Tayari Sabaya amechomoka, kama alipewa maagizo toka juu ujambazi anahusika vipi?

Kazi za kiofisi ufanywa kwa maandishi ndio maana hata alupoteuliwa alipewa cheti cha uteuzi.je anayo maandishi yaliyo mwelekeza kufanya mambo hayo?je hayo maelekezo yako ndani ya utendaji kazi ya ukuu wa wilaya kisheria?hapo ndipo panaposubiriwa.
 
Tunawasihi viongozi wetu pamoja na maugomvi yao binafsi lakini wawe makini isije ikatokea makosa yaliyofanyika 2015 wawe makini yasijirudie tena, aliyeachiwa madaraka wakati huo hakuwa mtu sahihi kaivuruga sana nchi hata hivyo tumshukuru mola wetu kwa aliyoyatenda.
 
Idungunde
sahau SABAYA atachomolewa kwa msamaha wa rais ikimpendeza baada yakutumikia kifungo

Mpango lazima akatoe ushahidi na huyo gavana
 
Sijui Kama umepata muda wa kufikiria na kutumia akili yako vizuri kabla ya kuandika
Nchi haingozi kwa maagizo ya utashi wa mtu binafsi
Inaongozwa kwa majibu wa katiba na sheria
Inaama rais angemtuma kuua angeuwa tu kwa sababu ni agizo la rais ?
Kila agizo lazima liwe ndani ya sheria za nchi
Hiyo ya kutumia magari ya serikali kutenda uhalifu ni kosa lingine ,
Na kwenda kutekeleza operation nje ya eneo lake la kazi ni kosa vile vile Kila cheo kina mipaka yake
In short amefunua ukweli ambao utawacjafua wengi
 
Anachomokaje hapo? kwanza mwendesha mashitaka atamuuliza ulitumwa kupora na kujeruhi na kufanya ujambazi? hapo sasa ndio atatakiwa kujibu kama alitumwa kufanya ujambazi lakini hata kama alitumwa kufanya ujambazi bado haimuondolei hatia ya kufanya uhalifu kama atakutwa na hatia ya kufanya ujambazi na uhalifu.

Nina hakika Sabaya alitumwa kushiriki kwenye operation lakini sio kufanya uhalifu kama alifanya uhalifu imekula kwake
 
Kwani kuwataja hao wakiomtuma ndiyo ushahidi tosha. Kama ni kweli ngoja Tusubiri kama watakuja mahakamani kuthibitisha hayo.
 
Una maana JPM alimtuma Sabaya kwenda kufanya jinai? Hebu kuwa na heshima kwa JPM japo kwa siku moja tu.
 
Ila wewe jamaa una akili ndogo sana sana. Issue sensitive hivi unakuja na hoja nyepesi kiasi hiki kweli?
 
Nilikuwa nimekublock, nilipoona post hii nikadhani akili imekurudi, kumbe unamtetea Sabaya kuwa alitumwa atende kinyume na Sheria hivyo Hana hatua. Nimechoka!
 
Sabaya labda achomoke kichwa kitengane na kiwiliwili na sio kuchomoka vinginevyo.
 
Sabaya kishatia ugoro puani sasa ni mwendo wa chafya aliowataja wanakinga kisheria sasa ngoja mahakama idili na huyu kapuku wa kimasai aliyefanywa chambo bila kujitafakari maisha yake baada ya jiwe kutokuwepo
 
Wwe ni mshamba
 
Kwa hiyo ukitumwa kuiba na ukaiba huna hatia?
 
Ana ushahidi wa anacho kisema rejea kesi ya Yule polichi bila kuingilia mwenendo wa shauri la Simba au kesi yoyote ya jamii forums
 
Uhalifu ni uhalifu, hata kama umegizwa toka juu, kila Mtu Yupo chini ya sheria! Kwa maneno mengine, aliye fanya na aliye agiza, ni majambawazi wakubwa!
 
Mkuu kuna kitu umekisahau au umejisaulisha, mali za serikali zinatumiwa na binadamu tunaowaita watumishi serikali.
Ikitokea hao watumishi wakakosa uhadilifu hizo mali ni rahisi kutumiwa vibaya.

Ukumbuke madaraka nayo ni nyenzo, kuna watu wanatumia vibaya nyenzo hii kinyume cha utaratibu ndo maana huwa
wanashtakiwa. Hapo sijaongelea silaha ambazo pia ni mali ya serikali,lakini tumeshuhudia kesi nyingi dhidi
ya watumishi waliotumia vibaya nyenzo hizo.
 
Ninachojifunza hapa ni kutufanya lolote kwa akili ya kutumwa.
Tumwa kwa mujibu wa sheria nje ya hapo jumba bovu linakuangukia.
na hutakuwa na wa kukuopoa.
Mfano mahakama ikimtaka awataje watu hao,vinginevyo huo ushahidi unatupiliwa mbali
maana utachukuliwa kama uongo mwingine wa kutaka kujinasua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…