Tatizo la kununua Umeme wa LUKU: Waziri Kalemani amsimamisha kazi kwa siku 10 Meneja wa TEHAMA wa TANESCO

Hiyo mifumo ya kielectronic ndo inahakikisha serikali inapata mapato yake stahiki, vinginevyo kuwepo na hujuma watu wanataka kurudi kwenye zama za upigaji, mh. rais usikubali watu wachache wachezee mifumo kwa manufaa yao binafsi.
 
😆😆During a crisis ambayo haijakua solved,unaenda kumsimamisha probably the most knowledgeable person responsible anaejua undani wa hilo tatizo, na pengine alikua mbioni kulitatua! Ok! Utakaemteua kulimaliza atakua briefed na Nani?
 
Mimi binafsi nasema hivyo kwa sababu mambo mengi yameharibika na kama wahusika wapo TANESCO wafanye hivyo kama njia ya kuwajari wateja wao.
 
Napitia comments za wadau wengi. Kinatamkwa HUJUMAA kamanni kweli bac huenda Tz ndio taifa la kwanza kwa na watu au watumishi mazumburu kuku.
 
Hii kitu inaweza isisaidie, mana huo ni mfumo, kama mfumo umecollapse angewaacha wasolve kwanza, then awaite awaulize tatizo, akigundua kulikuwa na uzembe wa mojakwamoja basi awawajibishe. Angalia katoa muda mpaka saa nane,kwani saa nane si imefika na umeme bado haununuliki.
 
Waziri amemsimamisha kazi kwa siku kumi Meneja wa Tehama na Huduma za Biashara wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) Lonus Feruzi na wasaidizi wake Frank Mushi na Idda Njau.

Wamesimamishwa kazi kuanzia leo na Waziri wa nishati ndugu Kalemani, ambaye pia amemwagiza Mkurugenzi wa Shirika hilo Mwinuka kuhakikisha huduma hii inarudi haraka baada ya muda mfupi.

Pia soma > TANESCO wapata hitilafu katika mfumo wa kununua LUKU

 
Safi sana DR. Kalemani.

miongoni mwa mawaziri nimekuwa nikiwakubali na nina endelea kumkubali.

Wapo pia baadhi ya Mameneja wanapima kina cha Maji. Umeme kukosa nguvu, wameunganisha nyumba nyingi kuliko uwezo wa transfoma na wala hawana muda wa kukagua wao ni kuunganisha tu ndio wanajua.
 
Wafanyakazi watatu wamesimamishwa kazi kwa kushindwa kutatua tatizo la LUKU na waziri mwenye dhamana. Waziri amemuagiza Mkurugenzi Mkuu kuutangazia umma kurejea kwa huduma ya LUKU saa 8 mchana leo
Saa nane bado?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…