TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

Tunataka muonekano angavu sio wavumbivumbi, pia navipind view vya kisasa zaidi

Vipindi vya kisasa kama vipi? Ungetaja mifano ingekuwa poa zaidi mkuu. Kutoa maelezo ya jumla jumla hakusaidii sana, kunasaidia nusu.
 
Watanzania tunaitaji kuyaona matangazo ya live pale timu ya taifa ikicheza ndani ya Tanzania na inje ya Tanzania,sio cheleko cheleko mala jiwe akitumbua bila utalatibu! Mmenielewa?
 
 


1. Rekebisheni volume (ukubwa wa sauti) za matangazo ya biashara.
Mtu unasikiliza taarifa ya habari kwa sauti ya kawaida, mara linatokea tangazo la tigo, volume iko juuuuuu, tunanza kutafuta remote ili kupunguza sauti. Tangazo likiisha inabidi kupandisha tena.

2. Usomaji wa habari za kimataifa:
Someni kwa vituo. Sio mnasoma kama mnaimba.
Mnashindwa hata kuchomekea maneno ya kuunganisha/kutenganisha habari kiasi kuwa habari ya Uturuki haijaisha vizuri, tayari inakuwa imeunganishwa na habari ya Marekani as if ni taarifa moja.

3. Ukamilifu wa habari.
Kamilisheni taarifa. Sio mnajiunga na mtangazaji aliye nje ya studio anaeleza kidogo na kabla taarifa haijaeleweka vizuri, mnakatisha.

4. Nitarudi kesho nikiwa kwenye computer.
 
Kwa haya uliyoeleza yote ni uzembe na lack of seriousness. Hapo wazidishe umakini na u serious.
 
Hivi TBC kumbe bado ipo? Na RTD je? Hawawezi kubadilika wale. Ndio maana siangalii vipindi vyao.
 
Travic unaangukia kwenye mtego ule ule wa kukataa maoni ya wananchi ambayo yapo kinyume na matarajio yako

Kumbuka hapa ni JF wadau wanaongea openly. Na anayekwambia ukweli anakupenda.

Ushauri mkubwa umetolewa katika nyanja kuu kama tatu hivi.

Moja, kuweni fair/impartial. Mnafahamu maana yake. Kama ni TV ya umma na ionekane hivyo. Hilo wamelisema na ndio kubwa sana.

Pili, boresheni ubora wa vipindi pamoja na ubora wa picha. Wadau wametoa mifano tatizo lilipo (aina ya vipindi) na vipi viongezwe. Wengine wamesuggest aina ya quality ya picha. Hadi wengine wamejitolea kuja kuwasaidia upande wa graphics.

Tatu, wadau wameshauri kuwa na channel zaidi ili kuaccommodate mahitaji ya vijana watoto wazee wapenda michezo nk lakini pia muonekano wa kimataifa wa TV yetu! Tunaweza kiwa na channel ta habari tu (TBC news) kisha nyingine ya mambo ya kawaida (documentaries-wildlife, elimu, ziara za tunatekeleza, this week in perspective, shuleni/watoto, science and engineering) halafu TBC Sport/music/emtertainmenr ( mpira wa nje na ndani tafuteni haki za kuonyesha japo mara moja moja, mieleka, muziki kwa sana wa vizazi vyote, bongo/nigerian movies, mambo kama hivyo kwa mpangilio maalumu).

Kutekeleza hayo ni dhahiri mnahitaji revamp ya hali ya juu, kuanzia staff training/upgrading, vifaaa, ubunifu nk.

Hamu yangu ni kuona kuwa mtanzania anaweza kuyapata haya yote in one package yaani TV station ya taifa ambayo kwa uchungu analipa kodi kuiwezesha. Lakini pia mtaweza kujiendesha na hata kutoa dividend kwa serikali kama mtatekeleza ushauri wa wadau humu.

Nawatakia utekelezaji mwema.
 

Ha ha ha ha ha no 4 umenifurahisha sana lakini nikuambia sio rahisi huwa wanaeka lile sura linatotishia hata mtoto wakati wa kula ukimwonyesha lazia ale.. So ni ngumu kuweka hiyo TBC3 kwenye hotel wakati kuna ile sura ile ukilogwa ukaiona asbh jua siku yako yote itakuwa kapa
 
Wale ambao hawajui hata kama hiyo chanel ipo kwenye progtam ya TV wao watoe maoni wapi?
 
Kazi nzuri sana na tulipofika sio pabaya endeleeni kuboresha vipindi na kuajiri watangazi vijana ili twende na wakati. ila hongereni sana, mimi naitazama kila wakati.

#DG
 
Sijajua kwa sasa ila hapo nyuma TBC zilikuwa zimegawanyika, 1,2...maana Kwa Ss tbc hawaelewi wako mlengwa gani, siasa, Habari, makala Au burudani... Kila sehemu wanajaribu jaribu, Kwa maoni yangu tbc 1 ingejikita zaidi kwenye Habari pasipo ubaguzi, mf kama habari za siasa ziwe kote kote isiwe chama fulani tu, sawa haiwezi kuwa 50,50 basi angalau chama pendwa kiwe angalau 60 na vilivyo salia viwe 40,
Pia watangazaji wenu muwavalishe vizuri, wawe wa kisasa cha mwisho studio zenu za Habari Dah! Ni za kizamani mno! Mf kuna kipindi Nilikuwa mnamuhoji sikumbuki jina lake ila alikuwa bondia wa zamani, mtangazaji amekaa chini, hana uelewa na mchezo wa ndondi, hajui historia yake vizuri hata maswali aliyokuwa anauliza ni mepesi mno....
Kuna kipindi flani mlikuwa mnamuhoji mtu wa serikali,kamera za studio zikaonesha miguu, yaani vumbi tupu basi angalau mungekuwa na mtu anaehusika na mavazi, maana kipindi sio tu yale mnayoongea Bali set up nzima kuanzia studio, muonekano

Sauti pia mara iwe juu mara chini.....
 

Kaizer,

Naomba radhi kama imeonekana nakataa maoni au siruhusu watu kuzungumza openly. Nilikuwa najaribu kuzuia tusiingie kwenye mtego wa kulalamika tu tukasahau kueleza tunajinasuaje kwenye changamoto zilizopo.

Ni imani yangu tunaweza kuzuia mihemko na kushauri kwa lugha elekezi bila kutusi na kulaumu pasipo kutoa mapendekezo ya nini kifanyike. Jambo ambalo nimeliona kwa wachangiaji wengi.

Mimi sio mwakilishi wa TBC. Ni mdau tu na mwananchi wa kawaida ambaye nalitakia mema shirika hili la taifa lifanye vizuri zaidi ya sasa.

Nakubaliana na ushauri wako kuhusu maboresho gani yafanyike. Kila mtu angetoa maoni kwa mtindo huo basi mpaka sasa tungeshapata ya kutosha na kufikia lengo la mnakasha huu.
 

Maoni mazuri sana. Tafadhali urejee ili umalizie mkuu. Karibu sana.
 
Wao wanachojali ni mshahara kwaiyo wanachofanya ni kumfurahisha anayefanya waipate iyo mishahara they don't care hata TBC ikifa na sidhani Kama Licha ya michango yote iliyotolewa humu ka itafanyiwa kazi hawawezi kufanya chochote ambacho bwana Yule hatakifurahia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…