Tanzania iwe upande gani Kama Ethiopia na Misri zinapigania maji ya mto Nile?

kwa hatua walitofikia sioni mwenye uwezo wa kuwazuia Ethiopia
 
Egypt wanajiona kama wakoloni. Hawatufai. Hata5kutoa maji Ziwa Victoria wanang'aka.

Ethiopia ni wenzetu zaidi. Ni moja ya nchi zilizokuwa upande wetu wakati wa vita dhidi ya Iddi Amin.

Tunajua Egypt wapo kwenye kwenye ujenzi wa bwawa la Stieglers.
 
Kwani nani aliipangia Tanzania kuwa mmiliki wa mlima Kilimanjaro.
Nani aliipangia Tanzania kumiliki eneo kubwa la maji ya ziwa Victoria na Kenya iwe na eneo dogo, kwanini wasigawane asilimia sawa na Uganda.
Kwanini Rwanda, Burundi nao wasiwe na eneo la ziwa.
Kwanini Uganda wapo landlocked wakati Tanzania ina bandari kama tatu.
Kwanini DRC iwe kubwa sana na yenye mali nyingi wakati Rwanda na Burundi ni ndogo na hazina maliasili.

Hayo maswali na mengine mengi yanafatia kwenye swali lako.
Misri ndo hakujipangia mipaka yake. Waliopanga matumizi ya maji ndio waliopanga mipaka ya Tanzania. Mbona sisi tulipigana na Iddi Amin alipotaka kuibadilisha?
Kenya wakisema Kilimanjaro ni ya kwao utatumia vigezo gani kusema si yao ni ya kwetu. Utatumia vigezo vilevile ambavyo Misri wanatumia, MKATABA. Na nchi zote za Afrika zilikubaliana kuheshimu mikataba ya kugawana milki. Hata sisi Tz na Malawi tunagombea ziwa Nyasa, kitakachofanyika ni kusoma na kutafsiri mkataba unasema ziwa linagawanyika kivipi.
 
Kwa hio yeye pekee ndie mwenye haki ya kuwanywesha wananchi wake wote zaidi ya milioni 100 maji ya mto nile, ila sisi tulivyotaka kupeleka mradi wa maji ya kunywa dodoma tokea ziwa victoria alitujia juu na kutuzuia?
Kwenye mto huo huo yeye amejenga bwawa kubwa Aswan la kuzalisha umeme hakuna mtu aliyemuuliza, ila kitu hicho hicho Ethopia anataka kufanya anampiga marufuku.
Mwambieni huyo Mmisri kua mimi nimeshaamua kama yeye hataki watu wengine wanywe maji ya mto Nile basi pia awakataze na wananchi wake kunywa hayo maji, na pia kama hataki wengine watumie maji ya mto Nile kuzalisha umeme basi na yeye pia aache mara moja kuzalisha umeme kupitia maji hayo ya mto Nile.
 
Brother Armata kiuhalisia upo sahihi, lakini ukifuatilia watu hawapingi Misri kutumia Mto Nile bali wanapinga Misri kutaka kutumia mabavu na kuweka zuio na kuingilia suala la taifa jingine.

Misri itumie diplomasia kutatua suala, iketi meza moja na Ethiopia wakubaliane huyu maji atapata vipi na huyu umeme atapata vipi, basi hakuna la ziada.
 
Wakenya ni majuha usishangae wapo upande wa Misri,,
 
Sijakuelewa labda unisahihishe umesema Ethiopia ni chanzo kikuu cha mto nile,kivp wakati tunajua souce kubwa ni ziwa victoria
 
Na hii program ya kupeleka maji ya Victoria mjini Dodoma makao makuu ya nchi, siku moja nasi tutatunishiwa misuli na hao washenzi.

Ninakumbuka Wakati wa Lowasa akiwa waziri wa maji alipoanzisha kampeni ya kuvuta hayo maji kuyaleta Shinyanga, hao washenzi walianza kuleta ngebe, lakini sikuelewa kilichoendelea baadaye!
 
Misri katumia ubavu gani kama wameita majadiliano na Ethiopia kagoma kushiriki. Mabavu gani yametumika wakati wanakaribisha mjadala mezani. Kuna mwanajeshi wa Misri kalipua bwawa, au lini wametishia kutumia jeshi.

Kwanza Misri alishabadili msimamo wake kwenye mjadala uliopita. Aliomba maji yajazwe kwa hatua, Ethiopia inataka kuyajaza kwa mkupuo jambo la hovyo kabisa. Pia Misri aliomba maji yasihamishwe mkondo maana yatapungua kwenye channel. Sasa ng'ang'ania alafu watumie jeshi uone Ethiopia anavyokaa asubuhi na mapema. Kwanza hakuna hata ya kupigana direct, kuna kabila la Wahoromo wakipewa silaha wanapigana wenyewe na serikali yao.
 
Vita kwa ajili ya maji haiko mbali, chanzo halisi cha mto Nile ni Lake Victoria. Time will tell
 
Oke, mie nawaombea amani, utulivu na kunufaika mto Nile.
 
Sijakuelewa labda unisahihishe umesema Ethiopia ni chanzo kikuu cha mto nile,kivp wakati tunajua souce kubwa ni ziwa victoria
Hata maji ya ziwa Victoria Kuna pahala yanakotoka, lakini Kuna white Nile na blue Nile ambayo inakutana pahala na kutengeneza Nile inayokwenda hadi Misri. Blue ndiyo inayochangia maji mengi kwenye Nile watanisahihisha Wana geography. Blue Nile inatoka Ethiopia/Eritrea huko
 
Nimeimeza kama ilivyo nitaipeleka kijiweni huko nionekane mtaalam.

Nitasimulia kila kwenye kilinge hadi ikae kichwani.

Salute kwako.
 
Maji ya Nile lazima yaje kuleta kizaazaa kikubwa. Inasemekana Vita ya tatu ya dunia itakuwa Ni kugombania maji.

Hata Israeli ilitakaga kuwaadhibu waarabu kwa kuugeuza uelekeo wa maji ya Nile kuingia bahari ya Hindi kupitia shinyanga singida, Dodoma, morogoro hadi bahari ya Hindi.

Lakini pia Ni rahisi kuweka sumu kwenye maji yanayokwenda kwa waarabu kutokea Ethiopia na nchi nyingine za bonde la Nile
 
Geographic location ya Ethiopia iko vizuri kivita dhidi ya Egypt.
 
Blue Nile inatoka Ziwa Tana, Ethiopia ni mchango kwa Greater Nile kwa asilimia 24, White Nile ni mkanganyiko inaweza kuanzia Ruvyironza, Nyabarongo (Rwanda x Burudani) na Mto Kagera kuelekea Ziwa Nyanza (Victoria) na kuanza safari kueleke Jinja, Juba hadi Khartoum kuungana na Blue Nile kutengeneza Greater Nile.

Chanzo cha Ziwa Nyanza (Victoria) ni mito mingi katika uwanda wa bonde la ufa kuu upande wa magharibi ya Afrika Mashariki (Kanda ya Ziwa Nyanza, Kusini Uganda, Rwanda na Burundi).
 
Mzee kwani mipaka ya nchi zetu tuliiweka sisi? Mbona Ni wakoloni haohao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…