Temeke: Meya wa Manispaa aanzisha kampeni ya kuuza Shule ya sekondari Kurasini kwa Mwekezaji

Temeke: Meya wa Manispaa aanzisha kampeni ya kuuza Shule ya sekondari Kurasini kwa Mwekezaji

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Meya_wa_Manispaa_ya_Temeke_Abdalah_Mtinika_(CCM)_anatuhumiwa_Kushawishi_viongozi_wa_Manispaa_h...jpg

Hii ndio Kashfa mpya inayozunguka kwenye Manispaa hiyo kwa sasa , ikiwa ni siku chache tangu kashfa ya Mwenyekiti wa ccm wa wilaya hiyo kutafuna zaidi ya sh. mil 300 za vikundi kuibuliwa.

Mstahiki Meya Abdallah Ntinika anatajwa kuwashawishi kwa nguvu kubwa viongozi wa Manispaa hiyo ili Waiuze Shule hiyo ya umma, ambayo tayari imekwishapelekewa pesa za serikali , zinazoitwa hela za COVID 19, na tayari madarasa saba mapya yakiwa yamekwisha jengwa.

Sababu hasa ya Meya huyo kufanya jambo hilo la Uhujumu Uchumi bado hazijafahamika, ingawa dalili za awali zinaonyesha kwamba kuna ushawishi wa 10%.

Kama kawaida yetu tutaendelea kukuletea kila kinachojiri kwenye manispaa hiyo baada ya Nzi wetu kuahidi kubaki ndani ya manispaa hiyo kutudokolea kila uhondo
 
Weka wazi makilakitu yao hapa Mali ya umma tena taasisi inawezaje kuuzwa hovyo????
 
Meya wa Manispaa ya Temeke Abdalah Mtinika anatuhumiwa Kushawishi viongozi wa Manispaa hiyo kuuza shule ya sekondari Kurasini kwa mwekezaji huku akitambua kuwa shule hiyo imepokea fedha zilizotolewa na Ras Samia Hassan ambapo tayari madarasa saba yamejengwa na yanatumika na wanafunzi.

Source: DarMpya

FLX7Q5kWUAAOdZ6.jpg
 
Meya na mauzo wapi na wapi? Msimamizi na mwajibikaji mkuu wa Mali za serikali katika halmashauri ni mkurugenzi. Kwa nini mkurugenzi alikuwa wapi?
 
Kumbe ndugai alikua mkweli maana tumeanza kuuzwa kidogo kidogo

Ngoja niandae safari ya Burundi maana haikwepeki.
 
Meya wa Manispaa ya Temeke Abdalah Mtinika anatuhumiwa Kushawishi viongozi wa Manispaa hiyo kuuza shule ya sekondari Kurasini kwa mwekezaji huku akitambua kuwa shule hiyo imepokea fedha zilizotolewa na Ras Samia Hassan ambapo tayari madarasa saba yamejengwa na yanatumika na wanafunzi.

Source: DarMpya

View attachment 2117085
Vuta mpunga Meya yanini ufe njaa wakati wengine wanakula kwa kuvuta kamba zao?
 
View attachment 2117016

Hii ndio Kashfa mpya inayozunguka kwenye Manispaa hiyo kwa sasa , ikiwa ni siku chache tangu kashfa ya Mwenyekiti wa ccm wa wilaya hiyo kutafuna zaidi ya sh. mil 300 za vikundi kuibuliwa...
Kama mwekezaji atajenga upya miundombinu ya shule sehemu nyingine na atalipa pesa Halmashauri na kuwekeza kitu chenye tija zaidi hakuna shida..

Hata Magereza au nyumba za Wananchi huwa wanahamishwa pale inapobidi..

Hapo kinauzwa kiwanja sio shule.
 
Back
Top Bottom