Tetesi: Tanzania Kuwekewa vikwazo vya kiuchumi

Dhahabu ya Tanzania kupitia Acacia counts nothing in US or UK economy. Google production/exports za dhahabu Duniani.

Dhahabu yetu yote (jumlisha na ya makampuni mengine), haifikii hata 25% ya dhahabu inayochimbwa ndani ya US, Canada, Australia, Brazil au China.
 
Tuwekewe vyote tu.
 
Hii Habari ni uongo mtupu. Ni propaganda za gazeti la East African la Kenya kuichafua Tanzania na sijui wanafanya kwa maslahi ya Nani au ni Nani amewatuma
Kenya hawajawahi kuwa raiki wa Tanzania. Ndo maana hata EAC inayumba kwa kukosa partnership. Ni nchi ambayo inataka glorification kwa gharama yoyote ile na bahati mbaya baadhi ya wananchi wengi wa Kenya wameamini huo ndo mtindo wa maisha.

Naikumbuka Kenya waliposema mabaya juu ya TZ kule CITE ili pembe za faru na meno ya tembo yasiuzwe badala ya kujadiliana na TZ kama member wa EAC. Waliona ni powa lakini KIkwete aliposema matatizo ya amani nchini kwao akiwa US, wakatimuka na maneno meengi ya kulaani comment hiyo.
 
Naona dalili za kuihama hii nchi , Wacha nimalizie mambo yangu
 
hao hawana mwelekeo sasa wanampigia kampeni MEMBE
@ Esther, hili linaloendelea nchini kwetu ni zao la chuki. Ukitengeneza chuki na watu kwa kuwabagua na kuwatesa nk. Siku ukipatikana na mabaya kila mtu atafurahi. Mmeo akiwa msaliti ktk ndoa yenu,siku akishikwa ugoni utachukia kwa nini amefumani au utafurahi? Au mtaani kwenu kuna mchawi anawaulia watoto,anawafanya msiwe na amani hata usingizi hampati. Siku akifa utahuzunika? KILA ZAO LINA MBEGU NA PANDO LAKE, watu wana madukudu mioyoni kama ilivyokuwa kwa Mugabe alipopinduliwa kiaina watu walishangweka mitaani.
 
Mmm hizi akili hizi, hivi ni siasa ndo zinaondoa kale kauwezo ka kufikiri au shida ni nini, hivi unatakaje kuvuna pasipo kupanda, huo ustawi wa watu unakujaje pasipo maendeleo ya vitu, kwako unaona barabara nzuri, reli ya kisasa na ukarabati wa reli ya mkoloni sio kitu?
Huyu dawa yake ni kumfyekelea kule kama Gaddaff/unajua kajikita kwenye maendeleo ya vitu badala ya ustawi wa watu
 
Kirama,jibu kwanza niyomuuliza Esther, tuanzie hapo, kisha unijibu hili, UONGOZI UNABEBA MAJUKU GANI?
 
Kwangu hivyo vyote ni hopeless kabisa ! Inakuingia akilini kuwa na flyover huku ukipanda pale juu kwenye flyover ili ustaajabu uzuri wa hiyo flyover unaishia kutekwa na watu wasiojulikana,logic ya kuwekeza kwenye hiyo miundombinu huku hali ya usalama wa raia wake ni tete ni nini ? Mathalani yupo wapi Ben Saanane ili afaidi huu uwekezaji wa flyover? Sitaki kuorodhesha matukio yote nika relate na huu uwekezaji unaoendelea ambao hauna reflection kwenye ustawi wa maisha ya mtu mmoja mmoja ! Kama nchi tunachechemea kidiplomasia na mataifa makubwa ya nje huku wale wanaotukosoa tujirekebishe tunawaita wanatumika cjui hawana uzalendo,hovyo kabisa ! As a country we have lost a right flight direction in my opinion !
 
Think out of the box mkuu !
 
hivi unafikiri kila mwenye ubaya hana mazuri yake?
Ukumbuke si kila jambo likufurahishe wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…