Hapana mkuu, hiyo inakuwa ni uamuzi wake binafsi baada ya kupata furaha na wala sio shinikizo kutoka upande wangu, wakati mwingine unakuta hata hamu sina na mashine yenyewe haijapandisha mafuta lakini mwenyewe anaijulia mpaka pampu inavuta mafuta juu gari inaondoka. Hapo inabidi nimtawanye tu.
Mkuu hakuna wa kuiiba pswd. Hata hivyo nashukuru kwa kunitia moyo.Mkuu grafani11 hebu mwambie aliyekuibia passwedi airudishe bana haya maneno makali sana aise
Hizo nazijua mkuu na unakuwa kama hutaki vile ila kwa kuwa wife anataka hapo mwanaume lazima ajipinde aise na siku kama hiyo ndo unaonyesha kwa nini uliitwa mnwanaume
Mkuu hakuna kitu kizuri kama kupata ushauri na ukawa ni ushauri wa maana na wa kutegemewaMkuu hakuna wa kuiiba pswd. Hata hivyo nashukuru kwa kunitia moyo.
Hahahahahahahahaaaaaaa Horsepower habari yako? Nisalimie wanajamii waliokaribu nawe hapo.
Vile vile ni vizuri pia tukajitahidi kusoma machapisho mbalimbali yenye mafundisho mazuri kuhusu ndoa na hata kuhudhuria semina mbalimbali zenye kujenga mahusiano. Wengi wetu mkuu bada ya ndoa hufikiri wamemaliza kumbe sivyo.Mkuu hakuna kitu kizuri kama kupata ushauri na ukawa ni ushauri wa maana na wa kutegemewa
Ndoa ni darasa ambalo kila siku kuna mapya yanajitokeza na hatuwezi kuiendesha ndoa in isolation bila kupata uzoefu na ushauri kutoka kwa wale ambao wapo tayari au wana ndoa au wana ujuzi zaidi yetu
Unapopewa ushauri vile vile uzingatie ni nani na ni kwa wakati gani unaweza kuutumia ushauri huo
Ndoa sio ya kwenda nayo kama msukule utajikuta umefikia mahali ambapo wanasema hakuna njia ya kupita yaani ushalikoroga na ndo maana unapopewa ushauri uombe pia hekima ya Mungu katika kujua je huu ushauri ni wa maana au unafaa kuchukuliwa
Mkuu mengi tunayaacha baada ya kuoanaVile vile ni vizuri pia tukajitahidi kusoma machapisho mbalimbali yenye mafundisho mazuri kuhusu ndoa na hata kuhudhuria semina mbalimbali zenye kujenga mahusiano. Wengi wetu mkuu bada ya ndoa hufikiri wamemaliza kumbe sivyo.
Mkuu tunabakia kusifia wakina Messi, Christian Ronaldo nawake zao tunasahau ya kwetu. Mwisho wa siku waifu akimpata mpaka rangi kucha anayejua kusifia mguu wa bia, mara macho mazuri wenzetu hawa hawakawii kulainika.Mkuu mengi tunayaacha baada ya kuoana
Outing zile zinakufa, zawadi ndo basi tena au kumpelekea wife maua kidogo ni shughuli
Kumsifia mke wako hata siku moja amevaa na kutokelezea zinaisha
Yaani wewe ni kukaa na marafiki kuangalia mechi unasahau kuwa una mke ambaye nae alipaswa awe na wewe sehem mnazungumzia maendeleo yenu na ya familia
Tunajisahau na ndo maana ndoa nyingi ni changa ila zinaonekana kama zina miaka mia
Mkuu tunabakia kusifia wakina Messi, Christian Ronaldo nawake zao tunasahau ya kwetu. Mwisho wa siku waifu akimpata mpaka rangi kucha anayejua kusifia mguu wa bia, mara macho mazuri wenzetu hawa hawakawii kulainika.
neno ahsante....naomba ....samahani ...na pole ni muhimu kweli kwenye ndoa.....mfano..
ahsante.....utakuta unampa mmeo/mkeo zawadi au umemfanyia jambo zuri la kumfurahisha....akitumia neno ahsante unaonyesha kuthamini kile kitu na hata unampa nguvu mmeo/mkeo kukufanyia jambo zuri tena siku nyingine...
samahani.....hapa unaonyesha umetambua kosa na unahitaji kusamehewa......na unahitaji mhusika alisamehe hilo jambo...
pole......unaonyesha kumjali mwenzako .
naomba....neno naomba linaonyesha heshima fulani..ukihitaji kitu kutoka kwa mwenza wako na ukatumia neno naomba linapendeza zaidi kuliko kusema nipe...niletee...bila ya kutanguliza neno naomba inakuwa haipendezi .
ni vizuri hayo maneno yakawa vinywani mwetu....
Umemaliza mkuu, labda jamii iangalie upya suala la kurudisha mafunzo ya jando na unyago. Maana siku hizi vijana wamekuwa na washauri wengi wanaoitwa mtandao, TV, filamu za wavaa nusu utupu nk. Wanayoyapata humo ndiyo haya tunayoyashuhudia sasa.Yaani kitu kidogo tuu wanaingia kwenye line bila hata kujua
Hayo ndio sumu kubwa kwenye ndoa mkuu na kweli majarida na semina za ndoa zinapaswa ziwe nyingi sana na huwa sometime naona kama viongozi wa dini wameacha kufanya kazi zao maana wakishawafungisha ndoa ndo hawarudi tena hata kuwapa somo na kuwauliza changamoto mnazozipata kwenye maisha ya ndoa
Kuna vitu vingi sana tunaacha kuvifanya vinavyohusu maisha ya ndoa mkuu yaani kuna mengi sana ambayo tunapwswa tufanye na haya mambo ya kusema sijui wife kafanya nini au ndoa inanishinda au sijui mke analalamika hafikishwi na mumewe au mume hampi mke haki yake yangekuwa historia
Umemaliza mkuu, labda jamii iangalie upya suala la kurudisha mafunzo ya jando na unyago. Maana siku hizi vijana wamekuwa na washauri wengi wanaoitwa mtandao, TV, filamu za wavaa nusu utupu nk. Wanayoyapata humo ndiyo haya tunayoyashuhudia sasa.
Maisha ya maigizo kulala maskini kuamka tajiri, kulala darasa la saba akiamka memaliza chuo kikuu na ajira mkononi. Subira hawataki.Mkuu hakuna kitu kibaya kwa wadada zetu hawa wanaoingia kwenye Ndoa wakitegemea ndoa zao na mapenzi yao yawe kama ya wale Wafilipino kwenye tamthilia zao hizo
Au wanategemea kukuta mambo ya akina Kanye West kwenye ndoa zao au ndoa za kwenye movie hizi ambazo mkuu hakuna kitu kama hicho
Sasa anapotafuta akutane na maisha ya wale wafilipino anakutana na maisha ya Masanja wa Usukumani mambo yanakuwa togfauti na ndio hao ambao hawaishi kulalamika ndoa ngumu bora nisingeolewa
Maisha ya maigizo kulala maskini kuamka tajiri, kulala darasa la saba akiamka memaliza chuo kikuu na ajira mkononi. Subira hawataki.
Ndiyo maana mapedeshee siku hizi wanajichagulia wanavyotaka, tena wengi wanajisifu huku mitaani kuwa hawataki kupita barabara ya lami ambayo hata maskini na kagari kake ka mkopo kasiko na 4WD anapita, wanataka barabara ya tope na mavumbi ambako watakuwa peke yao. Demu akikubaliana naye akitoa barabara ya tope siku ya pili anapelekwa yard kuchagua spacio.
Mkuu naona umeamua kupiga rungu upande mmoja tu leo, kama nawaona wanavyochekelea.Mkuu haya mambo tuyaache tuu
Na tukirudi nyuma hata sisi wanaume tuna makosa yetu ni vile tuu wanawake wanatuvumilia
Umepita pembeni huko ukapiga mpango wako wa kando umerudi home wife anataka haki yake unasingizia uchovu sijui ofisi ina madeni so una stress sijui leo boss kakufokea sana wakati siku nzima hujaonana na boss sijui leo tumbo linauma hijisikii vizuri
Siku akitoka nje unaanza kulalamika
Mkuu naona umeamua kupiga rungu upande mmoja tu leo, kama nawaona wanavyochekelea.
neno ahsante....naomba ....samahani ...na pole ni muhimu kweli kwenye ndoa.....mfano..
ahsante.....utakuta unampa mmeo/mkeo zawadi au umemfanyia jambo zuri la kumfurahisha....akitumia neno ahsante unaonyesha kuthamini kile kitu na hata unampa nguvu mmeo/mkeo kukufanyia jambo zuri tena siku nyingine...
samahani.....hapa unaonyesha umetambua kosa na unahitaji kusamehewa......na unahitaji mhusika alisamehe hilo jambo...
pole......unaonyesha kumjali mwenzako .
naomba....neno naomba linaonyesha heshima fulani..ukihitaji kitu kutoka kwa mwenza wako na ukatumia neno naomba linapendeza zaidi kuliko kusema nipe...niletee...bila ya kutanguliza neno naomba inakuwa haipendezi .
ni vizuri hayo maneno yakawa vinywani mwetu....
^^
Yanatumika sana katika uchumba,,yanachuja upesi ktk ndoa.
^^
Yap! True but kuna watu ni wagumu kuomba msamaha hata wanapokosea even kumsamehe mwenzie utachuniwa wiki nzima had jasho likutoke ndo utasamehewa! Ila kuomba omba msamaha kila wakati napo ni udhaifu mwingine!
Watu mada za kujenga kama hizi hawazitaki sijui kwanini?
Na kutumia sex kudai samahani?
is it fair?