TISS, PSU Jifunzeni kwa walioendelea

TISS, PSU Jifunzeni kwa walioendelea

Muangalie Biden akiwa Ikulu anavyomingo na raia bila wanajeshi au walinzi wa kumfuatafuta karibu. Hata anapokuwa nje ya Ikulu huwezi kuona mwanajeshi nyuma yake. Ni hivyo kwa viongozi wengi wa magharibi.
Tunaweza kuwaambia huko nje watufundishe na sisi Waafrika.
Kumbuka yule siyo Rais ni Makamo wa Rais.Halafu kila Jamii Ila Mfumo wake wa Ulinzi usilazimishe Rusia ifanane na USA. Hata aina ya Bunduki.

Kumbuka huyo hajaenda hutubia Wananchi kaenda hutubia Viongozi. Halafu kumbuka Ulinzi ni Elimu inafundishwa kulingana na Mazingira . Africa siyo America
 
Msafara mrefu inamaanisha watu wengi zaidi wanapata ulaji wa posho humo, marafiki na washikaji zao.
Rais, Makamu wanapita kwa spidi sana na wanatuelekezea bunduki upande wetu.
Kwenye ziara unakuta kuna magari zaidi ya 50
Unajiuliza hii vipi kumbe ni watu wanataka lipana posho
 
Yaani Mkurugenzi wa usalama wa taifa ambaye ni mtaalamu mwenye elimu ya mambo ya usalama pamoja na Mh. Rais wasilijue hilo ulijue wewe usiye na elimu mambo hayo haiwezekani.
Tatizo letu kuwa fanya kama maroboti au Malaika kumbe awajuhi chochote

Wangejua wangekaa kimya?
 
Mswahili fahari yake ni kumtisha mwezake. Mswahili anafarijika sana akiona mswahili mwenzake anapata hofu na kukosa amani kwa ajili yake
Yaani naona hilo ndo lengo lao.
PSU wanafukuza watu hata wasiangalie kinachoendelea.
Nchi nyingine wananchi wanamchungulia Rais wao sababu wamejipanga
 
Hata bango la kuonyesha ofisi ya TISS ilipo sidhani kama lipo, raia wamebaki wanabuni tu ofisi yao ilipo, mambo gizani kikomunisti zaidi[emoji16]
Ofisi zote za mashirika ya kijasusi yanajulikana
Ukienda mitandaoni unapata hadi tovuti yao

Wako twitter

Sisi sijui twajificha sababu gani?

Kuna siku niliongelea usiri katika ajira zao

Wenzetu walioendelea ili kuongeza uwajibikaji wameamua kuweka wazi ajira zao
 
Huu utaratibu wa mabunduki nafikiri ulianza au kukomaa zaidi awamu ya tano. Nikiangalia video za Mwalimu sioni mabunduki mengi.
Rais, Makamu wanapita kwa spidi sana na wanatuelekezea bunduki upande wetu.
Kwenye ziara unakuta kuna magari zaidi ya 50
Unajiuliza hii vipi kumbe ni watu wanataka lipana posho
 
Jana kaja Kamala wote tumeshuhudia Ulinzi imara usio na maonesho. Maonesho yenu ya kubeba mibunduki hadharani hayajaonekana jana. Siku zingine mnazingira Rais kama ni gaidi.

Hata yule mpambe anayevaa magwanda sioni umuhimu wake zaidi ya matumizimabaya ya kodi. Vile vidada vinavyokaa pembeni ya Rais akiwa anahutubia jana havijaonekana popote pale.

Jifunzeni bana
Mmekariri sana

Nendeni pale Hyatt Regency muone gari zinavyosachiwa haijalishi ni ya wapi, hawana cha yule ni mwenzetu, ukifika pale unasachiwa na MBWA afu waruhusiwa pita.

TISS ivunjwe maana imeshindwa msaidia Rais kazi
TISS ibaki kwenye kazi zake za msingi hasa Ukusanyaji wa Taarifa kupelekea walaji.

Presidential Security Unit itolewe TISS irudishwe Polisi Tanzania kama ilivyokuwa hapo awali.

ADC kukaa nyuma ya Rais wakati wote haina haja mpeni nafasi Kiongozi awe huru.

Mabunduki yale yaonekane maeneo hatarishi tu siyo kila mahali.
 
Huu utaratibu wa mabunduki nafikiri ulianza au kukomaa zaidi awamu ya tano. Nikiangalia video za Mwalimu sioni mabunduki mengi.
Waimarishe ulinzi kwa kutumia mifumo, watu bora

Jana nilikuwa naangalia Ziara ya Kamala

Aliagwa pale Airport walinzi waliendelea baki hadi ndege inapaa

Ndege nyingine nayo wakaisimamia ikaondoka

Walinzi wengine wakarudi na gari za kukodi

Nadhani wao ndo wataondoka wakimaliza kusanya masalia ya vitu vyao
 
TISS ibaki kwenye kazi zake za msingi hasa Ukusanyaji wa Taarifa kupelekea walaji.

Presidential Security Unit itolewe TISS irudishwe Polisi Tanzania kama ilivyokuwa hapo awali.

ADC kukaa nyuma ya Rais wakati wote haina haja mpeni nafasi Kiongozi awe huru.

Mabunduki yale yaonekane maeneo hatarishi tu siyo kila mahali.
Ipo siku yale mabunduki yatatumika against yeye, mtu anaweza toka huko na mastress yake akaamua weka rekodi yake.

Sheria ya muundo wa TISS yatakiwa irudiwe upya tuko 2023
 
Wote ni mashahidi wale mabaka mabaka, wale wadada wanaokaa pande mbili za Rais hawakuwepo jana nyuma ya Rais

Tujaribu kujifunza wao wanawezaje kumlinda Rais wao bila kukera watu, sasa TV inakuwa unaangalia hata watu wasiohusika wakati anayetakiwa onekana ni Rais pekee.
Wenzetu Kenya,Rwanda hili wanawezaje na sisi ugumu uko wapi?
 
TISS wengi walitajirika kipindi cha Jiwe, mtindo ulikuwa ni extortion kwa wafanyabiashara na wahindi. Kila mja aliogopa alipokuwa akitishiwa kupachikwa kesi za uhujumu uchumi au utakatishaji fedha. Kwa sasa hawana nguvu hizo.
Ni wale wenye vyeo anuwai ila hawa ambao ni changanyikeni tuko nao mtaani wanaomba mikopo na kuhitaji ukaribu kwa aliyenacho kwa minajiri ya nitakulinda boss .
 
Kumbuka yule siyo Rais ni Makamo wa Rais.Halafu kila Jamii Ila Mfumo wake wa Ulinzi usilazimishe Rusia ifanane na USA. Hata aina ya Bunduki.

Kumbuka huyo hajaenda hutubia Wananchi kaenda hutubia Viongozi. Halafu kumbuka Ulinzi ni Elimu inafundishwa kulingana na Mazingira . Africa siyo America
Huna unachokijua.
 
Juzi hapa FSB wamekamata watu kwa tuhuma za uhujumu wa nchi.
TISS wao haijulikana wanafanya kazi gani
Wapo wapo tu.

Wakivaa yale mabunduki wanajiona watu mno
Mkuu kazi za TISS ni kukamata watuhumiwa?
 
Heshimu Taasisi na Utaratibu wa Taasisi sawa? Siyo lazima kila lifanywalo na CIA / NSA (Marekani ) basi na TISS ( Tanzania ) nao walifanye au waliige.

Binafsi ( GENTAMYCINE ) nimebahatika Kukaa ( kuwa karibu ) na Walinzi wa baadhi ya Marais wa Ukanda wetu huu ( Kale Kayihura aliyekuwa CIG: wa Uganda ila kabla alikuwa Mlmoja wa Walinzi PPU wa Rais Museveni na Marehemu Noble Mayombo aliyekuwa CMI wa Uganda na aliyewahi pia kuwa ADC wa Rais Museveni ) achilia mbali wa Rais Kagame na wa Hayati Mzee Kabila ( Laureant Kabila ) na Sifa pekee niliyoisikia kutoka Kwao kuhusu TISS na hasa hasa PSU ni kwamba wako vizuri na Wameiva mno Kimedani.

PSU ndiyo blueprint ya Vikosi vingi vya Ulinzi wa Marais katika nchi nyingi za Ukanda huu ikiwemo na Msumbiji na nyinginezo.

Acheni Kudharau vya Kwenu TZ Oky?
Genta, Mfumo umekukubali 😂😂
 
Ofisi zote za mashirika ya kijasusi yanajulikana
Ukienda mitandaoni unapata hadi tovuti yao

Wako twitter

Sisi sijui twajificha sababu gani?

Kuna siku niliongelea usiri katika ajira zao

Wenzetu walioendelea ili kuongeza uwajibikaji wameamua kuweka wazi ajira zao
Tukiwaita “wasiojulikana” itakuwa kosa?
 
Ipo siku yale mabunduki yatatumika against yeye, mtu anaweza toka huko na mastress yake akaamua weka rekodi yake.

Sheria ya muundo wa TISS yatakiwa irudiwe upya tuko 2023
Hili nimewahi kuliwaza pia linaweza kutokea,FFU mmoja akavurugwa chuma ikafyatuka usawa wa mtu ni hatari,wale wanatakiwa wawepo ila warespond tu linapotokea jambo,ndivyo na wenzetu hufanya hivyo.
 
Waimarishe ulinzi kwa kutumia mifumo, watu bora

Jana nilikuwa naangalia Ziara ya Kamala

Aliagwa pale Airport walinzi waliendelea baki hadi ndege inapaa

Ndege nyingine nayo wakaisimamia ikaondoka

Walinzi wengine wakarudi na gari za kukodi

Nadhani wao ndo wataondoka wakimaliza kusanya masalia ya vitu vyao
Kuna mengi ya kujifunza kutokana na tukio la jana..kwanza ile level ya umakini ni kubwa mno.
 
TISS wasifuatile ushoga, usagaji au ukahaba.
Hayo labda yafuatiliwe na wenyeviti wa mitaa na vijiji kama mnaona ni muhimu sana.
Yani Kimsingi hawa jamaa wa TISS nawashangaa kweli unajua kuna kipindi nawaambia naowajua huko tukiwa kijiweni wajaribu kuwa wamechangamka badala ya kuzubaa kama wameachwa na treni imagine TISS wanaojiita watu wenye siri wanashindwa tu kujua sehemu na maeneo zinapofanywa biashara za usagaji na ushoga, au wauza unga? Na wakati zinajulikana kibao hapa Dsm wao utasikia wanapambana na Upinzani. Tiss wanashindwa kufaham watu wanaohujum Taifa leo hii kama hau waliopita na hela za ununuzi wa ndege.TISS wanaoishi kwa kujionesha na kutamba kwa watu sehem za starehe licha ya kuwa hao ni Taasis nyeti?
 
Back
Top Bottom