Tanzania yashindwa kwenye kesi, yaamuriwa kulipa fidia ya zaidi ya Tsh. Bilioni 260

Tanzania yashindwa kwenye kesi, yaamuriwa kulipa fidia ya zaidi ya Tsh. Bilioni 260

We subiri tu...

Hata Lissu kasema huu mkataba ni lazima uvunjwe hata tulipe pesa kiasi gani ni sawa tu...

Magufuli ndiyo alitumia maguvu kuvunja mamikataba haya ya hovyo lakini kimsingi alikuwa sahihi. Sema
sasa hakuna uzalendo na tumerudi kule kule. Hawa hawa wanaotushinda mahakamani wanaweza kurudi na wakasaini tena mikataba kama ile ile aliyoivunja Magufuli...Hovyo tu!

Screenshot_20230718_113710_Chrome.jpg
 
Mkataba huu je CCM italaani mabeberu na kuitisha maandamano nchi nzima kuhusu kesi za fidia za namna hii ?

Serikali ya CCM itambue hakuna mwekezaji aliye na fedha mfukoni.

Mwejezaji akisha saini kuenda kunadi mradi wake ktk mabenki na wabia wengine ili ku mobilise resources yaani kupata rasilimali fedha, watu mfano kutafuta mine engineers, kuhamisha heavy equipments tena kwa kukodisha, kutayarisha usafiri wa mavifaa haya mazito n.k, kulipa insurance n.k n.k

Hivyo ghafla ukimfutia mkataba au leseni wengi walio nyuma ya mwekezaji wanapata hasara ya mali, fedha,watu, wakati, kukosa kipato walichotarajia, hadhi / goodwill ya aliyesuka deal hili na serikali ya Tanzania kushuka kwa kudhaniwa hawakufanya makubaliano yaliyostahili na waswahili hivyo wanaweza kukosa kazi siku za usoni sehemu zingine za dunia n.k

Hivyo hakuna namna hasara hiyo lazima Tanzania iilipe kwa maamuzi ya kutoona mbali wakati wa kumkubali mwekezaji ukifikiri ana fedha kibao mfukoni zimekaa tu kumbe jamaa hawa wana watu wengi wanaocheza upatu katika miradi ya mikubwa uwekezaji wakisubiri mgao wao halali walipowekeza.

NACHINGWEA U.K. LIMITED (UK), NTAKA NICKEL HOLDINGS LIMITED (UK) AND NACHINGWEA NICKEL LIMITED (TANZANIA) V. TANZANIA refence Case ID:

ICSID Case No. ARB/20/38

N.B
Mkataba mbovu wa DP World nao una sifa hizo hizo za wawekezaji na huja na gharama zake kama hizo.
Nakazia tu
Hivyo hakuna namna hasara hiyo lazima Tanzania iilipe kwa maamuzi ya kutoona mbali wakati wa kumkubali mwekezaji ukifikiri ana fedha kibao mfukoni zimekaa tu kumbe jamaa hawa wana watu wengi wanaocheza upatu katika miradi ya mikubwa uwekezaji wakisubiri mgao wao halali walipowekeza.
 
Kwenye utawala wa kufuata Sheria na kanuni aliturudisha nyuma sana kipenzi chetu wanyonge
 
Mkataba wa Uwekezaji wa Nchi Baina ya Uingereza na Tanzania (BIT)

Ule wa mkataba baina ya serikali ya Tanzania na 'nchi' ya Dubai kuhusu bandari nao una mashaka makubwa

Azimio la Bunge : 10 June 2023
APPENDIX ONE

Mheshimiwa Spika, Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja
ambayo imeshughulikia alisema haya ni makubaliano na
makubaliano haya yanaweka msingi wa kitu kitakachokuja
kufanyika, hiyo mikataba itakayokuja kujengwa huko mbele. Huu
sio mkataba wameshazungumza watu, huu sio mkataba,
tunawatoa hofu Watanzania wayasikilize hayo maelezo vizuri,
lakini mikataba itakuja mmoja mmoja katika eneo moja moja.
Mheshimiwa Spika, ukienda katika mkataba huu kuna
appendix I ambayo kuna mambo ambayo phase one project
zitakazofanyika. Kwa hiyo, ndani ya project zile zitakapofanyika
ndipo kutakuwa kuna hiyo mikataba midogo midogo na mimi
nilitoe hofu Bunge hili na wananchi wa Tanzania sio kwamba kila
kilichotajwa kwamba kitafanyika kwa yote. Ukisikia kutafanyika
development, ukisikia kutafanyika improvement ukisikia
kutafanyika management, ukisikia kutafanyika operations, kuna
miradi au kuna phase au kuna project ziko katika hatua tofauti
tofauti. Ziko nyingine tutaanza kweli ku–develop kwa sababu ni
kitu kipya, lakini kuna vingine vinatakiwa kufanyiwa management,
lakini kuna vingine vitafanyiwa operation. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa ukitazama kuanzia hiyo gati zero
mpaka gati number seven utakuja kuona kwamba ni kweli, ukiijua
ile bandari kwamba kuna maeneo kutafanyika operation na kuna
maeneo mengine wao wata-improve lakini wataachiwa bandari
wenyewe waendeleze. Sasa na mimi na stick pale pale kwenye
ushauri wa Kamati kwamba ni lazima tuhakikishe hiyo mikataba
sasa iwe ina tija kwa Watanzania. Tuhakikishe hiyo mikataba
wanashirikishwa wadau husika tutakapoingia hiyo mikataba
mmoja mmoja, lakini pia mikataba hiyo ni lazima itoe ukomo au
itaje ukomo kama wananvyosema wengine na maoni mwengine
ambayo Mwenyekiti ameshauri na Wajumbe wengine Wabunge
wengine wameshauri.
Mheshimiwa Spika, lakini hofu nyingine kwamba huu
mkataba hauna ukomo, mkataba huu unao ukomo nao
umetajwa, sisi kama Wabunge wa Bunge lako hili tukufu tumekaa
hapa kwamba tunaelewa nini kinaendelea....

Soma zaidi toka : 10 June 2023 Bunge kuhusu pendekezo la kuridhiwa mkataba baina ya serikali ya Tanzania na serikali ya Dubai

: Parliament of Tanzania
Bunge la Tanzania / Parliament of Tanzania
 
ndio maana hatuwaamini wanasheria wetu wanaoendeshwa na wanasiasa hasa hawa wa serikali.

Ndio maana tunashindwa kuwaamini hata kwenye hili la DPworld.
 
Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) kimeiamuru Tanzania kulipa dola milioni 109.5 (zaidi ya bilioni 260 za Tanzania) kwa kampuni za uchimbaji madini zilizosajiliwa Uingereza, Ntaka Nickel Holdings Ltd na Nachingwea UK Ltd, kufuatia uamuzi wa mwaka 2018 kufuta Leseni yao ya Kuhifadhi madini ya Nikeli.

Kampuni hizo zilifanikiwa kuishitaki Tanzania katika mahakama ya Benki ya Dunia kwa kukiuka majukumu yake chini ya Mkataba wa Uwekezaji wa Nchi Baina ya Uingereza na Tanzania (BIT) na sheria za kimataifa kwa kunyang'anya leseni hiyo.

Tanzania pia imetakiwa kulipa dola milioni 3.859 za gharama za kisheria kwa wadai, pamoja na ada na gharama za mahakama ya ICSID.

Kampuni ya Indiana Resources Ltd iliyoorodheshwa kutoka Australia, ambayo ndiyo wanahisa wengi wa mradi wa nikeli wa Ntaka, iliwahi kutishia kukamata ndege zinazoendeshwa na Kampuni ya Air Tanzania (ATCL). Indiana inasema sasa itachukua hatua haraka kutekeleza tuzo ya mahakama

Kampuni za EcoDevelopment na EcoEnergy za Uswidi mwaka jana zilishinda uamuzi wa $165m dhidi ya Tanzania kwenye ICSID kufuatia uamuzi wa serikali ya Magufuli kuwanyang'anya wawekezaji hao ardhi ya Bagamoyo, kinyume na Mkataba wa Uwekezaji wa Nchi Baina ya Sweden na Tanzania (BIT)

Kampuni hizo zilikamata ndege ya Airbus inayomilikiwa na Wakala wa Serikali wa Ndege za Serikali (TGFA) inayoendeshwa na ATCL ili kutekeleza hukumu ya ICSID.

Ndege hiyo yenye namba za usajili 5H-TCH hivi karibuni ilirejea Tanzania baada ya serikali kumaliza kesi hiyo.

View attachment 2691787

Pia soma: Maamuzi ya Magufuli yaigharimu Tanzania zaidi ya Bilioni 266
shenzi type kwenye dp world tutauza hadi wajukuu na bado tutadaiwa
 
Mwendazake alitufanyia mabalaa yya ajabu. Na bado wengine.
Kiini cha tatizo hapa ni ccm na serikali zake. Kama unaona Mwendazake alifanya vibaya, alikuwa ni moja ya rangi za hicho chama.

Aliyeko sasa hivi ni balaa...JPM cha mtoto!
 
Hakuna watu wajinga Dunia hii kama watu wa CCM , yaani tahadhari zote mna pewa bado hamuelewi, watalaam, wapinzani, wananchi wenye nia njema wana jitahidi kuwaeleza na kuwa onyesha kuwa hii mikataba mibovu lakini hayasikii, kila mwaka kuna hasara ya mikataba hii, hivi akili zao sijui zime gotea wapi, maana sio kwa ujinga huu.
 
Mwendazake alitufanyia mabalaa yya ajabu. Na bado wengine.
Mnamsingizia Magufuli haya ni mazagazaga ya Kikwete na genge lake!! Samia lazima awe mwangalifu sana na Rostam ambae kisha muingia ; akifanya mchezo Rostama atamuangamiza huyo mwanae Abdul kama alivyomungamiza marehemu Balali!!! Rostam sio mtu wa kumuweka karibu atakuliza!! Amekwisha muingiza mkenge Samia sijui utatokaje?

Fedha za maendeleo mtaishia kuwalipa wajanja fidia kutokana na upumbuvu wenu kusaini mikataba bila kuielewa!! Ona sasa hiyo invoice nyingine ya faint ya mabilioni ya shilling imekuja huku mnaongeza bei ya cement muwalipe mabwana zenu!!
 
Hakuna watu wajinga Dunia hii kama watu wa CCM , yaani tahadhari zote mna pewa bado hamuelewi, watalaam, wapinzani, wananchi wenye nia njema wana jitahidi kuwaeleza na kuwa onyesha kuwa hii mikataba mibovu lakini hayasikii, kila mwaka kuna hasara ya mikataba hii, hivi akili zao sijui zime gotea wapi, maana sio kwa ujinga huu.

Wana ccm wote wanaishi bila UBONGO na ndio maana miaka yote ya utawala wao ni hasara kwa nchi!!!
 
Huenda Mwendazake alifanya maamuzi magumu kuwamba bora tupoteze hizo B 200 lakini madini yetu yenye thamani kubwa kuliko hizo pesa tubaki nayo sisi wenyewe.

JK aliyeingia huu mkataba mbovu hapa analawama zake nyingi sana.

Mkataba ungekuwa na maslahi kwetu JPM asingeufuta!
Ni hivi,Magufuli hakuwahi kuwa na nia ya kuwasaidia watz kwa ujumla.Mfano ni KIWANDA CHA SARUJI CHA DANGOTE.Kikwete aliwaangalia raia na kuwatafutia njia za kuwafanyia wepesi katika kupiga hatua kimaendeleo.Ujio wa Dangote ulilenga kuwasaidia raia katika kuleta makazi bora kwa kila raia,alikiruhusu kiwanda kizalishe Saruji ya viwango vyote ili kuwawezesha raia wa vipato vya kawaida pia kumudu gharama ya kununua Saruji kwa ujenzi wa makazi.
Kiwanda cha Dangote kilifanya Saruji huku mikoani kuuzwa kwa Tsh12000 kwa mfuko.
Magufuli alipoingia madarakani alimzuia Dangote kuzalisha Saruji ya viwango vyote na kumtaka abaki akizalisha Saruji ya viwango vya kimataifa tu ambayo mfuko mmoja ni kati ya Tsh 25000 hadi 35000.
Leo hii hakuna tena Saruji ya Dangote madukani huku mikoani,bei ya Saruji kwa sasa ni kati ya Tsh 18000 hadi 22000.

Sasa kwa mfano huu unaweza kusema Magufuli alikuwa akiwajali raia na maisha yao?.
Huo uzalendo mnaouimba toka kwake ni upi hasa?.
Kwa hiki alichokifanya kwa Saruji ya Dangote,alikifanya kwa manufaa ya nani?.
Tunawezaje muamini mtu wa aina yake katika malengo ya kuivunja mikataba hii tukiangalia mfano wa kiwanda cha Dangote?.
 
Bado Dp watakuja kujichotea pesa,mkataba mbovu sana utakaomtesa rais ajaye
 
Aliyeingia ndio mpumbavu, aliyevunja ndio alitumia akili, huwezi kuingia mkataba wa kipuuzi usio na maslahi kwa taifa halafu uje kumlaumu aliyeuvunja, wewe ndie utumie akili.
Wewe ndio huna maarifa,mkataba wowote mahali popote,wakati wowote ukiuvunja,ukisitisha,ukiuondoa kwa namna yoyote lazima ile kwako.Tumia maarifa.
 
Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) kimeiamuru Tanzania kulipa dola milioni 109.5 (zaidi ya bilioni 260 za Tanzania) kwa kampuni za uchimbaji madini zilizosajiliwa Uingereza, Ntaka Nickel Holdings Ltd na Nachingwea UK Ltd, kufuatia uamuzi wa mwaka 2018 kufuta Leseni yao ya Kuhifadhi madini ya Nikeli.

Kampuni hizo zilifanikiwa kuishitaki Tanzania katika mahakama ya Benki ya Dunia kwa kukiuka majukumu yake chini ya Mkataba wa Uwekezaji wa Nchi Baina ya Uingereza na Tanzania (BIT) na sheria za kimataifa kwa kunyang'anya leseni hiyo.

Tanzania pia imetakiwa kulipa dola milioni 3.859 za gharama za kisheria kwa wadai, pamoja na ada na gharama za mahakama ya ICSID.

Kampuni ya Indiana Resources Ltd iliyoorodheshwa kutoka Australia, ambayo ndiyo wanahisa wengi wa mradi wa nikeli wa Ntaka, iliwahi kutishia kukamata ndege zinazoendeshwa na Kampuni ya Air Tanzania (ATCL). Indiana inasema sasa itachukua hatua haraka kutekeleza tuzo ya mahakama

Kampuni za EcoDevelopment na EcoEnergy za Uswidi mwaka jana zilishinda uamuzi wa $165m dhidi ya Tanzania kwenye ICSID kufuatia uamuzi wa serikali ya Magufuli kuwanyang'anya wawekezaji hao ardhi ya Bagamoyo, kinyume na Mkataba wa Uwekezaji wa Nchi Baina ya Sweden na Tanzania (BIT)

Kampuni hizo zilikamata ndege ya Airbus inayomilikiwa na Wakala wa Serikali wa Ndege za Serikali (TGFA) inayoendeshwa na ATCL ili kutekeleza hukumu ya ICSID.

Ndege hiyo yenye namba za usajili 5H-TCH hivi karibuni ilirejea Tanzania baada ya serikali kumaliza kesi hiyo.

View attachment 2691787

Pia soma: Maamuzi ya Magufuli yaigharimu Tanzania zaidi ya Bilioni 266
Hili nalo wapewe DP World. Mwarabu ana pesa ndefu. Hili ni dogo sana kwake
 
Back
Top Bottom