TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

Asante kwa maoni. Namba 2, 4 na 5 ni mawazo elekezi. Hayo mengine ni malalamiko na kejeli ambazo nashauri tujaribu kuziepuka kwa sababu zinaficha ushauri.
Mpaka muambiwe jamani...mbona wengine wabunifu...aya bhana ngoja tuone kama hayo mapendekezo yatatiliwa maanani maana vitendo ni vichache kuliko kujitetea
 
Acheni kutumika kisiasa! Tunashindwa kuwelewa kama nyie ni Television ya Taifa au tawi la chama?
Ubora wa picha ni sifuri kabisa!
Nchi hii imejaa vijana zaidi ya 70% nyie asilimia 80 ya vipindi vyenu ni vya kizee!
Mnashindwa hata kuonesha mechi ya Taifa stars mmekalia ziara za viongozi wa chama wakitembelea matawi sijui kigoma gani huko!
Mmetangaza kufunga mitambo mipya ya kisasa na picha ndo kabisa zimerudi zile za kiwango cha chini kabisa!
Subirini na wengine wanakuja na mjiandae kwa POVU ZAIDI
Kwani ukelazmishwa kuangalia TBC acha ujinga wako
 
Umeishia darasa la ngapi mkuu?
Nenda shule ulosoma kadai ada yako maana hata kuandika hujui achia mbali hoja za msingi za kujibishana na mm!
Na kama wewe ndo muangaliaji wa TBC ndo maana wanazidi kushuka kila kikicha!
Sema wewe utakuwa hulipii wapenda vitu vya bure.. Kwani haupo kwenye list ha dudu baya
 
Naamini mna nia ya dhati ya kufanya mabadiliko chanya TBC1; wanajamvi wametoa maoni mengi mazuri ambayo naamini hata dhamiri zenu wahusika zinakushuhudieni kwamba ni maoni yenye kujenga, ni vema kuyachukua na kuyafanyia kazi maoni hayo pasipo kujali sana kwamba yamewasilishwa ktk sura au namna gani.
Mkiamua kwa dhati, inawezekana.
 
Maajabu ni kwamba hata bibi yangu haangalii TBC juzi kati nme mtembelea nika tune hio channel yenu akaniuliza mjukuu wangu hua una angalia hio channel? nikazuga eeh bibi akasema mh! unaroho ya ushujaa
 
Ndugu WanaJF,

Kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na hata hapa JF kuhusiana na changamoto ya vipindi vya Televisheni ya Taifa (TBC1). Malalamiko hayo yameegemea zaidi katika eneo la ubora wa vipindi na ubunifu.

Kwa bahati nzuri, Mkurugenzi pamoja na Watendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ni wadau wakubwa wa JamiiForums na huwa wanafuatilia taarifa na mijadala mbalimbali inayoendelea hapa. Hivyo tukiitumia vyema nafasi hii, tutawasaidia kuboresha maeneo ambayo yanatakiwa kurekebishwa kwa haraka.

Naomba tutumie uzi huu kutoa maoni, ushauri na mapendekezo kuhusu aina ya vipindi na ubunifu ambao ukitumiwa utasaidia kuifanya televisheni hii ya taifa kuvutia kutazamwa na kufurahiwa.

Tumeshalalamika sana. Sasa ni wakati wa kuchukua hatua na kutaja suluhu kwa mifano ili kuimaliza changamoto hii kabisa.

Karibuni sana.
Ubora wa picha unaiodhoofisha taasisi yenu ya TBC........
 
doh! the TBC is among of dhe television which deals with one chama,foristance ukada wa ccm and there is more,..ngoja waje wengine wadadavue huko chini
 
Mtakapoacha kutumika CCM na mkatafuta habari ambazo hazina upendeleo na mkatoa fursa kwa kada zote kutoa maoni yao mtabaki vile
Vile gamna watazamaji, muda sana sijaitazama na hata wakati wa habari naangalia BBC news.
Iweni wabunifu ktk habari burudani na matukio
 
Back
Top Bottom