TANZIA Thomas Mashali afariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

TANZIA Thomas Mashali afariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

Maisha unayoishi kwenye hii dunia yanatabiri hata kifo chako kitakavyokuwa.
 
View attachment 426997 View attachment 426990
Thomas Mashali,bondia mashahuri wa Tanzania amefariki usiku wa leo baada ya kupigwa mapanga maeneo ya Kimara.Inasemwa kuwa Mashali alikuwa kambini akijiandaa na pambano,lkn alitoka kambini na jamaa zake na kwenda kunywa moja moto na moja baridi.

Baada ya kupata kilaji,Mashali alihama Bar moja na kwenda nyingine,ambapo wanasema akilewa huwa anakuwa na fujo.Sasa aliingia Bar nyingine akaanza kuleta ubabe wa kupiga watu.Raia wakamuitia mwizi,watu wakaja na mapanga na marungu wakampiga mpaka kufa.Walipokuja kugundua ni Mashali,ilikuwa ameshauwawa na kupoteza damu nyingi.

Madereva wa bodaboda wakamchukua na kumpeleka Muhimbili.Mpaka sasa mabondia wanakusanyika Muhimbili kwa ajili ya utaratibu wa mazishi.

Kwa Heri Bondia Thomas Mashali.

Mleta mada ongezea hii kama imeshakuwa confirmed, maana inaeleza vizuri tukio lilivyokuwa.
 
Mm simfahamu kihivyo ila alikuwa anapenda sana kuja Meridian bar na alikuwa anakaa hadi usiku mnene sikuwahi ona anazinguana na mtu yyte
Pamoja na tofauti zote tulizo nazo binaadam, lakini wote tuna common behaviours kama kuchangamana, huzuni, furaha, uchovu n.k hivyo yoyote kati ya tabia hizo au zote kwa pamoja haimuondolei mtu tabia zake.
 
Alikuwa ni jamaa fulani anayeishi maisha ya uswahili japo jina lake ni kubwa sana.
images

MASHALI2.jpg
Nadhani nitalazimika kuanza Program ya kusaidia hawa vijana wa aina hii na timu yetu ya taifa ya soka ili wawe washindi badala ya kuishia waishiapo.
 
Huu mchezo unaweza kumkuta yeyote, muda wowote, inabidi ukomeshwe haraka. Upiversity unatoka na manzi anayemtaka, anakuitia tu mob wanakutanguliza mbele ya enzi.

R.I.P Mashari/Mashali.
...hahahahaha..arifu sie marasta tunakula mmea,hatuli nyama wala mamanzi!
..on a serious note,kweli huu 'mchezo' inatakiwa ukomeshwe;maana kirahi rahisi sana unaweza kuuwawa!
 
Waliua watafiti wakisema ni wanyonya damu, Leo wameua bondia wanasema ni mwizi.. Duh hili liangaliwe kwa jicho la tatu. Mashali alikuwa ni Icon ya nchi. Very sad. R.I.P Kamanda.
 
Zimeripotiwa taarifa kusikitisha kuhusu kifo cha
bondia maarufu nchini wa ngumi za kulipwa Thomas Mashali kulichotokea usiku wa kuamkia leo. Inasemekana bondia Thomas Mashali amepoteza uhai baada ya kupigwa sana na watu wasiojulikana
maeneo ya Kimara baada ya kupigiwa kelele za
mwizi na watu ambao alijikuta akigombana nao
baada ya kulewa.
 
Waliua watafiti wakisema ni wanyonya damu, Leo wameua bondia wanasema ni mwizi.. Duh hili liangaliwe kwa jicho la tatu. Mashali alikuwa ni Icon ya nchi. Very sad. R.I.P Kamanda.
Icon ukiingia kwenye anga zake lzm uite maji maa


.R I P
 
Icon ukiingia kwenye anga zake lzm uite maji maa


.R I P
Haitoi uhalali wa kujichukulia sheria mkononi. Mpaka mauti yanamkuta kuna ushahidi wowote kuwa kweli alimuibia huyo aliyemuita mwizi.
 
Clauds wametangaza aliitiwa mwizi baada ya kutokea ugomvi Baa Na rafiki yake.

Hivyo wananchi wenye hasira wakamshambulia Na mapanga baadae watu wa bodaboda wanaomfahamu wakamkimbiza Mhimbili ambako mauti yalimkuta.

R.I.P.
Akiwa mtu mmoja wanajifanya wanahasira lakn kikiwa kikundi cha vijana watano wakiwa na mapanga wanatafuta pa kutokea ..

Kama wanajifanya wanahasira mbona panya road wamewashinda? Wanaume Wa dar wanatabia za kike kweli
 
Aisee! Sijui ni lini tutajifunza kuheshimu Uhai, watu wakisikia kelele za mwizi kitu cha kwanza wanachofikiria ni kuua!!

Hii itabia ifike kipindi ikome, watu wengi wanauwawa pasipo hatia!

R.I.P Mashali
 
Ila sio habari ya sasa hivi maana toka asubuhi ipo humu JF, ahsante kwa taarifa STUNTER leo umetupumzisha wanawake! hahahahah
 
Back
Top Bottom