi ndivyo kenge alivyo , ukilipiga mpaka litoke damu Ndiyo litakimbia.

Sijui Nani katuloga.


Kwamba ikija mikataba YENYE terms za kutuangamiza tusaini tu.

Strategy ya bandari ya Bagamoyo unaijua, uliisoma vizuri!
 
Umeandika mengi na ni hisia zako, japo unaruhusiwa kuwa nazo kama mimi ninavyoruhusiwa kuwa na zangu.
Nani asiyeyajua maandiko yako humu ya kulamba miguu?

Sijayaona mawazo chanya uliyonayo kuhusu hili.

Na hapa najua uko kazini kuhusu hili swala la bandari. Kuhakikisha unawatoa watu kwenye HOJA.

Hovyoo!
 
Seems hata bandarini kwenyewe toka uzaliwe hujaingia
Kwamba wanaoongea humu lazima wawe walishaingia bandarini.

Logic yako Ni kwamba Kama hujawahi kuingia bandarini huna Cha kuchangia.

Nafuu Hata mangungo alikua hajui kusoma!
 
Nani asiyeyajua maandiko yako humu ya kulamba miguu?

Sijayaona mawazo chanya uliyonayo kuhusu hili.

Na hapa najua uko kazini kuhusu hili swala la bandari. Kuhakikisha unawatoa watu kwenye HOJA.

Hovyoo!
Kuwa mzalendo sio lazima upingepinge hovyo tu. Natazama mantiki nzima kabla sijaandika mchango wangu wa mawazo.

Tutafute kwanza elimu pana ya huo uwekezaji hapo bandarini kabla hatujanaswa na mtego wa kupinga tusichokijua.

Tutafute uelewa mpana kwanza kabla hatujaruhusu mapovu yakatutawala wakati wa kuandika maoni yetu.
 
Lete suluhisho mtoa mada, mm nashauri tuingie barabarani kujificha nyuma ya key hakutabadili kitu
Suluhisho Ni kuangalia mikataba ya waliofanikiwa Ina terms za Aina gani na Sisi tukapita humo humo kwa maslahi mapana.

Hawa Waarabu wanajua Waafrika Hata sahani ya wali wanaweza kukupa bandari yote.

Hebu ona CCM wamewatuma Msukuma na Lusinde kuja kushawishi umma. Na Hawa Hawa ndiyo walienda Dubai kwa ofa. Darasa la Saba ambao Hata lugha yenyewe Ni shida.
 
Kuwa mzalendo sio lazima upingepinge hovyo tu. Natazama mantiki nzima kabla sijaandika mchango wangu wa mawazo.

Tutafute kwanza elimu pana ya huo uwekezaji hapo bandarini kabla hatujanaswa na mtego wa kupinga tusichokijua.

Tutafute uelewa mpana kwanza kabla hatujaruhusu mapovu yakatutawala wakati wa kuandika maoni yetu.
Hivi Wewe uko humu halafu hujui watu wanapinga Nini!

Duuuh! hili nalo Ni ajabu la Tisa la dunia.
 
Back
Top Bottom