The Royal Tour: Mchungaji Peter Msigwa wa CHADEMA ampongeza Rais Samia Suluhu Hassani kwa kazi nzuri

The Royal Tour: Mchungaji Peter Msigwa wa CHADEMA ampongeza Rais Samia Suluhu Hassani kwa kazi nzuri

Mchungaji Msigwa

Nipo katika rekodi nikikutetea kuhusu sakata la Ngorongoro. Nilisema una haki ya kutoa maoni kama Mtanzania na kiongozi uliyeongoza shughuli za chama chako Bungeni

Niliwashauri wanaotaka usiseme waache kwani demokrasia ina upana na gharama zake ikiwemo kuvumiliana kwa misimamo tofauti nikitoa mfano wa Democrats kule US na Conservatives UK

Kwa hili la Royal tour nipo katika rekodi nikisema ' kilichofanyika kina nia njema' tatizo linalowasumbua watu ni jinsi gani imefanyika. Nilipongeza mjadala wa mawazo tofauti

Leo Msigwa unaandika kwamba viongozi wenzako hawajui utalii. Una haki ya maoni lakini maoni hayo yana stara zake. Kutofautiana kimawazo hakufanyi wewe au wenye mitazamo tofauti wawe wajinga. Kwa hili unawakosea wenzako! Omba radhi

Pili, ukiandika na kusema huogopi kuitwa hata kabla ya tendo kutokea ni self defense.
Katika mazingira ya kawaida halifai, tumia uhuru wako hadi vinginevyo si kujenga 'uncertainty'

Picha unayoipaka kwa wenzako si nzuri na hulazimiki kujitetea pasipo na tuhuma! unahofia nini?

Tatu, mawasiliano kati yako na wenzako ni yenu si kila mawasiliano ni 'for the public consume'

Lakini kama unaona kuna mazingira usiyoyapenda kwanini usijiweke huru bila kusubiri kibali cha kutumia kinywa chako au kutumia kinywa chako kwa hofu!


Fundi Mchundo JokaKuu Pascal Mayalla

Siku hizi anatoa maoni tofauti na wenzake wa chama, kisha anasema haogopi kufukuzwa chama! Unajua maana yake ni nini, tayari anataka kwenda ccm ila anaona aibu kwenda moja kwa moja, hivyo anatengeneza mazingira ya kufukuzwa ili aonekane kafukuzwa. Cdm wakitaka kumpatia inabidi wasimfukuze bali wampotezee lazima ataondoka kwa aibu.
 
CHADEMA haiwezi kumfukuza, ni Chama cha Kidemokrasia na moja ya nguzo zake kuu ni uhuru wa kutoa maoni (bila kuathiri haki za msingi za wengine). Anajistukia tu, unless kama anautaka Uenyekiti.
Historia inawahukumu

Rejea kufukuzwa kwa Zitto
 
Mchungaji Msigwa

Nipo katika rekodi nikikutetea kuhusu sakata la Ngorongoro. Nilisema una haki ya kutoa maoni kama Mtanzania na kiongozi uliyeongoza shughuli za chama chako Bungeni

Niliwashauri wanaotaka usiseme waache kwani demokrasia ina upana na gharama zake ikiwemo kuvumiliana kwa misimamo tofauti nikitoa mfano wa Democrats kule US na Conservatives UK

Kwa hili la Royal tour nipo katika rekodi nikisema ' kilichofanyika kina nia njema' tatizo linalowasumbua watu ni jinsi gani imefanyika. Nilipongeza mjadala wa mawazo tofauti

Leo Msigwa unaandika kwamba viongozi wenzako hawajui utalii. Una haki ya maoni lakini maoni hayo yana stara zake. Kutofautiana kimawazo hakufanyi wewe au wenye mitazamo tofauti wawe wajinga. Kwa hili unawakosea wenzako! Omba radhi

Pili, ukiandika na kusema huogopi kuitwa hata kabla ya tendo kutokea ni self defense.
Katika mazingira ya kawaida halifai, tumia uhuru wako hadi vinginevyo si kujenga 'uncertainty'

Picha unayoipaka kwa wenzako si nzuri na hulazimiki kujitetea pasipo na tuhuma! unahofia nini?

Tatu, mawasiliano kati yako na wenzako ni yenu si kila mawasiliano ni 'for the public consume'

Lakini kama unaona kuna mazingira usiyoyapenda kwanini usijiweke huru bila kusubiri kibali cha kutumia kinywa chako au kutumia kinywa chako kwa hofu!


Fundi Mchundo JokaKuu Pascal Mayalla

..Naamini kuna mchangiaji amepotosha maelezo ya Peter Msigwa, mahojiano kamili yako hapa chini.

..Na hakuna mahali amezungumzia kumpigia simu Tundu Lissu.

..infact amesema anakubaliana namna Lissu anavyotoa challenge ya kutaka taarifa zaidi kuhusu Royal Tour.

..Msigwa pia ameeleza kwamba anakubaliana na baadhi ya hoja za Lema kuhusu approach iliyotakiwa kuchukuliwa kuitangaza nchi.

..amefafanua kwa kirefu kwamba anapingana na wale ambao wametoa hukumu kwamba kuna ufisadi, amesema yeye bado hajauona.

..sasa mtu aliyetoa maelezo hayo ataitwa vipi kwenye "kamati ya maadili"? mimi sijawahi kusikia Chadema wana kamati ya maadili, mara nyingi wanachama wao husulubiwa ktk Kamati Kuu.

 
..Naamini kuna mchangiaji amepotosha maelezo ya Peter Msigwa, mahojiano kamili yako hapa chini.

..Na hakuna mahali amezungumzia kumpigia simu Tundu Lissu.

..infact amesema anakubaliana namna Lissu anavyotoa challenge ya kutaka taarifa zaidi kuhusu Royal Tour.

..Msigwa pia ameeleza kwamba anakubaliana na baadhi ya hoja za Lema kuhusu approach iliyotakiwa kuchukuliwa kuitangaza nchi.

..amefafanua kwa kirefu kwamba anapingana na wale ambao wametoa hukumu kwamba kuna ufisadi, amesema yeye bado hajauona.

..sasa mtu aliyetoa maelezo hayo ataitwa vipi kwenye "kamati ya maadili"? mimi sijawahi kusikia Chadema wana kamati ya maadili, mara nyingi wanachama wao husulubiwa ktk Kamati Kuu.
Ahsante Mkuu

Nilisoma maoni huko tweeter halafu nikaona hapa JF
Nadhani angejitokeza au ange tweet kukanusha
 
Aliyekuwa mbunge wa Iringa mjini kupitia CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa amempongeza Rais Samia Suluhu Hassani kwa kazi uzuri na ubunifu wa Filamu maarufu ya kitalii ya THE ROYAL TOUR.

Kiongozi huyo wa CHADEMA wa nyanda za juu kusini amesema kuwa inawezekana labda kuna mapungufu madogomadogo lakini kimsingi kazi aliyoifanya Rais Samia Suluhu Hassani ni ya KIZALENDO na inahitaji kuungwa mkono na watanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa kwa kuwa hata yeye mara kadhaa akiwa bungeni mara kadhaa ameshauri kutumika kwa nguvu ya ziada kuitangaza Tanzania na vivutio vya utalii.

Filamu ya The ROYAL TOUR ni filamu ya kihistoria inayoelezea kuhusu vivutio mbalimbali vya utalii vya Tanzania ambayo iliandaliwa na muandaaji Maarufu wa filamu PETER JOHN GREENBERG kutoka nchini Marekani.

Filamu hiyo mpaka sasa imezinduliwa ktk majiji makubwa matatu.. Jiji la LOS ANGELS na NEW YORK USA, Pamoja na jiji la kitalii ARUSHA, TANZANIA.

Filamu hiyo maarufu ya kitalii inatarajiwa kuzinduliwa ktk mji wa kihistoria wa Zanzibar na jiji kubwa la kibiashara DAR ES SALAAM.

ROYAL TOUR inatarajiwa kuleta matokeo makubwa ktk sekta ya utalii nchini Tanzania na kuongeza mapato yatokanayo na utalii.

Filamu ya The Royal Tour inapatikana ktk mtandao maarufu wa amazon.com na inatarajiwa kuoneshwa ktk vituo lukuki vya television duniani.

Hongera Mchungaji Peter Msigwa kwa kuweza kuchuja pumba na mchele na kutambua kuwa kuna tofauti kati ya itikadi za kisiasa linapokuja suala la ujenzi wa nchi yetu japo tegemea kushambuliwa na wafuasi mbalimbali wa upinzani kwa kuwa sera za chama chako haziamini ktk kupongeza jambo zuri linapofanywa na serikali lakini umeonesha ukomavu wa kisiasa...

MAMA SAMIA IMARA; KAZI IENDELEE👋🇹🇿
View attachment 2204628

View attachment 2204835

View attachment 2204836

View attachment 2204837

View attachment 2204838
Jambo jema but pengine hakukuwa na ulazima wa kuigiza yeye✍️
 
Nimemsikiliza Msigwa na naona ni kama amewekewa maneno. Ila kuna umuhimu wa yeye kuwa muwazi na kuya own yale maneno au kuyakataa.

Tofauti na ilivyokuwa kwenye suala la Ngorongoro, kwenye hili sikubaliani nae. Naona amekosea kwa kuwataka wenzake wote waikubali hii Royal Tour. Kwa kufanya hivyo anakuwa anawafunga mdomo. Kwa vile sidhani kama yeye atakubali kufungwa mdomo basi awaachie wenzake waseme. Cha kudai ni sababu zao za kupinga Royal Tour.

Mimi sikubaliani na tour kwa sababu zifuatazo:
1. Value for money. Sidhani kama hii ni the most cost effective way ya kuwavuta watalii. Haya mambo ya matangazo kwenye TV yamepitwa na wakati. Siku hizi social media ni much more effective. Tweet moja ya influencer katika social media itaangaliwa na mamilioni zaidi ya watakaokodisha documentary Amazon. Kuliko PBS bora wangewaomba wakina Netflix, HBO, Disney n.k. watayarishe contents ambazo watazistream kwenye app zao. Kukodisha bango Time Square na kumweka Ronaldo au Messi itakuwa ni kutupa hela chooni maana hawana huo mvuto Marekani.
2. Gharama za launching nazo hazi make sense. Hivi kweli the only "celebrity" waliyeweza kupata ni baba ya Rihanna? Kwa nini hawakumbembeleza Lupita Nyong'o? Au Daniel Kazuya? Hatuwataki kwa sababu ni wakenya na waganda? Hii inanipeleka kwenye point yangu ya 3.
3. Hii ngoma ya kusema kuwa watu wanadhani Mlima Kilimanjaro uko Kenya imepitwa na wakati. Tunatakiwa tuanze kushirikiana katika kutangaza nchi zetu. Kuna ubaya gani kuuza Afrika Mashariki kwa ujumla wake? Hivi mtu akija na Kenya Airways, akashukia Nairobi halafu akaja Tanzania kupanda mlima Kilimanjaro tuna hasara gani? Tunaweza kutumia nyota ya Lupita na Daniel kuwavuta watu waje Afrika Mashariki na sisi tutafaidika maana kila nchi ina uvutio wake.
4. Tumeifanya hii Tour kama magic bullet ambayo itatuondolea matatizo yote badala ya kuangalia kwa dhati kwa nini watalii hawaji Tanzania ( sio kwa sababu ya Kenya). Huduma zetu zikoje? Je mazingira yetu ni rafiki kwa watalii ( nilizungumzia unyanyasaji tunaowafanyia wakitaka kupiga picha n.k.). Je tuna hoteli na makampuni ya kitalii ambayo yana global impact? Haya mahoteli na makampuni yanaweza kututangaza kuliko tunavyojitangaza wenyewe.
5. Usalama ukoje nchini mwetu? Tusidharau haya mambo ya panya road maana travel advisory moja ya State Department kuhusu hali ya usalama nchini inafuta faida zote za Royal Tour. Jawabu sio kuwalaamu kwa kutoa hizo taarifa bali ni kuhakikisha hao panya road wanabadilisha ajira.
6. Tunahitaji kupanua wigo wa utalii wetu. Tanzania ni zaidi ya Kilimanjaro na Ngorongoro. Kuna watu wanavutiwa zaidi na miji, na historia, na fukwe, na maisha ya watu wa kawaida, na masuala ya mazingira n.k. Tuangalie namna ya kuwarahisishia wao kutimiza ndoto zao. Sio mtu anakuja ili akae na wenyeji halafu tunamtaka anunue special visa ya bei mbaya! Au wanafunzi wanatembelea shule vijijini lakini immigration wanawasumbua ili wapate dawa za viatu.
7. Tuangalie kama ada zetu ni competitive. Tunaweka ada za kuua mtu kuingia kwenye mbuga zetu. Tuwatambue diaspora kama wenzetu ili wawe encouraged kuja na family na rafiki zao kutembelea mbuga zetu.
8. Tuwe wabunifu. Ghana walianzisha Year of Return ili kuwavuta African Americans kwenda kutalii Ghana na hata kuwekeza. Waliwapa masharti nafuu sana kama ndugu zao waliopotea. Kwa nini na sisi tusifanye hivyo? Tuwa target African Americans kuja kujifunza historia.
9. Tuachane na rhetoric za kijinga kama hizi za mashoga. Mashoga wapo na hata tupige kelele vipi haibadilishi ukweli huo. Wao pia ni binadamu kama sisi. State Department ikisema tu kuwa maisha yao yako hatarini wakiwa Tanzania, hawatakuja wao na sympathisers wao. Katika dunia ya leo impact ya kutokuja kwao tutaipata.
10. Tujiulize kwa nini mashirika ya ndege ya kimataifa kama British Airways, Lufthansa n.k. yaliacha kuja Tanzania. Dawa sio kununua ndege zetu.

Zoezi la kuuza Tanzania ni endelevu. Kwa hiyo badala ya kutumia mapesa kibao kwenye tour tungewekeza kwenye vitu ambavyo vitakuwa na impact kwenye maisha ya watu wetu ili wasione kukaba watalii ni dili.

Amandla...

Cc. JokaKuu Nguruvi3
 
Kama hii ni kweli Mchungaji yuko njiani kuondoka Chadema. Sio kwa sababu ametofautiana nao bali kwa kuingiza majina ya wakina Lissu, kuanza kuzungumzia kuitwa kwenye kamati ya maadili na kufukuzwa uanachama. Hii ni dalili ya mtu kutafuta kufukuzwa ili aonekane shahidi. Nadhani Chadema hawatamjibu, kitu ambacho kitazidi kumkasirisha na kumfanya azidi kutoa matamshi ya kujionyesha kuwa yeye ni tofauti na chama chake. Hafukuzwi ila uchaguzi ujao watamSumaye.

Amandla...
"Wata msumaye" bado nacheeeka
 
Aliyekuwa mbunge wa Iringa mjini kupitia CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa amempongeza Rais Samia Suluhu Hassani kwa kazi uzuri na ubunifu wa Filamu maarufu ya kitalii ya THE ROYAL TOUR.

Kiongozi huyo wa CHADEMA wa nyanda za juu kusini amesema kuwa inawezekana labda kuna mapungufu madogomadogo lakini kimsingi kazi aliyoifanya Rais Samia Suluhu Hassani ni ya KIZALENDO na inahitaji kuungwa mkono na watanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa kwa kuwa hata yeye mara kadhaa akiwa bungeni mara kadhaa ameshauri kutumika kwa nguvu ya ziada kuitangaza Tanzania na vivutio vya utalii.

Filamu ya The ROYAL TOUR ni filamu ya kihistoria inayoelezea kuhusu vivutio mbalimbali vya utalii vya Tanzania ambayo iliandaliwa na muandaaji Maarufu wa filamu PETER JOHN GREENBERG kutoka nchini Marekani.

Filamu hiyo mpaka sasa imezinduliwa ktk majiji makubwa matatu.. Jiji la LOS ANGELS na NEW YORK USA, Pamoja na jiji la kitalii ARUSHA, TANZANIA.

Filamu hiyo maarufu ya kitalii inatarajiwa kuzinduliwa ktk mji wa kihistoria wa Zanzibar na jiji kubwa la kibiashara DAR ES SALAAM.

ROYAL TOUR inatarajiwa kuleta matokeo makubwa ktk sekta ya utalii nchini Tanzania na kuongeza mapato yatokanayo na utalii.

Filamu ya The Royal Tour inapatikana ktk mtandao maarufu wa amazon.com na inatarajiwa kuoneshwa ktk vituo lukuki vya television duniani.

Hongera Mchungaji Peter Msigwa kwa kuweza kuchuja pumba na mchele na kutambua kuwa kuna tofauti kati ya itikadi za kisiasa linapokuja suala la ujenzi wa nchi yetu japo tegemea kushambuliwa na wafuasi mbalimbali wa upinzani kwa kuwa sera za chama chako haziamini ktk kupongeza jambo zuri linapofanywa na serikali lakini umeonesha ukomavu wa kisiasa...

MAMA SAMIA IMARA; KAZI IENDELEE👋🇹🇿
View attachment 2204628

View attachment 2204835

View attachment 2204836

View attachment 2204837

View attachment 2204838
 
SSH hafanyi biashara haramu ya kununua chadema ,afanye hivyo Ili imsaidie nini?

Ujue nyie Chadomo ni hamnazo kichwani kwenu, endeleeni kupinga tuone mwisho wenu.
Kwani jiwe alikuwa anafanya biashara hiyo? Si mlisema waliounga mkono juhudi wanamkubali uchapakazi wake?
 
..Naamini kuna mchangiaji amepotosha maelezo ya Peter Msigwa, mahojiano kamili yako hapa chini.

..Na hakuna mahali amezungumzia kumpigia simu Tundu Lissu.

..infact amesema anakubaliana namna Lissu anavyotoa challenge ya kutaka taarifa zaidi kuhusu Royal Tour.

..Msigwa pia ameeleza kwamba anakubaliana na baadhi ya hoja za Lema kuhusu approach iliyotakiwa kuchukuliwa kuitangaza nchi.

..amefafanua kwa kirefu kwamba anapingana na wale ambao wametoa hukumu kwamba kuna ufisadi, amesema yeye bado hajauona.

..sasa mtu aliyetoa maelezo hayo ataitwa vipi kwenye "kamati ya maadili"? mimi sijawahi kusikia Chadema wana kamati ya maadili, mara nyingi wanachama wao husulubiwa ktk Kamati Kuu.


Mama anaupiga mwingi

Mch Msigwa ameona siasa za kupinga kila kitu ni za kizamani hazijengi
 
Back
Top Bottom