Tanzania kuendesha mnada wa vitalu vya uwindaji; wawindaji kuruhusiwa kuua Tembo, Simba na wanyama wengine wazee

Tanzania kuendesha mnada wa vitalu vya uwindaji; wawindaji kuruhusiwa kuua Tembo, Simba na wanyama wengine wazee

Huu ni unafiki,tembo wanakufa kila siku kupitia majangili na serikali kukosa mapato

Sasa serikali imeweka njia rasmi, bado unapinga
Majangili ni zama za nyerere hukoooo!!!wewe unaishi wapi??.....wkt nchi haina watu.....siku hizi kila mita tano kuna satelite zinazungumza na jangili kwa kumpa onyo...asithubutu kuua mnyama tena zinamwambia kabisaaa " wewe flani picha yako tunayo na unaishi paleeee!!....sasa endelea uone......
 
Hiyo lugha ndio inakuchanganya? Kwamba hapo awali Tanzania ilikuwa na simba 100,000, pamoja na hizo nchi zingine nazo kila mmoja awe na simba 100,000 kila moja, sasa katika kipindi cha miaka 50 wauwawe kwenye kila nchi kiasi Tanzania wabaki 10,000 tu toka laki 1, na kwenye nchi zingine wabaki 5,000 ; 2,000 ; na kwengine 1,000. Sasa kwamba Tanzania ndio wamebaki wengi kuliko huko kwingine ndio inamaanisha kwamba hawajapungua?! Kutoka laki 1 hadi elfu 10 we unaona hawajapungua?
 
Simba na Tembo ni endangered species, hakuna any quota unaweza kumpa mtu ili auwe, na kwa rushwa ilivyotapakaa hatuna sababu ya kuamini kwamba watafuata hiyo quota, maana wako hatarini.
Tunajua kwamba simba na tembo ni endangered species, lakini bado huwa wanapewa thamani zao katika uwindaji. Unakumbuka kesi ya yule simba Cecil aliyeuwawa Zimbabwe na muwindaji Mmarekani? Alilipia $50,000 na kupewa kibali.
 
awamu hii ni ya mafisadi na tena ni walafii kweli kweli, wanacho taka ni kuwahangamiza wanyama pori woote ili tanganyika iwe sawa na zanzibar, mbona hiyo minada yenu haram haikuepo enzi za magufuli ?
 
Kwahiyo unataka ufuge hao simba wanaliwa nyama? Unadhani yule faru rajabu au babake faru John wangeuzwa wakiwa hai si tungepata hela?
Kwa hiyo haya Mambo ya kulinda sijui Ikolojia na hifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo kumbe ni unafiki mtupu??

Kwa mantiki hii basi majangili waruhusiwe, wawe wanatozwa Kodi tu, hela iingie, ama vipi?
 
Kwa hiyo haya Mambo ya kulinda sijui Ikolojia na hifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo kumbe ni unafiki mtupu??

Kwa mantiki hii basi majangili waruhusiwe, wawe wanatozwa Kodi tu, hela iingie, ama vipi?
Unajua maana ya jangili?
 
Mwaka 2019/2020 serikali ilianzisha mabucha ya wanyama pori sijui napo unasemaje.

Uwindaji haujaanza leo ,ni biashara ya kitambo na Kwa sasa wanyama wamekuwa wengi kupita kiasi.

Wanyama kama viboko na mamba wanatakiwa kupunguzwa kwa kiasi kikubwa maana wanahatarisha maisha na kuharibu Mazao.
Ila mkuu hapo mbona wameandika Simba na tembo pia wanauawa..

Mimi Sina shida na uwindaji, lakini Kama wanyama Hawa Hawa tunaopiga kelele kuwa wamepungua sana na wanaweza kuingia kwenye kundi la waliopo hatarini kutoweka, Kisha wanawindwa? Hata Kama ni 'wazee' kweli?
 
Ila mkuu hapo mbona wameandika Simba na tembo pia wanauawa..

Mimi Sina shida na uwindaji, lakini Kama wanyama Hawa Hawa tunaopiga kelele kuwa wamepungua sana na wanaweza kuingia kwenye kundi la waliopo hatarini kutoweka, Kisha wanawindwa? Hata Kama ni 'wazee' kweli?
Wala hawajapungua kwa kiwango kinachoelezwa.

Kwa hali ya Sasa ni wamezidi uwezo wa hifadhi na kuhatarisha maisha ya watu.
 
Tunajua kwamba simba na tembo ni endangered species, lakini bado huwa wanapewa thamani zao katika uwindaji. Unakumbuka kesi ya yule simba Cecil aliyeuwawa Zimbabwe na muwindaji Mmarekani? Alilipia $50,000 na kupewa kibali.
Kwa kusema tu kwamba, unafahamu kwamba hao wanyama ni endengared species ila bado unataka wauwawe kwa manufaa ya pesa tayari inatia shaka ya afya yako ya akili.
 
Wala hawajapungua kwa kiwango kinachoelezwa.

Kwa hali ya Sasa ni wamezidi uwezo wa hifadhi na kuhatarisha maisha ya watu.
Hao wanyama tunaambiwa kila siku wako hatarini kutoweka, hasa Tembo na Simba, wewe unasema hawajapungua sana, ulitaka wabaki 10 au 20 kama wale Faru weupe ndio ujue wamepungua? Tuwe na busara kidogo kuliko tamaa ya pesa
 
Hao wanyama tunaambiwa kila siku wako hatarini kutoweka, hasa Tembo na Simba, wewe unasema hawajapungua sana, ulitaka wabaki 10 au 20 kama wale Faru weupe ndio ujue wamepungua? Tuwe na busara kidogo kuliko tamaa ya pesa
Umefuatilia maelezo Tanapa? Ishu ya kutoweka ni lazima watoweke ni suala la muda tuu.

Hata binadamu wa awali walikuwa madubwana nao walitoweka.
 
Umefuatilia maelezo Tanapa? Ishu ya kutoweka ni lazima watoweke ni suala la muda tuu.

Hata binadamu wa awali walikuwa madubwana nao walitoweka.
Unaonaje uuwawe leo, maana kufa utakufa tu, sasa kwanini tu usiuliwe leo tuokoe muda? We unaonaje eti?
 
Huu ni unafiki,tembo wanakufa kila siku kupitia majangili na serikali kukosa mapato

Sasa serikali imeweka njia rasmi, bado unapinga
Yaani hii jamii ya Tanzania ni ya kuoonea huruma kaka? Una tembo wazee, Simba wazee na wanyama wengine wazee then jamii inayozunguka wanyama hao hawana hata maji. Then mtu mwenye akili anaweka uhalali wa "kuvuna" wanyama hao ili jamii husika wapate maji yeye hataki? Kuna maana gani kuwa na Nyati milioni moja halafu unakufa kwa kukosa maji safi au Huduma nzuri za afya?
 
Back
Top Bottom