Taswira ya Yesu anayehubiriwa ni tofauti na Yesu halisi

Taswira ya Yesu anayehubiriwa ni tofauti na Yesu halisi

Wao ni wapumbavu, maana wao walimuona kwa macho, waliona Miujiza anafanya, sisi tunasikia habari zake kwa kupitia Manabii na tunaamini, Inamaana sisi tuna IMANI kubwa sana...
Hapo kwa kumwona kwa macho ndipo point ilipo.
Kuwa wakimwona kwa macho lakini hakuamini maana alikuwa haendani na kile walichokitegemea ndio maana nasema walimwona kama outcast
 
Ndio neno linavyotuambia, na neno la Mungu ni kweli, hata sasa mimi na wewe tunatofautiana ni kwakuwa mi ninavyomuona au kumjua Yesu sio kama wewe...

Ni ngumu sana kumjua YESU kwa kibinadamu lazima uwe mtu wa Rohoni
Neno linanimbia kwamba kabla petro hajaamua kuwa mwanafunzi wa Yesu alikutna kwanza na Mwanafunzi wa Yohana Mbatizaji

Yohana 1:40-45

Screenshot_20231031-100707.png
 
Sasa hapo point yangu ya msingi ndipo ilipo. Waliokuwepo physically wakamuona physically kwa maisha yake physically wengi walimwona hivyo nilivyoandika. Na ndio maana Wayahudi ambao alisema yeye ni mfalme wao mpaka leo hawamwamini wanahisi bado hajaja maana wana picha yao ya Yesu na physical life ambalo wanadhani ndilo angekuwa nalo.
Huenda hata wewe ungekuwepo usingeamini.

Mtu ambaye anafufua wafu mbele yako,anaponya wagonjwa mbele yako na miujiza kibao bado unahisi ni tapeli,huoni kama shida iko kichwani kwako!!!

Kwa ulimwengu wa sasa hivi angetoka hata mtu wa kushika wagonjwa vichwa wapone achia mbali kufufua wafu,hakuna mtu asingemsikiliza.
 
Sasa hapo point yangu ya msingi ndipo ilipo. Waliokuwepo physically wakamuona physically kwa maisha yake physically wengi walimwona hivyo nilivyoandika. Na ndio maana Wayahudi ambao alisema yeye ni mfalme wao mpaka leo hawamwamini wanahisi bado hajaja maana wana picha yao ya Yesu na physical life ambalo wanadhani ndilo angekuwa nalo.
Huenda hata wewe ungekuwepo usingeamini.
Hakuna aliyemuona Physically Yesu aliandika habari ambayo tunaisoma leo Injili Nyingi zimeanza kuandikwa mwaka 70 AD miaka zaidi ya 30 baada ya kufa kwa yesu na injili zote ni third part Authenification
 
Hakuna aliyemuona Physically Yesu aliandika habari ambayo tunaisoma leo Injili Nyingi zimeanza kuandikwa mwaka 70 AD miaka zaidi ya 30 baada ya kufa kwa yesu na injili zote ni third part Authenification

Hata angekuwepo aliyemuona kwa macho na kula naye ugali bado asingekuwa hai mpaka leo hii.still ungekuwa na wasi wasi tu na uhakika wa taarifa za Yesu.
 
Ukisoma na kutafakari kwa umakini kuhusu Yesu unagundua kwamba alikuwa ni wale watu ambao jamii inawachukulia kwamba wamepinda yani outcast.

Hata wale wanafunzi wake aliokuwa akiongozana nao jamii inaonekaan ilikuwa inawachukulia kama watu wasiokuwa na maadili waliopotoka yani waliopinda.

Ndio maana kuna sehemu hadi anaulizwa, inakuaje anakula na kunywa na wenye dhambi? Hii bila shaka haina tofauti na sasa unamuuliza, we jamaa unaonekana ni mwenye ehshima inakuaje unashinda na wazinzi na walevi?

Hebu fikiria mtu unayemheshimu sana anakuja kahaba analia miguuni mwake anampangusa kwa nywele anambusu miguu, assume huyo jamaa anayefanyiwa hivyo ni hakimu na huyo kahaba ana kesi. Halafu baada ya kufanyiwa hivyo hakimu anamwambia kesi yako utashinda!

Bila shaka utasema hakimu kasema hayo kwa sababu kahaba kamtamanisha kwa kumshika shika na kumbusu miguu huenda watamalizana huko mebeleni. Hiki ndicho kilichotokea kwa yule kahaba na bila shaka wale jamaa walisema moyoni huyu jamaa amelegea kwa kahaba atakuwa msela tu anatuigizia.

Ukichukulia hali hii kwakweli hata angekuja leo hapa TZ bado watu wangemkataa. Wangemwona msela Fulani hivi mwenye group la watu waliopinda. Yani kipindi anajiita kwamba yeye ni mfalme wa Wayahudi, huenda wale viongozi walikuwa wanamchukulia kama Ney wa Mitego anavyojiita raisi wa masela au Madee anayejiita rais wa Manzese hawakuwa wakimchukulia serious kihivyo mpaka alipoanza wazingua.

Kama akirudi kwa style hiyo hiyo sijui ni wangapi wataamini kuwa ni Yesu.
Aseee! Hongera sana Kwa tafakuri mardhawa kabisa. Ukweli mtupu
 

Luka 5:31-32 BHN​

31. Yesu akawajibu, “Wenye afya hawamhitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.

32. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, wapate kutubu.”
Mtoa mada kakurupuka kumponda Yesu kwamba alikaa na watu waliopinda.

Angesoma Biblia kwa utulivu asingeanzisha huu uzi. Lakini kwa kuwa hamjui Yesu Kristo, na hajui alikuja kufanya nini duniani ndio kaleta uzi wa kitoto kabisa.

Mzee wa kupambania ubarikiwe sana kwa kumkumbusha mleta uzi ni nini kilichomleta Yesu Kristo duniani.
 
Wao ni wapumbavu, maana wao walimuona kwa macho, waliona Miujiza anafanya, sisi tunasikia habari zake kwa kupitia Manabii na tunaamini, Inamaana sisi tuna IMANI kubwa sana...
Hivi unaamini kuwa wewe ni zaidi ya Wafarisayo wa Zamani haujafika hata robo kwa Jinsi walivyokuwa wakishika sheria na maandiko😅😅

Sasa msikie yesu anavyowaambia wanafunzi wake..
Mathayo 5:20

Screenshot_20231031-102012.png
 
Hata angekuwepo aliyemuona kwa macho na kula naye ugali bado asingekuwa hai mpaka leo hii.still ungekuwa na wasi wasi tu na uhakika wa taarifa za Yesu.
Hapana kam angeandika kwa mkono WKe ningeamini ila sio hizi Pseudepigrapha au Apigrapha Tulizonazo
 
Mtoa mada kakurupuka kumponda Yesu kwamba alikaa na watu waliopinda.

Angesoma Biblia kwa utulivu asingeanzisha huu uzi. Lakini kwa kuwa hamjui Yesu Kristo, na hajui alikuja kufanya nini duniani ndio kaleta uzi wa kitoto kabisa.

Mzee wa kupambania ubarikiwe sana kwa kumkumbusha mleta uzi ni nini kilichomleta Yesu Kristo duniani.
Ndio maana watanzania mnashindwa kufanya reasoning za kawaida. Hata wewe hujaelewa maelezo yangu. Hakuna sehemu nilipomponda. Nilichosema ni kuwa watu waliokuwa wamemzunguka na lifestyle lake lilikuwa tofauti na lile ambalo jamii ya kipindi kile ilivyokuwa inaamini mtu kama masiah anapaswa kuwa hivi.
Hiyo ni mojawapo ya sababu hata hao Wayahudi hawamwamini mpaka leo wanahisi hajaja.
Hizo hoja alizotoa mimi sizikatai na zinaeleweka, hapa nazungumzia tu lifestyle na perception ya watu wa kipindi hicho.
Hata sasa akija hapa akawa anazunguka na masela watu hawawezi kumuamini. Unakumbuka goodluck gosbert alipoperform fiesta watu walisemaje? Ni kwasababu perception ya jamii ina picha ya mpendwa anafaa kuwa hivi, mpendwa hafai kuwa bar, mpendwa anafaa kuchomekea.
 
Mathayo 21:42 Zaburi 118:22-24
Yesu akawaambia je hamkupata kusoma katika maandiko, jiwe walilolikataa waashi hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni

Ina maana kuwa Yesu alikataliwa na Wayahudi na hata sasa watu wapo wanamkataa...

Ila pamoja na hayo alitushindia akatupa neema ya kufa na ufufuo..
 
Hivi unaamini kuwa wewe ni zaidi ya Wafarisayo wa Zamani haujafika hata robo kwa Jinsi walivyokuwa wakishika sheria na maandiko[emoji28][emoji28]

Sasa msikie yesu anavyowaambia wanafunzi wake..
Mathayo 5:20

View attachment 2798673
Mi sio Mfarisayo, Mimi ni Mlokole, nimempokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu...

Siongozwi na sheria naongozwa na Roho Mtakatifu
 
Mleta mada na vyanzo vingine kuhusu wasifu wa Yesu??
Yeah wasifu wa Yesu uliandikwa sehemu nyingi sana na watu wengi sana walielezea Hii ilikuwa miaka mingi sana baada ya kufa kwake...
Ni kama Sasa hivi Watu wengi Waanze kuelezea Kuhusu Historia ya kifo cha Karume na karume alikuaje..
Na wengine waanze kuandika sahzi kumuhusu karume japo tunaamini kwamba wengi waliokuwa vijana kipindi hicho mwaka 65 sio wote wapo unless ana miaka 120 na kuendelea au 100 na kuendela au 90 ...

Na ndo maana nampenda sana luka alisema hivi..
Screenshot_20231031-103551.png
 
Mleta mada na vyanzo vingine kuhusu wasifu wa Yesu??
Yeah wasifu wa Yesu uliandikwa sehemu nyingi sana na watu wengi sana walielezea Hii ilikuwa miaka mingi sana baada ya kufa kwake...
Ni kama Sasa hivi Watu wengi Waanze kuelezea Kuhusu Historia ya kifo cha Karume na karume alikuaje..
Na wengine waanze kuandika sahzi kumuhusu karume japo tunaamini kwamba wengi waliokuwa vijana kipindi hicho mwaka 65 sio wote wapo unless ana miaka 120 na kuendelea au 100 na kuendela au 90 ...

Na ndo maana nampenda sana luka alisema hivi..
View attachment 2798688
 
Back
Top Bottom