Ndo mlolongo wenyeweee?? TobaaaaahRoho mbaya ya utawala ndo kisa.
Passport tu kuipata mpaka uulizwe tupe letter mfano ya chuo unachoenda. Na chuo unachoomba hawakupi letter wanataka uwape passport number ili waandike letter. Sasa wangapi watatoka?
Chuo wanakuomba maombi yako ili wayafikirie wanataka barua ya TCU kwamba una qualify kusoma hicho ulichoomba, unakimbia TCU kuwaomba barua, wao TCU wanakwambia ili wakuandikie wanataka admission letter ya hicho chuo.
Unaamini Watanzania ni wajinga Sababu hawaendi Nje?Laiti nusu ya Watanzania wangeenda kuishi ughaibuni alau kwa miaka mitatu tu kisha wakarejea nyumbani, kungewasaidia sana katika kuboresha uwezo wao wa kufikiri. Naamini, ingelikuwa hivyo, hata watawala wasingekuwa wepesi kuwadanganya kirahisi rahisi.
Home seeking ndio ugonjwa mkubwa ambao huwakuta watu walio mbali na nyumbani.Watz wengi kwa akili zetu fupi tunafikiri kuwa na diaspora wengi ndio mafanikio.
Ni kweli kuna changamoto katika taratibu za kutoka nje. Pia kuna shida na tabu nyingi ndani ya nchi hii, zikichangiwa zaidi na mfumo wetu wa kiutawala.
But all in all, we should thank God a thousand times for the way we are. Ukitaka kuelewa kidogo tu Tz tulivyo safi vuka border hapo Sirari uone maisha yalivyo tofauti kule utakakoingia, hata salamu utatamani uinunue.
Kuna watu humu juzikati nimeshangaa kuona wakiwasifia Somalia kwa kuwa na diaspora wengi, huku wakiwish nasi tuwe kama Somalia! Wonderful!
Magufuli hakutaka uende nje na ulishangilia sana. Vipi unalizungumziaje hili? Au naye alikuwa mkoloni mweusi? Au double standards? Au au au...Wakoloni weusi wanapenda tuendelee kubakia hapa tusipate akili ili waendelee kutuburuza.
Ila watoto wao wanawapeleka nje kusoma na wao wanakwenda kutibiwa na kufanya shoping.
Watanzania si wajinga, lakini kusafiri kutachangamsha zaidi akili waliyojaliwa na Mungu.Unaamini Watanzania ni wajinga Sababu hawaendi Nje?
Unaamini wote waliopo nje wanauwezo wa kufikiri kuliko waliopo ndani?
Sana, hasa kama hupendi kutoa rushwa. Lakini kama ni mwepesi wa kunyoosha mkono, hata na fomu unaweza ukasaidiwa kujaza. Ukiritimba woote uliopo ni kwa ajili ya kufanikisha project takrima. Ni mradi wa watumishi wabinafsi.Ilipaswa kila anayezaliwa apewe passport bila maswali kama ya kipolice. Kupata passport Tanzania ni changamoto sana
Na inawezekana sababu kubwa ni kwa vile wenye dhamana hawana exposure. Wanaamini wanajua kuliko wengine kumbe...Ndo mlolongo wenyeweee?? Tobaaaaah
Wa upande gani, Tanganyika au Zanzibar? Mi nahisi ni wa Tanganyika!Hii ipo kwa watanzania tu sijui kwanini
Hapana mkuu! Ujinga haujawahi kuwa "bliss". Ujinga hukufanya wajanja wakufaidi huku wewe ukiumia bila kujua!I'm proud of my country,japo hatupo exposed na hatuna elimu sana ila hua nakubaliana kua most of the times ignorance is bliss. Ujinga wetu ni faida sana kwetu.
Watanzania ni watu flani hivi maskini jeuri and I proud of that. Japo hatuna pesa ila hatushoboki Kwa watu,pia hatupendi kulia Lia njaa.
Ni kweliRoho mbaya tu anayetangulia hataki wengine wafike huko
Siupendi huo msamiati ulioutumia lakini umefikisha ujumbe barabara.tanzania ni jela isiokuwa na fensi
Inamaanisha nini?Juzi nimeenda Makao Makuu Kurasini ni patupu waombaji hata 10 hawafiki tofauti na zamani watu walikuwa wanajazana.
Hapo umenenaInawezekana pia ikawa inaongoza kwa raia wake wengi kutokuwa na passport.