Tanzania kupokea zaidi ya wawekezaji 300 kutoka nchini Misri

Tanzania kupokea zaidi ya wawekezaji 300 kutoka nchini Misri

Yaani washindwe kujenga hivyo viwanda 100 huko kwao Misri halafu waje kujenga hivyo viwanda hapa Tz?

Sijui nani katuloga watz.
Sema wamekuja Tz kuvuna kupitia mikataba hewa na viongozi wetu kupewa 10% zao kisha ufukara uendelee.
Barikiwa
 
Yaani wageni wafanyabishara unasema ugeni mzito?

Hao ni wafanyabishara wapambanaji wanaopambana kujiongezea utajiri, sio wakuwaonea huruma.... wewe ndio inabidi ujionee huruma maana wewe ndio mtaji,soko na nguvu kazi yao.
 
Serikali ya Tanzania tarehe 04/12/2021 inatarajia kupokea zaidi ya wawekezaji 300 kutoka nchini Misri ambao watawekeza nchini katika sekta za Usafirishaji, ujenzi, uzalishaji wa bidhaa za petroli, kilimo, kemikali, ujenzi na madawa...
Hao ni masikini wenzetu, watawekeza nini la maana? Haya bwana....
 
KAma ni kweli WAMISRI wanakuja kuwekeza wengi namna hiyo, basi mjue ni kwa makusudi kabisa tunauzwa utumwani. MAneno haya yawekwe kwenye kumbukumbu. HAwa hawa wamewaweka vijana wengi sana wa Kitanzania kitumwa majumbani mwao mjini Cairo. Hizi Balazi zetu sijui zinafanya kazi gani haki ya Mungu.

hebi fafanua, naona kama unachanganya Misri n Oman....wafanya kazi wengi wa ndani huwa wanakwenda Oman na ndio kwenye tabia hiyo.... Misri sidhani kama kuna tabia hiyo..
 
wasije wakawa akina YUTEK tu...

vyombo vya intelejensia kuweni macho sasa, tuna tatizo la watu wetu kujali kushibisha matumbo yao na kusahau majukumu yao kwa Taifa... wawekezaji wanaowekeza Tanzania wananufaika sana kwa kupiga superprofit huku wakiacha watanzania masikini...wanaenjoy sana kupata cheap labor na kutofuata taratibu makazini na kuishia kuumiza labor force yetu..
 
Baadala ya kupoteza muda na hawa wawekezaji tulipaswa kujengea uwezo watu wetu tuwekeze wenyewe na kujitegemea kuliko kuzalisha matajiri wa kihindi, kiarabu, kichina, kizungu na kituruki....tunapaswa sasa kuzalisha matajiri wakimakonde, kizanaki, kizaramo, kichaga, nk...

Serikali ifikiri sasa kuzarisha matycoon weusi kwa kujenga uwezo kwa watanzania kwa kuwapa elimu na kurahisisha upatikanaji wa mikopo... shusheni riba za mabank mpaka chini ya 5% na vigezo viwe rahisi vya mikopo kwa watanzania ili sasa tuwekeze wenyewe...
 
Hahahaaaa....... Umeshapanic.

Wangetoka Ubelgiji ungeshangilia!
Any developed country ukikaa nao vema kwa negotiation za win win utasonga mbele... negotiating team iwe na uzaendo maana nao "wabelgiji" wanatuhitaji sana for their survival. Lakini Misri sidhani kama has anything to offer! Kwao wanashida kama sisi
 
Baadala ya kupoteza muda na hawa wawekezaji tulipaswa kujengea uwezo watu wetu tuwekeze wenyewe na kujitegemea kuliko kuzalisha matajiri wa kihindi, kiarabu, kichina, kizungu na kituruki....tunapaswa sasa kuzalisha matajiri wakimakonde, kizanaki, kizaramo, kichaga, nk...

Serikali ifikiri sasa kuzarisha matycoon weusi kwa kujenga uwezo kwa watanzania kwa kuwapa elimu na kurahisisha upatikanaji wa mikopo... shusheni riba za mabank mpaka chini ya 5% na vigezo viwe rahisi vya mikopo kwa watanzania ili sasa tuwekeze wenyewe...
Umesema vizuri sana. Ukiangalia mabilioni ya pesa zinazolipwa makampuni ya nje kupitia ujenzi ni mengi sana. Serikali ingewezesha wazawa kufanya kazi hizo pesa ingebaki nyingi sana nchini na mzunguko ungekua mkubwa.

Wizara ya ujenzi ina budget kubwa sana lakini zaidi ya asilimia 80 inaenda nje. Chakushangaza watendaji wa hiyo miradi ni watz uongozi tu na mitaji ndio wageni.

Sijui hata tunakwama wapi? Tungechukua hata mfano wa kagame anayewekeza kwenye elimu na technology ili kupunguza wageni na kuongeza ajira kwenye maeneo hayo.

Hakika tawala zetu zinapaswa kuweka mikakati ya kuinua uchumi wa nchi na watu wake. Wataalamu nao wanapaswa kuisaidia nchi badala ya kujificha kwenye kichaka cha siasa.
 
Umesema vizuri sana. Ukiangalia mabilioni ya pesa zinazolipwa makampuni ya nje kupitia ujenzi ni mengi sana. Serikali ingewezesha wazawa kufanya kazi hizo pesa ingebaki nyingi sana nchini na mzunguko ungekua mkubwa...

Chief, hivi vitu vinahitaji vifaa na teknolojia tu, wapo vijana wengi wa kitanzania wanaweza kufanya uwekezaji mwingi tu hapa na kutoboa tatizo wengi wanafeli hawana mitaji wala access ya kupata hiyo mitaji.

Mfano: ujenzi wa mabarabara haya unahitaji vifaa na watalaam, vifaa vipo vinanunuliwa ni hela yako tu, watalaam wapo unaweza kuajili kwa gharama nafuu kutokea huko huko China na India na baadhi wabongo hapa...Shida riba za mabank zipo juu na access ya fund kwa namna nyingine hazipo matokeo yake ndio wanakuja wahindi, wachina na waarabu wenye muscles wanachukua hiyo miradi na kupiga hela huku wabongo wakibaki kuwa cheap labor.

Serikali ilipaswa sasa kuwekeza kwa watu wake kiteknolojia na mitaji ili hela ibaki hapa na watu wake wenyewe wawe wamiliki wa makampuni makubwa na kuzungusha hizi hela hapa hapa.
 
Chief, hivi vitu vinahitaji vifaa na teknolojia tu, wapo vijana wengi wa kitanzania wanaweza kufanya uwekezaji mwingi tu hapa na kutoboa tatizo wengi wanafeli hawana mitaji wala access ya kupata hiyo mitaji...
Same language! I salute you comrade.
 
hebi fafanua, naona kama unachanganya Misri n Oman....wafanya kazi wengi wa ndani huwa wanakwenda Oman na ndio kwenye tabia hiyo.... Misri sidhani kama kuna tabia hiyo..
Nakufafanulia kuwa ninamaanisha Egypt! Sijakosea kitu, nimekaa kule miaka michache tu iliyopita ninachokiongea siyo cha kusikia. Pia ningependa kukusisitizia kwamba wa Misri tabia na mila zao zinafanana saana na nchi za Kiarabu, kwahiyo usishangae hata kidogo kusikia wanayafanya yanayofanyika huko Oman, UAE nk.
 
Nakufafanulia kuwa ninamaanisha Egypt! Sijakosea kitu, nimekaa kule miaka michache tu iliyopita ninachokiongea siyo cha kusikia. Pia ningependa kukusisitizia kwamba wa Misri tabia na mila zao zinafanana saana na nchi za Kiarabu, kwahiyo usishangae hata kidogo kusikia wanayafanya yanayofanyika huko Oman, UAE nk.

hiyo ni ngeni kwangu, naona mabinti wengi wanamiminikaga Oman...hii ni mpya kumbe na Misri pia wanakwenda....asante kwa ufanunuzi...kifupi muarabu ni muarabu tu haijalishi katoka wapi wote tabia na fikra ni zile zile tu...mwafrica kwao ni mtumwa na ni haki yao kumfanya chochote kile...
 
Chief, hivi vitu vinahitaji vifaa na teknolojia tu, wapo vijana wengi wa kitanzania wanaweza kufanya uwekezaji mwingi tu hapa na kutoboa tatizo wengi wanafeli hawana mitaji wala access ya kupata hiyo mitaji.

Mfano: ujenzi wa mabarabara haya unahitaji vifaa na watalaam, vifaa vipo vinanunuliwa ni hela yako tu, watalaam wapo unaweza kuajili kwa gharama nafuu kutokea huko huko China na India na baadhi wabongo hapa...Shida riba za mabank zipo juu na access ya fund kwa namna nyingine hazipo matokeo yake ndio wanakuja wahindi, wachina na waarabu wenye muscles wanachukua hiyo miradi na kupiga hela huku wabongo wakibaki kuwa cheap labor.

Serikali ilipaswa sasa kuwekeza kwa watu wake kiteknolojia na mitaji ili hela ibaki hapa na watu wake wenyewe wawe wamiliki wa makampuni makubwa na kuzungusha hizi hela hapa hapa.
Hii nimeipenda. Na zaidi ya hapo mswahili akiwa na uwezo wa kuwekeza, huo uhuni, utapeli, vikwazo na ulaghai atakaofanyiwa, tozo kuongezwa viwango atakaofanyiwa ataishia kufilisika. Kwanza TRA huwa wanafika wanaanza kukukadiria hata kabla hujaanza kazi na wanataka ulipe kwanza. Nchi yetu hatupendani!
 
hiyo ni ngeni kwangu, naona mabinti wengi wanamiminikaga Oman...hii ni mpya kumbe na Misri pia wanakwenda....asante kwa ufanunuzi...kifupi muarabu ni muarabu tu haijalishi katoka wapi wote tabia na fikra ni zile zile tu...mwafrica kwao ni mtumwa na ni haki yao kumfanya chochote kile...
sasa umenielewa, na sasa tunawakaribisha huku huku. Nakuhakikishia watatuvua nguo! Nina hakika huu mpango umetokana na wao kupewa ule ujenzi wa Sigglers Gorge- mtambo wa kufua umeme, wameleta watu wao sasa wameshatengeneza upenyo mpaka ikulu. Ni watu corrupt sijapata kuona mfano! Hapo ninakuhakikishia ni sawa na kumkaribisha shetani kuishi naye ukidhania anayo nia ya kukufundisha kuwa Padre au Imam. LAZIMA TAIFA ZIMA LITASIKITIKA muda si mrefu. Ni afadhali ya waChina mara elfu moja. Tena nasikia hao hao wameshaanza michoro ya kushika eneo kubwa tu la Ardhi maeneo fulani Mkoa wa Tanga. Angalia hotuba ya Prof. Lumumba Addis Ababa aliyotabiri kuwa kwa mwendo huu Africa iko mbioni kurudi utumwani miaka 25 ijayo!
 
Back
Top Bottom