Tatizo la miguu kuwaka moto (neuropathy): Ushauri, Kinga na Tiba

Tatizo la miguu kuwaka moto (neuropathy): Ushauri, Kinga na Tiba

Wakuu, natumai mu wazima.

Kwa muda wa miezi miwili sasa nasumbuliwa na miguu ambapo inawaka moto na joints za vidole vya miguu zinauma balaa, maumivu yanaanzia kwenye angle lakini kuanzia hapo kurudi juu (hadi kichwani) niko sawa.

Nimeenda hospitali tatu tofauti mara tano lakini hawaoni ugonjwa na nimepima damu,stool na haja ndogo lakini majibu yanaletwa ni kwamba hawaoni tatizo. Siwezi kuvaa viatu kwani ni kama moto unawaka haswa huku kwenye kucha zinapootea miguu haina uvimbe wowote.

Kwa yeyote mwenye wazo la kunisaidia anakaribishwa ili mwenzenu niendelee na masomo vizuri kwani mimi ni mwanafunzi wa chuo mwaka wa kwanza.

Naomba kuwasilisha.
zima
 
Zamani kabla ilimu haijasambaa mtu akiumwa miguu inakuwa kama inawaka moto,watu wanajurge kuwa karogwa,kumbe haya mambo yana maelezo ya kisayansi
 
Wakuu, natumai mu wazima.

Kwa muda wa miezi miwili sasa nasumbuliwa na miguu ambapo inawaka moto na joints za vidole vya miguu zinauma balaa, maumivu yanaanzia kwenye angle lakini kuanzia hapo kurudi juu (hadi kichwani) niko sawa.

Nimeenda hospitali tatu tofauti mara tano lakini hawaoni ugonjwa na nimepima damu,stool na haja ndogo lakini majibu yanaletwa ni kwamba hawaoni tatizo. Siwezi kuvaa viatu kwani ni kama moto unawaka haswa huku kwenye kucha zinapootea miguu haina uvimbe wowote.

Kwa yeyote mwenye wazo la kunisaidia anakaribishwa ili mwenzenu niendelee na masomo vizuri kwani mimi ni mwanafunzi wa chuo mwaka wa kwanza.

Naomba kuwasilisha.
pole sana mi mwaka jana niliumwa huo ugonjwa mpaka nikawa siwezi kukanyaga nilizunguka hospitali kubwa zote unazozijua hapa mjini nikatumia kama milioni mbili sijapona uzuri nilikuwa na bima so sikutoa hela mfukoni,nilienda Aga Khan kuna dk mmoja mwanamke wa kihindi nimesahau jina lake nikummushe kesho nicheki vyeti vyangu,alinichoma sindano inaitwa neorobin injectiobn na nyingine siikumbuki na nikapewa food supliment ginsomin sasa nikikwambia nina uwezo wa kucheza mpira na kuruka kama ndama huwezi amini wakati nilikuwa nadhani naelekea kuwa mlemavuunaitwa peripheral neuropath
 
Nilikuwa na huo ugonjwa zaida ya mwaka
Ulianza kama masihara baadae ukaongezeka
Nashukuru kupitia jamii forum doctor nimepata maarifa kidogo
Nikaenda google kikaongeza upeo kidogo hivi sasa namshukuru m , mungu nimepona kabisa na nimejitibu mwenyewe kwa kusoma soma tu mitandao..
 
Mkuu nilienda hindu mandal hospital nikapewa hiyo neorobin za vidonge lakini sokupona
 
Wakuu natumai mu wazima kwa kudra za muumba. Siku chache zilizopita niliweka Uzi hapa jukwaani, nikiomba msaada wa ushauri ili tatizo langu la miguu kuwaka moto nipate namna ya kulitatua kwani ilikuwa ni miezi miwili imepita nikiwa na tatizo hilo na nisingeweza kuvaa viatu kutokana na maumivu niliyokuwa nayo.

Msaada wa mawazo: Miguu inawaka moto

Nashukuru wanajukwaa mlinipa ushauri wa kila aina na niliufanyia kazi na sasa nimerudi kuwashukuru wanajukwaa wote kwa moyo uliojaa upendo kwa kuguswa na hali niliyokuwa nayo. Sasa tatizo nililokuwa nalo limeisha na viatu ninavaa na chuoni ninaenda bila tatizo.

Mungu aibariki JF na Wanajukwaa wote. Upendo wa namna hii udumu milele na milele.

Asanteni sana.

#Mavindozii.
 
Hongera, ulifanya nini ili wenzako wenye tatizo kama lako wapate msaada
 
Tusaidie jinsi ulivyoweza kuyashinda hayo majaribu.
 
Tuta
pole sana mi mwaka jana niliumwa huo ugonjwa mpaka nikawa siwezi kukanyaga nilizunguka hospitali kubwa zote unazozijua hapa mjini nikatumia kama milioni mbili sijapona uzuri nilikuwa na bima so sikutoa hela mfukoni,nilienda Aga Khan kuna dk mmoja mwanamke wa kihindi nimesahau jina lake nikummushe kesho nicheki vyeti vyangu,alinichoma sindano inaitwa neorobin injectiobn na nyingine siikumbuki na nikapewa food supliment ginsomin sasa nikikwambia nina uwezo wa kucheza mpira na kuruka kama ndama huwezi amini wakati nilikuwa nadhani naelekea kuwa mlemavuunaitwa peripheral neuropath
Tutajie gharam na dozi ya hizo dawa. Tujipange kwenda.
 
Tuta

Tutajie gharam na dozi ya hizo dawa. Tujipange kwenda.
aga khan kumuona doctor 40,000.hizo dawa zilikula kama laki.ila wahuni wale hata kama wameshaujua ugonjwa lazima wakufanyie vipimo fulani wale hela yako.uzuri nilikuwa na bima bila hivyo ningepata shida sana
 
Mkuu nawashukuru wanajamii forums wote waliojitokeza kunipa ushauri na sasa maumivu kwisha kabisa.Credit to jamii forum.
 
Mkuu nawashukuru wanajamii forums wote waliojitokeza kunipa ushauri na sasa maumivu kwisha kabisa.Credit to jamii forum.

Hongera sana kaka kama unajisikia vzr ss hv.Tueleze na wengine umetumia dawa gani ukapona
 
Kapige MRA inawezekana kuwa baadhi ya mishipa imesinyaa.. Mie nilikuwa na tatizo Kama lako.. Nenda Hindu mandal kamuone Dr Mahinda.. Atakusaidia
 
Baadhi ya Tiba

Limao

kuhusu limao, mhusika anapaswa kuosha miguu na nyayo kwa maji ya moto na sabuni na baadaye kukata limao katika vipande viwili kisha kupaka sehemu zile ambazo huwa unahisi kama kuungua.

Maji ya uvuguvugu /chumvi.
Wakati umekaa, tumbukiza miguu ndani ya maji ya uvuguvugu, yaliyoongezewa na chumvi ya mawe yakiwa ndani ya karai kwa muda wa nusu saa, lakini wakati umetumbukiza miguu unakuwa unaosha sehemu ambazo huwa unajihisi kuwaka moto.

Msubili
Osha miguu na nyayo kwa maji moto na sabuni, kisha pondaponda jani la msubili na upake sehemu zote unazojihisi kuungua.
 
wasikupotezee muda tatizo hilo linaitwa peripheral neuropath nenda aga khan kuna doctor fulani nimemsahau jina mama mmoja wa kihidi specialist wa mishipa atakuchoma sindano mbili ugonjwa kwisha mi nilikuwa na huo ugonjwa na sina uzito mkubwa nina kilo 60 tu na nina futi sita kasoro baada ya hizo sindano sasa niko fit
Mkuu,
Ninasikitika sana kukujulisha na kuwajulisha wagonjwa wote kwamba huyo Mama wa Kihindi alikwisha ondoka nchini. Amerudi kwao India.
 
Back
Top Bottom