TCRA: Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole kinatolewa pasipo kuzingatia misingi, sheria na kanuni za huduma ya utangazaji

TCRA: Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole kinatolewa pasipo kuzingatia misingi, sheria na kanuni za huduma ya utangazaji

Hapana hizi sheria kali za maudhui ya mtandaoni/sheria ya huduma za habari na takwimu zilipitishwa kipindi polepole ni katibu NEC!!

Je hakujua hizo sheria ni kandamizi kiasi aje kulia lia sahivi? Kipindi anazuia blog zenye mawazo kinzani zisi operate alikua hajui umuhimu wa uhuru wa maoni?

Cha kuchekesha hyu polepole anaweza gombea Urais 2025 kupitia ACT alafu ataanza kulia lia tume huru ilihali alipokua na cheo CCM hakukumbuka umuhimuwa tume huru!!

Fundisho ni kuwa ukipata cheo andaa mazingira mazuri ya kesho yako kwa kutovunja madaraja yote uliyovuka kufikia hapo ulipo; otherwise ukipoteza cheo utashindwa kusimama tena maana atakayerithi kiti chako atatumia sheria hizo hizo mpya kukunyoosha
Inaitwa 'a taste of your own medicine'.
 
😂😂😂,chakubanga enzi za mwendazake wakati anatembelea V8,ndipo zilipitishwa hizi Sheria za hovyo na kwasababu alijua haziwezi kumgusa basi akawa anakula tu bata kwenye V8 na kuwananga wengine!
Leo hii kisu kile kile kinapita kwake,na ana bahati maana angeweza kubambikwa kesi za uhujumu uchumi akasota jela bila dhamana!
 
Mbona TCRA imeshindwa kuwafungia akina Maria Sarungi TCRA wakati maudhui yao ni ya hovyo sana kuliko hayo ya Polepole?
 
Kamati ya Maudhui ya TCRA imesema kipindi cha Shule ya Uongozi cha Mbunge Humphrey Polepole kinatolewa pasipo kuzingatia misingi, sheria na kanuni za huduma ya utangazaji. Kamati imeongeza kuwa maudhui ya kipindi ni ya upotoshaji na yanayoweza kusababisha taharuki kwa wananchi.

Sasa kiki ya penalt tayari, mpira wetu Polepole ana hanjahanja, goli nani analifunga!

======

KAMATI ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kipindi cha Shule ya Uongozi cha Mbunge Humphrey Polepole kinatolewa pasipo kuzingatia misingi, sheria na kanuni za huduma ya utangazaji huku kamati hiyo ikisimamisha kipindi chake cha Shule ya uongozi na kumpa masharti ambayo anapaswa kuyatimiza ili kirudi hewani.


Akisoma hukumu hiyo, baada ya kusikiliza upande wa Kamati na Upande wa Utetezi, Mwenyekiti wa Kamati, Habbi Gunze amesema maudhui ya kipindi cha shule ya uongozi yalikuwa ni ya upotoshaji na yanayoweza kusababisha taharuki kwa wananchi.

"Kuhusu kuwapanga wamachinga, Humphrey Polepole Online TV iliwatuhumu viongozi wa Serikali kuhusu kutofuata maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu ya kuwapanga vizuri wamachinga. Kituo hiki kimevunja kanuni na maadili ya uandishi na utangazaji kwa kutowapa nafasi viongozi hao kutoa ufafanuzi juu ya tuhuma alizotoa.

"Polepole alitoa maneno ya uongo na udharirishaji kwa viongozi akisema ni waoga na hawajitokeizi kutoa ufafanuzi kuhusu deni la Taifa bila kuwapa nafasi viongozi hao kufafanua madai yake wakati viongozi waandamizi wa serikali akiwemo Waziri wa fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba mwezi Juni alisema bungeni kuwa deni la taifa ni himilifu.

"Katika utetezi wake alisema amejikita katika utoaji wa elimu tu bila kuzingatia mizania na kwamba TV yake si kama vyombo vingine vya habari vinavyotoa maudhui ya habari, yeye anatoa elimu tu. Pia alidai kanuni hazijitoshelezi kwani hazielezi kwa mtu anayetoa maudhui ya elimu afanyeje, jambo ambaloi si kweli kwani kanuni zinajitosheleza na zinatoa mwongozo wote.

"Kamati imebaini kuwa Polepole TV haina waandishi wenye taaluma ya uandishi wa habari hivyo kukikua misingi ya uandishi na imemuelekeza ahakikishe anazingatia uchaguzi wa maneno yenye sitaha, kuzingatia misingi, kanuni na maadili ya utoaji maudhui mtandaoni.

Maamuzi ya Kamati

Kama imejiridhisha kuwa Polepole TV imekiuka shria za mawasiliano kwa njia ya kieletroniki, hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 44, kifungu kidogo cha kwanza, sehemu G cha sheria ya mamlaka ya mawasiliano ya Tanzania, sura ya 172, na marejeo yake ya mwaka 2017, na kanuni ya 21, kanuni ndogo ya tatu na sehemu A ya kanuni tajwa hapo juu, Kamati inatoa adhabu zifuatavyo.

Kituo kinapewa onyo kali. Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole TV kusimamishwa kwa muda mpaka pale atakapofanya yafyatayo. Kuwa na wafanyakazi wenye taaluma ya uandishi wa habari na utangazi na kuleta tija na ufanisi katika vipindi vyake. Kuhakikisha vipindi vyake vyote vinazingatia sheria, misingi na kanunia za uandishi na utangazaji wa habari pamoja na masharti ya leseni yake.

"Baada ya kuzingatia maelekezo hayo Kituo cha Humpohrey Polepole kitatakiwa kutoa taarifa TCRA ambapo TCRA ikijirishisha kuwa maelekzo yote yamezingatiwa kipindi cha Humphrey Polepole kitajrejea na kitakuwa chini ya uangalizi wa TCRA kwa muda wa miezi sita.

Uamuzi huu umetolewa leo jijini datr es Salaam, uamuzi wa kukata rufaa kupitia FCT upo wazi ndani ya siku 21.

Mwenyekiti wa Katai ya Maudhui ya TCRA, Habbi Gunze.
Unadhani_huyu_MHUNI_anafanya_Nini_hapa%3F%0A%0AA._Anahalalisha_UHUNI%0AB._Anahalalisha_wizi_wa...jpg
 
1639749210087.png

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imemtaka aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa (CCM) ambaye kwa sasa ni Mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole kusimamisha maudhui ya kipindi chake cha Shule ya Uongozi kinachoruka kupitia Humphrey Polepole Online TV.

Uamuzi huo umetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Hans Gunze ambapo amesema uamuzi huo unakuja baada ya kutenda makosa matatu ikiwemo kuzungumzia Deni la Taifa, Virusi vya Corona na suala la Machinga (Kwamba Wakuu wa Mikoa hawakufuata utaratibu).

"Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole Online Tv kinaamriwa kusimamishwa kwa muda hadi Mmiliki atakapohakikisha anakuwa na Wafanyakazi wenye taaluma ya Uandishi wa Habari na Utangazaji ili kuleta ufanisi na tija katika vipindi vyake, pili kuhakikisha vipindi vyake vyote vinazingatia sheria, kanuni, misingi na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari na leseni yake"

"Pia baada ya kutekeleza maelezo hayo kipindi cha Humphrey Polepole Online kitatakiwa kutoa taarifa TCRA kuwa maelekezo yote yamezingatiwa na kuwa kipindi kitarejea chini ya Uangalizi wa TCRA kwa miezi 6, haki ya kukata rufaa ipo wazi ndani ya siku 21 Kisheria kuanzia siku ya kutolewa uamuzi"
#MillardAyoUPDATES
 
Pale mchinjaji anapochinjwa. Ila tuache Mungu aitwe Mungu. Leo hii mtu ambae alikuwa na uwezo wa kusema na kufanya lolote kwenye nchi hii anapangiwa cha kusema na kufanya. Ama kweli kila kitabu na zama yake.

Walio karibu na mzee kijana wampe moyo, maana huyu jamaa kwa jitimai anaweza jinyonga na zile toilet paper zake.
 
View attachment 2047592
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imemtaka aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa (CCM) ambaye kwa sasa ni Mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole kusimamisha maudhui ya kipindi chake cha Shule ya Uongozi kinachoruka kupitia Humphrey Polepole Online TV.

Uamuzi huo umetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui wa TCRA, Hans Gunze ambapo amesema uamuzi huo unakuja baada ya kutenda makosa matatu ikiwemo kuzungumzia Deni la Taifa, Virusi vya Corona na suala la Machinga (Kwamba Wakuu wa Mikoa hawakufuata utaratibu).

"Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole Online Tv kinaamriwa kusimamishwa kwa muda hadi Mmiliki atakapohakikisha anakuwa na Wafanyakazi wenye taaluma ya Uandishi wa Habari na Utangazaji ili kuleta ufanisi na tija katika vipindi vyake, pili kuhakikisha vipindi vyake vyote vinazingatia sheria, kanuni, misingi na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari na leseni yake"

"Pia baada ya kutekeleza maelezo hayo kipindi cha Humphrey Polepole Online kitatakiwa kutoa taarifa TCRA kuwa maelekezo yote yamezingatiwa na kuwa kipindi kitarejea chini ya Uangalizi wa TCRA kwa miezi 6, haki ya kukata rufaa ipo wazi ndani ya siku 21 Kisheria kuanzia siku ya kutolewa uamuzi"
#MillardAyoUPDATES

Polepole alichelewa kujua kunyamazishana ni dhuluma.

Tumedhulumiwa sana!

Hata hivyo tuungane kupinga dhuluma.

Kumshabikia dhulumati dhidi ya yeyote haina tija yoyote kwa yeyote.
 
Mwaka mmoja nyuma Polepole hakufikiria kabisa kwamba mapito anayopitia leo angeyapitia..

Hata ungemwambia hii sheria ya TCRA ni mbovu na inaumiza raia asingekuelewa ndio kwanza angekujibu ni sheria ya kuwanyoosha wahuni...

Leo Polepole amekuwa mhuni kwa kutofuata sheria na ananyooshwa kweli kweli ndugu zangu.
 
Back
Top Bottom