Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

...nimeelewa vema kabisa mkuu.
 
3. Kumlipa mfanyakazi fidia ya mshahara wa miezi isiyopunguakumi na mbili.Pamoja na fidia hiyo,pia atalazimika kumlipa stahiki zake nyingine anazostahili kulipwa kwa mujibu wa sheria yoyote ile au makubaliano yoyote yaliyokuwepo kati ya muajiri na muajiriwa.

Kiongozi mkali kwanza.
Hapo kwenye hiyo "option" ya tatu. Ni muajiriwa wa muda gani inamhusu kwa maana ya time toka afukuzwe?

Je hata mimi wa mwez mmoja toka nifukuzwe kihuni inanihusu?

Natanguliza shukran mkuu
 
Nimemuuliza jamaa yangu mmoja aliyesomea Law kabisa kaniambia ujinga ukianza kufanywa hata kama ni siku mkuu sheria inakuwa applicable. Hata kama una masaa umefanyiwa haya mambo provided hawajafata sheria wewe ukifata sheria unapata haki zako mkuu.
 
Je mwajiri anaweza kukupangia kazi ambayo sio profession?Na kama uwezi kuhimudu na unamwandikia barua bado anakulazimisha ukaimu kazi ambayo uipendi toka moyoni na sio ya fani yako.Je katika hiki kikombe nikiepuke vipi?naomba msaada wa kisheria ndugu cc:deonova
 
Nimemuuliza jamaa yangu mmoja aliyesomea Law kabisa kaniambia ujinga ukianza kufanywa hata kama ni siku mkuu sheria inakuwa applicable. Hata kama una masaa umefanyiwa haya mambo provided hawajafata sheria wewe ukifata sheria unapata haki zako mkuu.


UBARIKIWE KIONGOZI (Mkali Kwanza)
 

Wewe ni mtumishi wa umma ama unafanya kazi shule za private mkuu?
 

Kikubwa hapa walifanya hivyo ili kuepuka kucreate madeni kwa watumishi, kumbuka Rais alishawaagizi watendaji wa chini (makatibu wakuu wa wizara na wakurugenzi wa halmashauri) kuepuka kucreate madeni mapya, hivyo kwa yale maagizo naona ndio walipokuja kutoa barua mpya zinazoonesha tarehe na mwezi uliyopewa barua na sio ile ya nyuma manake inge-create malimbikizo ambapo ni tofauti na maelekezo ya serikali, na kumbuka ktk kipindi hicho ndipo uhakiki ulikuwa unafanyika.

Lakini pia bado una haki ya ku-querry kwa Katibu Mkuu ktk wizara yako kwa ufafanuzi zaidi chief.
 

Kufanya kazi ambayo ni nje na ile Job Description yako, tena kwa kulazimishwa ama kwa kuwekewa sanction kwamba usipoifanya utapata adverse repercussions kutoka kwa mwajiri....kimsingi hii ndio tunaweza kui-term kama 'forced labour'

Tazama kifungu cha 6 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Namba 6 ya mwaka 2004; kinachokataza kazi za shuruti mahali pa kazi;

"For the purposes of this section, forced labour includes bonded labour or any work exacted from a person under the threat of a penalty and to which that person has not consented"

Na kimeeleza kabisa pale mwanzoni kuwa "Any person who procures, demands or imposes forced labour, commits an offence"

Hivyo katika case yako ni suala tu la kukusanya evidence na kuwasilisha either Ofisi ya Idara ya Kazi iliyo ktk mkoa ulipo wao kama Maafisa Kazi waliotajwa kwenye hiyo sheria watamfungulia mwajiri kesi, au pia unaweza kufungua mwenyewe case kwenye Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA).
 
Mkuu deonova ubarikiwe sana kwa msaada wako mkubwa unao utoa hapa

Mm nina tatizo kwenye ajira yangu imepita miaka miwili sasa toka nimejiunga na hii kampuni
Ninakatwa hela 10% ya mfuko wa hifadhi ya jamii PPF lakini sijaungwa ppf kwahiyo hizo hela haziendi ppf wala ppf hawanitambui

Je ikitokea nimeachishwa kazi au nineacha kazi ninaweza kulipwa hiyo pesa na mwajiri wangu?

Au ni hatua gani napaswa kuzichukua sasa hv maana maana kila nikimkumbushia mwajiri kuhusu hili anasema ana lishughulikia lakini hamna matokeo chanya...

Naomba msaada kwenyehili
 

Pole kwa hilo mkuu, je una kadi ya uanachama ya kwenye huo mfuko wa PPF?
 

 


 
Pole kwa hilo mkuu, je una kadi ya uanachama ya kwenye huo mfuko wa PPF?
Ndio kadi ninayo lakini nilijiunga nikiwa kwa mwajiri wangu wa zamani ambae alikuwa anaiingizia michango ppf vyema
baada ya mwajiri wangu wa zamani kusitisha ajira yangu.

Ndipo nikaingia kwa huyu mwajiri wangu mpya nikampa na namba yangu ya uanachama ya ppf ili awe anaingiza michango yangu huko. Lakini hakufanya hvyo

Kwahiyo ppf hawamtambui huyu mwajiri wangu mpya
 

Upo mkoa gani chief?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…