Ndugu yangu, lakini haya masharti si ndo yalikuwa hivi siku zote? Yamekazwa wapi katika hizo stages? Ila sikujua kwamba mwisho wa siku RPC ndio anapitisha maombi. RPC ni mtu mkubwa mno kupitia maombi ya sijui Horseshoe anaomba bastola, hivi hawana kazi za maana hawa watu jamani?
Na tunaposema wakiona unahitaji ndio watakupa kwa nini isiwe kwenye sheria ya wazi ni wakati gani unaonekana unahitaji? Nasikia mpaka uwe na kipato / mfanyabiashara mkubwa. Hivi jambazi akikuingilia Boko Bunju huko kama walivyomfanya Dr. Mvungi jambazi anakuwa amefanya research ya salary slip yako?
Halafu utaratibu wa kumiliki bunduki kwa nchi za wenzetu hauwezi kubadilika badilika ovyo kwa sababu eti visa vya kimapenzi vimezidi. Visa vyenyewe vitatu, na hakuna aliyefanya research kujua vimezidi by how much and why. Wanawake wanafyekwa mapanga na wame zao ma heathen upcountry huko kiiiiila siku, mbona wasiminye kumiliki mapanga? Wamekufa watoto shuleni jimbo la Connecticut USA nchi ikalia weee halafu wakabadili sheria. Hapa kwetu Kamanda Kova ana uwezo wa kuamua the gun law of the month. I am very frustrated na gun law ya Tanzania, vitu vyooote hapa kwetu havi make sense, why?