This is Africa: Rais wa Nigeria yabainika alitumia cheti cha mwanamke kudanganya ni degree yake. Je, atawajibika kwa kuidanganya nchi anayoiongoza?

This is Africa: Rais wa Nigeria yabainika alitumia cheti cha mwanamke kudanganya ni degree yake. Je, atawajibika kwa kuidanganya nchi anayoiongoza?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
images (2).jpeg

Degree yake ya kwenye CV inayoonyesha kasomea chuo kikuu cha Chicago nchini Marekani ilizua maswali, wananchi wakatuma maombi Marekani kutaka kujiridhisha elimu ya Rais wao.

Wamarekani wapo Direct, siku ya jana Jaji wa Marekani aliamuru taarifa za uhalali wa cheti zitolewe leo na imebainika kwamba ni kweli alisoma hapo lakini alitumia cheti cha Mwanamke kutuma maombi ya kujiunga.

Ni sawa na huku kwetu mtu kafeli form 6, atumie cheti cha mtu wanaefanana jina kutuma maombi ya kujiunga chuoni.

Siku ya jana baada ya jaji wa Marekani kutoa agizo la kuweka mambo wazi, nae Rais wa Nigeria akatoa agizo la kuongeza mishahara.

Baada ya kupata ushahidi usio na shaka kwamba kakiuka kanuni za integrity (uaminifu), je kutakuwa na accountability (uwajibikaji)?

JE ATAWAJIBIKA?
 
View attachment 2770078


Degree yake ya kwenye cv inayoonyesha kasomea chuo kikuu cha Chicago nchini Marekani ilizua maswali, wananchi wakatuma maombi Marekani kutaka kujiridhisha elimu ya Rais wao...
Liraisi ni libashite kabisa.

Sasa lingesema halikusoma kama wanalipenda bado wangelipa nchi tu ila sio kuwadanganya watu
 
Marehemu mwenyewe elimu yake ilikua magumashi!!

Aliepo nae pitia elimu yake uone makambarisi.

Faster akatunukiwa PhD ili aonekane kipanga kwa wananchi wasioelewa!!

Yale yale ya Mkwere na gentleman pass ya GPA ya 2.
Akaenda uturuki akapewa PhD ya jukwaani!!
 
Je atawajibika? 😅😅

Never! Bado tupo mbali sana!
 
Marehemu mwenyewe elimu yake ilikua magumashi!!

Aliepo nae pitia elimu yake uone makambarisi.

Faster akatunukiwa PhD ili aonekane kipanga kwa wananchi wasioelewa!!

Yale yale ya Mkwere na gentleman pass ya GPA ya 2.
Akaenda uturuki akapewa PhD ya jukwaani!!
Ukweli kama utani. Mkuu unajua alipo Ben Saa8?
 
Yale yale ya Mkwere na gentleman pass ya GPA ya 2
Naomba unipe uhusiano wa G.P.A kubwa na akili ya mtu. Namaanisha hivi ukipata G.P.A kubwa ndiyo unakuwa na akili zaidi??

Unafahamu first class ngapi zimewahi kuongoza nafasi za juu hapa nchini? Namaanisha first class kutoka Havard, University of Oxford, Yale university n.k siyo UDSM.

Yaleyale, ukipata division one basi lazima uwe na maisha mazuri! Ukimkuta aliyepata division four amekupita kimaisha mnaanza kujaa wivu,chuki,husuda,hasira,roho mbaya ,kijiba cha roho n.k!

Acha kukariri, mtaa hautaki kukariri!
 
Back
Top Bottom