TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

Hapo naomba kutofautiana na wewe. Kwa Rais aliepo madarakani swala ni kujenga hoja baada ya kujitathmini. Taasisi kama TBC imezeeka kimuundo na kimfumo. Kwa kutizama tu vipindi vyao unajua jinsi wanavyoplan. In incremental. Ya mwaka ujao ni ya mwaka jana badilisha hapa na pale ...maisha yasonge. TBC inahitaji total overthaul. Unapotafuta mkuu wa taasisi na vitengo unatafuta mtu mwenye vision na uwezo wa kusimamia vision. Nani asieikumbuka National Housing ilivyobadilika baada ya kupata viongozi sahihi? CRDB Je, nk. Taasisi zimekuwa tamu mpaka watu wameanza kupigana vikumbo kwa fitna.
Tubadili mbinu jinsi ya kutafuta CEOs na waachwe watekeleze vision zao. Political interference iwe pia tamed.
Utamlaumu Rais kama kweli anaingilia kazi nzuri. Lakini kama kazi ni mbaya unamtegemea akae kimya?
Tuwasaidie TBC kwa kuwaeleza njia na mbinu sahihi za kupitia watoke hapo walipo maana kweli wana hali mbaya.
Its too sad to see our cash cow being mismanaged.
Ng'ombe huyo alipaswa kutoa lita 20 lakini anayoa lita 5 japo anakula majani yaleyale.
Majani sio yale yale yameongezwa mara dufu,kama hujui uliza kule kwa mpwa wa mzee wanavyochotewaga bila idadi.Kule ni kujumlisha tu hakuna kutoa.Mimi sijuagi siku nyingi huko kwenye kioo picha ikoje maana funguo nilitupa chooni choo cha tundu kwa hasira siku nyingi.

Hapa nataka kushauri.Watanzania tumshauri mzee awabambikize vituo vingine vyote kesi za uhujumu uchumi,kukwepa kulipa kodi akianzia na Azam,Itv,ile kule Mwanza,claud Abood,Upendo nk.Wapelekwe mahakamani,hukumu itoke kwa mzee vifungiwe milele. Hapo labda watapatikana watazaji.Lakini sio mimi.Funguo sina niacheni.
 
Ndugu zangu mnaonitumia jumbe PM. Mna nafasi yenu mbinguni. Mawazo ni mazuri sana na yanaweza kutumika kuendelea kusaidia TBC1 kufanya mapinduzi. Hakuna linaloshindikana.

Naomba muendelee kuyaweka hapa hadharani. Kwa wale mnaoogopa kutambulika kutokana na ID zenu au nafasi mlizonazo (verified accounts) basi tuendelee kuwasiliana, nitawasilisha hapa kwa niaba yenu.

Kwa msisitizo >> Ujumbe muhimu kwa wanaodhani nafanya kazi TBC (Shirika la Utangazaji Tanzania) - JamiiForums
 
Wanajamvi, leo kama kawaida sitakua na merefu. Nataka tuishauri serikali basi irudi kwenye misingi ya mali ya umma. Mimi ni mmoja wa watazamaji wa runinga hii ambayo tangu enzi tulijurishwa kua ni Mali ya Umma na inaendeshwa kwa kodi zetu walima kahawa wa Itahwa, Korosho - Tandahimba ,pamba - maswa nk

Basi katika kulijua ili bila shaka hiki kituo cha runinga ilibidi kuangalia maslahi ya Umma kuliko porojo,propaganda,mhemko ya uchama na kazi za chama cha Siasa asa CCM. Inafika muda kweli mpaka unaweza kuniuliza hii ni runinga ya umma wa Chama. Mh.Pole Pole ,Mh.Bashiru (GS) CCM yaani unatumia CCM kama watakavyo kufanya propaganda za CCM. Ina kua aibu kuona chombo kama hiki kinakua na upande ( affiliated) na chama cha Siasa. Hii sio sahii kabisa.Kazi na propaganda za CCM tutumie TV yetu ya Chanel Ten ambayo wanaccm tumetoa pesa zetu kuinunua.

Mwisho,nilitarajia kua kwakua watoto ( wanafunzi) wapo nyumbani basi huu ulikua muda muafaka TBC kupanga vipindi vya masomo kwa vijana wetu pamoja na kutoa elimu kuhusu Covid-19. Kuna vijana wa kidato cha sita,pili ,darasa la saba na kidato cha nne ambao niwatahiniwa mwaka huu. Kwakua wapo nyumbani basi TBC kama bado kweli ni mali ya Umma huu muda ungetumika hivyo kuliko kufanya dhuluma kwa walipa kodi.
Ni ayo tu kwa leo.
CCM TUITUMIE CHANNEL TEN MAANA NI MALI YETU
 
Ujumbe huu umfikie CEO wa TBC Dr Ayoub Ryoba.

Kunapokuwa na matukio ya kitaifa muwe mnajiandaa " vyema" kuyarusha hewani na kama hamuwezi jukumu hilo wapeni Channel ten au hata luninga za kampuni binafsi.

Ikiwezekana wapeni hata Jf watanzania wote watafikiwa kwa 100%. Mnatuchosha kwa kweli.

Maendeleo hayana vyama!
 
kuna siku walirusha ile cartoon ya Akili na kulikuwa na tukio kubwa la kitaifa muda huo, natune nakutana na “Akili akili hellow..”
 
OB Van itakuwa inamatatizo. Sijui kama TBC walitegemea kwamba wangehitajika kurusha matangazo toka Chato leo.inategemea wamepewa lini taarifa.
 
Sasa hivi mtangazaji kaweka CD iendelee yeye ameenda kunywa supu[emoji1787]

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Ob van itakuwa inamatatizo.sijui kama TBC walitegemea kwamba wangehitajika kurusha matangazo toka chato leo.inategemea wamepewa lini taarifa
Mkuu samahani naomba kuuliza, kuna siku niliona katika Documentary fulani ya kumbukumbu za hii nchi yetu kuna kifaa kipo kama briefcase walisema ndicho kilitumika kurusha matangazo ya vipindi kutoka zanzibar miaka hiyo ya 70 huko, swali langu ni je inawezekana vipi mpaka leo 2020 TBC wasiwe na vifaa hivo vya kisasa ila wategemee van ile ambayo kwa uelewa wangu ni moja au hazizidi 5 hapa nchini.
 
Usilaumu TBC mbona bata ikulu wameshindwa kwenda live kwenye Chanel yao ya you tube, wanamjua boss wao hachelewi kuropoka.
 
Ujumbe huu umfikie CEO wa TBC Dr Ayoub Ryoba.

Kunapokuwa na matukio ya kitaifa muwe mnajiandaa " vyema" kuyarusha hewani na kama hamuwezi jukumu hilo wapeni Channel ten au hata luninga za kampuni binafsi.

Ikiwezekana wapeni hata Jf watanzania wote watafikiwa kwa 100%. Mnatuchosha kwa kweli.

Maendeleo hayana vyama!
Hivi kwa nini Watanzania ni mambumbumbu kiasi hiki?! Huhitaji kuwa na PhD kujua kuwa tatizo halipo TBC!
 
Back
Top Bottom