Uchaguzi 2020 Tarime: Tundu Lissu ampiga marufuku Kassim Majaliwa kufanya kampeni, Yadaiwa anavunja maadili ya uchaguzi

Uchaguzi 2020 Tarime: Tundu Lissu ampiga marufuku Kassim Majaliwa kufanya kampeni, Yadaiwa anavunja maadili ya uchaguzi

Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu amemuonya Kassim Majaliwa kwa kitendo chake cha kufanya kampeni za Urais kote anakopita , kwa vile kitendo hicho ni kukiuka maadili ya uchaguzi .

Kwa mujibu wa Lissu, Waziri Mkuu Kikatiba hatakiwi kumpiga kampeni mgombea Urais wa chama chake nje ya jimbo lake la uchaguzi ambalo ni Ruangwa tu na ameonya kwamba NEC isipochukua hatua kwenye hili basi itajisimika rasmi kuwa TUMECCM .

Je, Wanasheria mliopo hapa JF hili jambo limekaaje?



Kama ni kizunguzungu wamekipata. Kila kona wanavurunda, alafu tume imekaa kimya kama vile hawaoni.
Mambo yamepamba moto. Ni mwendo washeria na siasa. Sasa huyu vyote anaviweza. Kamatia hapo na ongeza makali kidoo. HAPA NI MWENDO WA KANYAGA TWENDE TU.

Watajitetea anatekeleza majukumu yake ya kazi kiserikali, wakati huo ni kijani kitupu na chopa inayotumika ni hile iliyokodiwatoka kule--------.

Mahera hiyo kamati ya maadili ina meno kwa wapinzani tu au ndo maagizo toka juu?
 
Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu amemuonya Kassim Majaliwa kwa kitendo chake cha kufanya kampeni za Urais kote anakopita , kwa vile kitendo hicho ni kukiuka maadili ya uchaguzi .

Kwa mujibu wa Lissu, Waziri Mkuu Kikatiba hatakiwi kumpiga kampeni mgombea Urais wa chama chake nje ya jimbo lake la uchaguzi ambalo ni Ruangwa tu na ameonya kwamba NEC isipochukua hatua kwenye hili basi itajisimika rasmi kuwa TUMECCM .

Je, Wanasheria mliopo hapa JF hili jambo limekaaje?


Kweli kabisa
 
Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu amemuonya Kassim Majaliwa kwa kitendo chake cha kufanya kampeni za Urais kote anakopita , kwa vile kitendo hicho ni kukiuka maadili ya uchaguzi .

Kwa mujibu wa Lissu, Waziri Mkuu Kikatiba hatakiwi kumpiga kampeni mgombea Urais wa chama chake nje ya jimbo lake la uchaguzi ambalo ni Ruangwa tu na ameonya kwamba NEC isipochukua hatua kwenye hili basi itajisimika rasmi kuwa TUMECCM .

Je, Wanasheria mliopo hapa JF hili jambo limekaaje?

Ndo maana nikashangilia Lissu kuitwa na Tume.
 
Kwamba Lissu ndiye peke yake anajua tafsiri ya sheria? Kama nawe unaamini hivyo iweje ahamasishe wapiga kura kuingia barabarani iwapo hatatangazwa mshindi?
Kwahiyo akishinda halafu asitangazwe unataka afanyeje? Bila shaka inajua kabisa kwa sheria zetu rais akitangazwa na tume hakuna mahali popote utakapokwenda kukata rufaa. Usijifanye hamnazo kwa sababu ya ushabiki wako. Kwanza hajasema yeye atangazwe akishindwa ila akishinda kusiwe na kigugumizi cha kumtangaza vilevile.

Jitahidi kuushirikisha ubongo wako.
 
Majaliwa anatembea jimbo kwa Jimbo na akifika kwenye Jimbo mwenyeji wake nimgombea wa ubunge wa Jimbo husika.
Inawezekana mgombea ubunge wa jimbo jingine kwenda kumpigia kampeni mgombea wa jimbo jingine?
Kiongozi wa Chama kwenda kumpigia kampeni mgombea wa jimbo jingine.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Tumefikia patamu sasa, ni dk ya 15 tu ya mchezo mambo ndiyo yanazidi kunoga mnogage! Twende Lissu twende !!
 
Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu amemuonya Kassim Majaliwa kwa kitendo chake cha kufanya kampeni za Urais kote anakopita , kwa vile kitendo hicho ni kukiuka maadili ya uchaguzi .

Kwa mujibu wa Lissu, Waziri Mkuu Kikatiba hatakiwi kumpiga kampeni mgombea Urais wa chama chake nje ya jimbo lake la uchaguzi ambalo ni Ruangwa tu na ameonya kwamba NEC isipochukua hatua kwenye hili basi itajisimika rasmi kuwa TUMECCM .

Je, Wanasheria mliopo hapa JF hili jambo limekaaje?

Amesema "Kikatiba" Waziri Mkuu haruhusiwi kutumia cheo chake na resources za Serikali kufanyia kampeni zake binafsi au za mgombea wa udiwani, ubunge au urais.
Je maana yake hata JPM, kama Rais, nae asifanye hivyo?
Mazoea yana tabu kidogo!
 
Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu amemuonya Kassim Majaliwa kwa kitendo chake cha kufanya kampeni za Urais kote anakopita , kwa vile kitendo hicho ni kukiuka maadili ya uchaguzi .

Kwa mujibu wa Lissu, Waziri Mkuu Kikatiba hatakiwi kumpiga kampeni mgombea Urais wa chama chake nje ya jimbo lake la uchaguzi ambalo ni Ruangwa tu na ameonya kwamba NEC isipochukua hatua kwenye hili basi itajisimika rasmi kuwa TUMECCM .

Je, Wanasheria mliopo hapa JF hili jambo limekaaje?


Si kweli. Anakwenda kama mjumbe wa kamati kuu
 
Wajinga nyie, mikutano ya kampeni inapangiwa ratiba jee Majaliwa anapangiwa ratiba na NEC?
Hivi kama kila mjumbe wa kamati kuu wa kila chama atafanya mikutano jee haitakuwa fujo hiyo?
Msipende kutetea ujinga!
Kama anajisikia kupiga kampeni aongozane na mgombea wao

Nani kawakataza?
 
Otherwise Kama anatumia mwamvuli wa uwaziri mkuu. Ila Kama anatumia mwamvuli wa kada na mjumbe wa kamati kuu ya ccm Sheria Wala maadili ya tume hayambani hata kidogo. Endapo anajiamini Hana haja ya kampeni Jimboni kwake Basi habanwi kumwombea kura magufuli popote Tanzania.
Tatizo lipo hivi, Je anaweza kuihakikishia Tume kwamba anapokwenda mikoani anaachana na uwaziri Mkuu na anakwenda kama kada na Mjumbe wa kamati kuu? Je hii inawezekana?

Kama akisema yeye bado ni Waziri Mkuu na nakwenda kutimiza majukumu yake hilo ni sawa, lakini je huko kuwa haongelei masuala ya kumwombea JPM kura?
 
Lissu The Greatest
Lissu nilimwamini kwamba ni NGULI pale tu alipowafundisha watu Sheria kwamba UGAIDI hadi uitwe ugaini lazima uhusishe watu zaidi ya wawili - wakati kale ka Clip ketu ambako kangepita ilikuwa CDM ifutwe kakawa na sauti za watu wawili.

Lissu ni darasa tosha la hata wana Lumumba kujichotea weredi tena bila malipo.
 
Returning officer ni nani kwa mujibu wa hii sheria?Na je,katika ngazi ya uraisi, kuna returning officer mwenye mamlaka ya kupanga/kupokea ratiba ya mikutano ya wagombea uraisi au kuidhinidsha watu wa kumpigia kampeni mgombea uraisi?

Kwa maneno mengine,mtu mwenye wadhifa wa returning officer, anatakiwa/ana uhalali wa kisheria wa kupewa taarifa za nani atampigia kampeni mgombea uraisi katika eneo lake?
 
Otherwise Kama anatumia mwamvuli wa uwaziri mkuu. Ila Kama anatumia mwamvuli wa kada na mjumbe wa kamati kuu ya ccm Sheria Wala maadili ya tume hayambani hata kidogo. Endapo anajiamini Hana haja ya kampeni Jimboni kwake Basi habanwi kumwombea kura magufuli popote Tanzania.
Wewe humuoni anavyofanya; anakagua na kuzindua miradi kwa mwamvuli wa Waziri Mkuu halafu hapo hapo anajigeuza mjumbe wa kamati kuu ya CCM kupiga kampeni!
 
Ile dhana ya Great Thinker kwa wana Jamii Forum inapotea kabisa maana yanatoka majibu kama ya Facebook. Mleta uzi kauliza sheria inasemaje kuhusu Kassim Majaliwa kumpigia kampeni JPM? Nimeona ni kawoli tu ndo kaweza kutoa jibu. Wanasheria tuisaidieni, imekaaje hiyo?
 
Hakuna kiingereza cha "Lissu The Greatest", ni "Lissu The Great", ukiandika Lissu The Greatest lazima umalizie na sifa yake yoyote. Mfano ungeandika: "Lissu The Greatest Politician". Au "Lissu The Greatest Lawyer"

Kila siku mnakandia watu hawajui kiingereza kumbe na nyie Grammar ni ZERO.
Wewe ni mwalimu mzuri sana wa grammar, sasa mbona humfundishi bosi wako baba Jeska???
Hadi anakimbia vikao vya SADC kisa lugha..teh teh teh

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom