Basi Nenda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 20,774
- 47,866
SGR inaelekea Chato?
haiwezi kwenda inatoka Mwanza mpaka Dar
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
SGR inaelekea Chato?
Kuna tatizo Jaduong?
Alieruka kutoka section 2 hadi five analijua vema hilo ndio maana karukia huko ili beberu mwingine akiingia ikuru asije akakata bomba itamlazimisha kuunga,anayo experience ya bagamoyo port jamaa sio mbumbumbu anajua kusoma na kuandika.Dar-Moro=300Km
Moro-Makutupora=426Km
Makutupora-Isaka=435Km
Isaka-Mwanza=220Km
Isaka-Rusumo=371Km
Kwa nini kazi zisiende kwa mfuatano ili hata ngoma ikikwama njiani ruti iwepo ya kuishia hata Isaka.
Wachina watamaliza na kukabidhi Isaka-Mza huku kipande cha Makutu-Isaka kikiwa bado hata tenda haijatangazwa halafu anaingia Rais mwingine na kusema reli siyo kipaumbele chake,mradi unaachwa kwenye mataa kama katiba mpya.
Yawezekana!unadhani wanajipendekeza !!! hawajipendekezi kama wangekuwa wanajipendekeza jiwe asingeenda Chato mapema ila kwakuwa yupo huko basi kataka mwenyewe
kwa nini hatuona umuhimu wa kuifikisha SGR kigoma kwenye business kubwa na DRC tukaamua kuipeleka mwanza kwanza?
Hapa tumefichwa jambo mkuu.Dar-Moro=300Km
Moro-Makutupora=426Km
Makutupora-Isaka=435Km
Isaka-Mwanza=220Km
Isaka-Rusumo=371Km
Kwa nini kazi zisiende kwa mfuatano ili hata ngoma ikikwama njiani ruti iwepo ya kuishia hata Isaka.
Wachina watamaliza na kukabidhi Isaka-Mza huku kipande cha Makutu-Isaka kikiwa bado hata tenda haijatangazwa halafu anaingia Rais mwingine na kusema reli siyo kipaumbele chake,mradi unaachwa kwenye mataa kama katiba mpya tunakuwa tumepoteza pesa bure.
KUna uwanja wa Mpira unakuja. Mkubwa sanaSio muda watajenga na UCHato= University of Chato
Ni mjamaa sikatai lakini kuwa mjamaa haikatazi kuwa beberu bali inakataza kuwa bepariMchina ni mjamaa kwa asili
Jamani wana JF wenye mlengo usio na nia njema kwa taifa letu tuache kulaumu hovyo.
Sisi kama Watanzania tunahitaji reli,maana reli itapunguza gharama za maisha kwa 40%. Hivyo kwa mkataba wa ujenzi wa reli ulisainiwa leo ni jambo jema kwa nchi yetu.
Tuache tabia ya kulaumu na kuponda kila jambo,China wamekuwa rafiki za watanzania kwa muda mrefu. Na wamekuwa msaada kwetu kila tunapowahitaji.Kabla na baada ya vita vya Kagera tulipata hali ngumu ya kiuchumi,China walitushika mkono, tusisahau.
Sioni kama ni jambo jema kuanza kuponda huu mkataba kisa tu ni wafuasi wa vyama vya upinzani ambavyo vimefanya vibaya kwenye uchaguzi uliopita. Habari za kuleta hisia kuwa wachina ni matapeli sio nzuri.
Pia tuwaamini viongozi wetu,sidhani kama wanaweza kuingia mikataba mibovu kiasi cha kuiweka rehani nchi yetu.
Maoni; SGR ikikamilika itakuwa na manufaa kwa kila mtanzania,tuache siasa za kizandiki na kupinga maendeleo.
Kuidharau China kuwa ni tajiri uchwara sio hoja ya msingi. Utapeli wa taifa la China upo wapi? Unatakiwa China imrkuwa na msaada mkubwa sana kwa Tanzania usio na harufu ya kibeberu miaka nenda rudi.Wachina ni matapeli a.k.a matajiri uchwara, na viongozi wetu wana 10% kwenye huo mkopo wa China. Kama ni kuwaamini viongozi waamini ww, lakini sio kila mtu anaweza kuwaamini viongozi walioko madarakani kwa wizi wa kura.