Top 3 GOAT Tanzania Rappers, Serikali itambue mchango wao ikibidi watunukiwe Phd

Top 3 GOAT Tanzania Rappers, Serikali itambue mchango wao ikibidi watunukiwe Phd

Ninakupinga hapo kwenye namba 2 na 3 kwa sababu zifuatazo
Kwanza prof J sio msanii wa kumuweka kwenye kundi moja na rappers, aina ya muziki aliokuwa anafanya ni kama mchanganyiko, sometimes anaimba kawaida sana mada mchanganyiko mfano Siasa, mapenzi n.k reffer album zake zote,machozi na damu,mapinduzi,J.O.S.E.P.H n.k ni msanii asiyezingatia misingi ya uandishi wa Rap zaidi bali content na flow.

Nikki Mbishi ni good rapper kiujumla ila kwa ubora sioni akimfikia hata Songa maana hana content na utulivu
1. Nitajie wimbo wa Prof. Jay ambao anaimba.

2. Je, unajua kwamba kurap si lazima uwe unarap kama Fid Q, bali kuna delivery styles tofauti.?
 
1. Nitajie wimbo wa Prof. Jay ambao anaimba.

2. Je, unajua kwamba kurap si lazima uwe unarap kama Fid Q, bali kuna delivery styles tofauti.?
Ni sahihi kumuita prof Jay Mwanahiphop/bongofleva bora, Ila si sawa kumuita rapper bora. Mfano nyimbo kama zali la mentali,kamili gado,starehe,nikusaidieje n.k unaweza kunipa 'mstari kwenzi' hata mmoja hapo? Ni nyimbo za hiphop/bongo fleva za kawaida sana sio pure rap.
 
Itanibidi nikafanye sala ya toba kwa kusoma uzi uliojaa kufuru dhidi ya wakali wa muda wote wa Tanzanian Hiphop.
 
Kama kwenye list umemuweka Songa na young killer ila hakuna chindo,fazza Nelly, Hashim dogo .Jay Mo,Mwana FA ,Joh Makini ..Kala Pina,Afande sele.. Inspector Aroun...mkuu Nina mashaka na uelewa wako wa Rap Game
Mwana FA, Inspector wanaimba bongo fleva sio rappers, Chindo, fazza Nelly,Joh makini wanafanya hardcore hiphop, sio pure rappers. Jay mo hana uandishi, ila ana flow, ila anaimba zaidi bongo fleva tangu enzi za cheza kwa step.
 
Fid hana mchango wowote Kwa jamii
 
Huyo Dizasta vina ni mchumba na vimistar vya kuunga unga.... Hapo mkali Fid... Walau huyo Songa yupo vizuri kwenye story telling
Mpe sikio vina sio shoga kama wote ni kichwa haswa
 
Tujifunze kutofautisha, Prof Jay, Afande sele,Juma Nature, Mwana FA sijui kina Jay mo hao ni pioneers wa Bongo fleva sio rappers. Rapper pekee mwenye misingi ya Rap wa kutokea kitambo hicho ni Fid q angalau na Sugu, ila sugu ni hiphop zaidi sio speciffically rapper.
 
Ni sahihi kumuita prof Jay Mwanahiphop/bongofleva bora, Ila si sawa kumuita rapper bora. Mfano nyimbo kama zali la mentali,kamili gado,starehe,nikusaidieje n.k unaweza kunipa 'mstari kwenzi' hata mmoja hapo? Ni nyimbo za hiphop/bongo fleva za kawaida sana sio pure rap.
Hizo nyimbo ulizotaja ni story..focus ya uandishi inakuwa tofauti na nyimbo za mtindi mwingine. (Kasoro hiyo starehe. Professor hana wimbo unaitwa Starehe.)
Ushawahi kuandika hata verse moja?

Story telling inategemea zaidi mpangilio wa mawazo kuvutia hadhira kuliko hizo dope bars.

Nyimbo za kimtaa, hustle na starehe ndiyo hufocus kwenye mistari konzi ili hadhira iendelee kuwa engaged na entertained.

Kama unamsikiliza Tupac, utajua Keep your head up au Brenda gotta Baby hazina mstari wowote konzi. Yet ni Ngoma kali kabisa.

Pia, kuchanganya ladha kidogo, hakumfanyi rapper aache kuwa rapper. Tunzingatia catalogue yake kwa ujumla.

Hata Eminem ana Ngoma kama Hailie anaimba kabisa. Je, na mara nyingi anaimba bridges kwenye nyimbo zake. Ref: Not Afraid na So bad. Je, tuseme Em si rapper mkali tena kwa kuwa huwa anajiimbisha sometimes?
 
Tujifunze kutofautisha, Prof Jay, Afande sele,Juma Nature, Mwana FA sijui kina Jay mo hao ni pioneers wa Bongo fleva sio rappers. Rapper pekee mwenye misingi ya Rap wa kutokea kitambo hicho ni Fid q angalau na Sugu, ila sugu ni hiphop zaidi sio speciffically rapper.
Misingi gani ya rap ambayo Fid Q anayo ambayo Professor Jay, Afande Sele au FA hana?
 
Kama BAKITA kweli taasisi zingine za Lugha na sanaa zinatambua na kuenzi kazi za sanaa, basi nadhani wasanii hawa walipaswa kuenziwa na ikibidi kuthaminiwa sana na serikali kwa kuwashirikisha katika matukio muhimu ya sanaa badala kuwashirikisha watumbuizaji peke yao ambao hawana mchango wowote zaidi ya burudani pekee.

Laiti kama serikali ingetambua michango na maudhui ya wasanii hawa wangeweza kuwatumia zaidi si tu kuburudisha, bali kuelimisha jamii.

Hii ni orodha ya wasanii watatu wenye uandishi bora ambao ukisikiliza utajiuliza ukubwa wa IQ zao mpaka kupata hizi tenzi.

3. Fid Q
Haina ubishi, kila mmoja anamfahamu, huyu ni mmoja kati ya nguli na miamba ya rap Tanzania, uandishi wake una ladha ya aina yake.Mfano

"kutaka kujua ukwel ni sawa na kumenya kitunguu kila ganda litakutoa chozi na kubaki macho juu juu"
View attachment 3122560

2. SONGA
Linapokuja suala la uandishi wa mistari, inajulikana Songa, pamoja na sauti yake ya upole isiyo na mbwembwe lakini IQ yake ni kubwa sana, mfano

"Wazazi wanasema nimeshakua
Ina maana… vibaya na vyema nimeshajua
Jua linazama tazama inanyesha mvua
Nakesha kwa dua kumuombea anayekesha akivua"

View attachment 3122568

1. DIZASTA VINA
Huyu katika ulimwengu wa Rap ana dunia yake! Hakuna msanii yoyote anayeweza au aliyewahi hata kumsogelea katika uandishi na ubora wa mistari yake.Ni mmoja kati ya rappers wenye IQ kubwa sana, Tukianza kumuelezea sifa zake nadhani hatutamaliza leo, Ila itoshe kusema ni hazina kubwa sana kwa taifa. Hata uhalisia wa maisha yake unajieleza, si mtu wa kujipendekeza, kushiriki siasa, kutafuta umaarufu, mapenzi n.k ni rapper anayeishi misingi ya rap kweli, kazi yake kushika kalamu na kuelimisha jamii. Ingekuwa Marekani tungeweza kumfananisha na Kendrick Lamar
Baadhi ya Lyrics zake:

"Eyo eyo kwa Insha na methali
Nawazika ka Ujamaa ulivyozikwa na Ubepari
Nishachoka na uongo so nafoka mpaka mtondogoo
Kwa world class Protocal, Internationally"

"Hizi tenzi ni pure, Niko real toka enzi nakua
Nili-rap kabla mapenzi sijajua
Kwenye game wanavyoenzi majuha
Wana track mbovu na wanafanya Media tours"

"Niko shega Bro
Genius ni Understatement half Man half God Paradox
Niite Vina just for lack of the better words
Literally, yet metaphorically undebatable"

"Sikutaka kutoka niliingia chaka
Nikatulia nikaisoma dunia utafikiria NASA
Nikawa fear factor, nikashika njia
Wabia wakanihofia kama wanavyoihofia Cancer"

View attachment 3122576
Acha izo
Hv Kuna mtu aliye Fanya vzuri kama Chidy Benz au sababu mnamuona ana shoti
 
Mpe sikio vina sio shoga kama wote ni kichwa haswa
Rapper inatakiwa uwe mkali kwenye flows... Sasa yeye flows zake zimepoa habadiliki... Rappers Bora 5 wa muda wote, fuatilia flows zao ndo utajua kama huyu jamaa Yako anajua ku-rap kweli au anaunga vimistari.
Tupac, Notorious BIG, Jay Z, Nas Eminem

Huyu jamaa Yako anazumbaa sana kwenye beat Hana ladha kabisa... Kuandika anajua but Hana flows nzuri na Yuko predictable/ dormant
 
Wazee vipi kuhusu Albert Mangwea RIP na Godzilla RIP
Hamna hata mmoja anaingia kwenye iyo list ya The best rappers?
 
Back
Top Bottom