Top 3 GOAT Tanzania Rappers, Serikali itambue mchango wao ikibidi watunukiwe Phd

Top 3 GOAT Tanzania Rappers, Serikali itambue mchango wao ikibidi watunukiwe Phd

Hizo nyimbo ulizotaja ni story..focus ya uandishi inakuwa tofauti na nyimbo za mtindi mwingine. (Kasoro hiyo starehe. Professor hana wimbo unaitwa Starehe.)
Ushawahi kuandika hata verse moja?

Story telling inategemea zaidi mpangilio wa mawazo kuvutia hadhira kuliko hizo dope bars.

Nyimbo za kimtaa, hustle na starehe ndiyo hufocus kwenye mistari konzi ili hadhira iendelee kuwa engaged na entertained.

Kama unamsikiliza Tupac, utajua Keep your head up au Brenda gotta Baby hazina mstari wowote konzi. Yet ni Ngoma kali kabisa.

Pia, kuchanganya ladha kidogo, hakumfanyi rapper aache kuwa rapper. Tunzingatia catalogue yake kwa ujumla.

Hata Eminem ana Ngoma kama Hailie anaimba kabisa. Je, na mara nyingi anaimba bridges kwenye nyimbo zake. Ref: Not Afraid na So bad. Je, tuseme Em si rapper mkali tena kwa kuwa huwa anajiimbisha sometimes?
Hapo kwa Tupac, unajua kwanini sometimes Eminem, Kendrick Lamar,Nas hata Lil Wayne wanatajwa mbele ya 2pac ila best Hiphop anabaki kuwa 2pac na BIG?
Mbona ROSTAM wanafanya story telling lakini humohumo kuna dope bars? Same to fid q, Songa n.k

Prof na wengine kama Afande sele, Jay mo n.k wako vizuri kwenye story telling lakini sio rap.
 
Inaonekana umezaliwa around mwaka 2000, jaribu kupata nafasi ya kusikiliza kazi za wasanii kabla hujazaliwa.
Pfofesa Jay alifanya wazazi wetu waanze kusikiliza muziki wa kufoka foka baada ya kusikia wimbo wake wa chemsha bongo.
Sugu alianza kuimba harakati zilizokosoa maovu ya Serikali kupitia Album yake ya Muziki na Maisha.

Hiyo ni mifano michache tu ya wasanii wanaopaswa kuwa kwenye kundi la G.O.A.T, hao uliowataja ukiondoa fid q hawastahili kuwa kwenye hilo kundi.

Mimi binafsi naona kama kuna wasanii watatu wanapaswa kupewa tuzo za u GOAT kwenye sanaa ya muziki Tanzania ni :
1. Profesa Jay
2. Sugu
3. Afande Sele
 
Inaonekana umezaliwa around mwaka 2000, jaribu kupata nafasi ya kusikiliza kazi za wasanii kabla hujazaliwa.
Pfofesa Jay alifanya wazazi wetu waanze kusikiliza muziki wa kufoka foka baada ya kusikia wimbo wake wa chemsha bongo.
Sugu alianza kuimba harakati zilizokosoa maovu ya Serikali kupitia Album yake ya Muziki na Maisha.

Hiyo ni mifano michache tu ya wasanii wanaopaswa kuwa kwenye kundi la G.O.A.T, hao uliowataja ukiondoa fid q hawastahili kuwa kwenye hilo kundi.

Mimi binafsi naona kama kuna wasanii watatu wanapaswa kupewa tuzo za u GOAT kwenye sanaa ya muziki Tanzania ni :
1. Profesa Jay
2. Sugu
3. Afande Sele
Sugu duh!
 
Rapper inatakiwa uwe mkali kwenye flows... Sasa yeye flows zake zimepoa habadiliki... Rappers Bora 5 wa muda wote, fuatilia flows zao ndo utajua kama huyu jamaa Yako anajua ku-rap kweli au anaunga vimistari.
Tupac, Notorious BIG, Jay Z, Nas Eminem

Huyu jamaa Yako anazumbaa sana kwenye beat Hana ladha kabisa... Kuandika anajua but Hana flows nzuri na Yuko predictable/ dormant
Mkuu ukimsikiliza Kendrick Lamar unaona amepoa au hajapoa? Hao kina BIG na Jay z wanafanya hiphop zaidi, ila kwenye rap hapana
 
Misingi gani ya rap ambayo Fid Q anayo ambayo Professor Jay, Afande Sele au FA hana?
Mwana FA huyuhuyu aliyeimba bado niponipo, mwanaume suruali, mabinti? Nitajie punchline moja tu kwenye hizo nyimbo! Prof jay nineshazungumza hapo juu, Afande sele hao ni bongo fleva
 
Kama BAKITA kweli taasisi zingine za Lugha na sanaa zinatambua na kuenzi kazi za sanaa, basi nadhani wasanii hawa walipaswa kuenziwa na ikibidi kuthaminiwa sana na serikali kwa kuwashirikisha katika matukio muhimu ya sanaa badala kuwashirikisha watumbuizaji peke yao ambao hawana mchango wowote zaidi ya burudani pekee.

Laiti kama serikali ingetambua michango na maudhui ya wasanii hawa wangeweza kuwatumia zaidi si tu kuburudisha, bali kuelimisha jamii.

Hii ni orodha ya wasanii watatu wenye uandishi bora ambao ukisikiliza utajiuliza ukubwa wa IQ zao mpaka kupata hizi tenzi.

3. Fid Q
Haina ubishi, kila mmoja anamfahamu, huyu ni mmoja kati ya nguli na miamba ya rap Tanzania, uandishi wake una ladha ya aina yake.Mfano

"kutaka kujua ukwel ni sawa na kumenya kitunguu kila ganda litakutoa chozi na kubaki macho juu juu"
View attachment 3122560

2. SONGA
Linapokuja suala la uandishi wa mistari, inajulikana Songa, pamoja na sauti yake ya upole isiyo na mbwembwe lakini IQ yake ni kubwa sana, mfano

"Wazazi wanasema nimeshakua
Ina maana… vibaya na vyema nimeshajua
Jua linazama tazama inanyesha mvua
Nakesha kwa dua kumuombea anayekesha akivua"

View attachment 3122568

1. DIZASTA VINA
Huyu katika ulimwengu wa Rap ana dunia yake! Hakuna msanii yoyote anayeweza au aliyewahi hata kumsogelea katika uandishi na ubora wa mistari yake.Ni mmoja kati ya rappers wenye IQ kubwa sana, Tukianza kumuelezea sifa zake nadhani hatutamaliza leo, Ila itoshe kusema ni hazina kubwa sana kwa taifa. Hata uhalisia wa maisha yake unajieleza, si mtu wa kujipendekeza, kushiriki siasa, kutafuta umaarufu, mapenzi n.k ni rapper anayeishi misingi ya rap kweli, kazi yake kushika kalamu na kuelimisha jamii. Ingekuwa Marekani tungeweza kumfananisha na Kendrick Lamar
Baadhi ya Lyrics zake:

"Eyo eyo kwa Insha na methali
Nawazika ka Ujamaa ulivyozikwa na Ubepari
Nishachoka na uongo so nafoka mpaka mtondogoo
Kwa world class Protocal, Internationally"

"Hizi tenzi ni pure, Niko real toka enzi nakua
Nili-rap kabla mapenzi sijajua
Kwenye game wanavyoenzi majuha
Wana track mbovu na wanafanya Media tours"

"Niko shega Bro
Genius ni Understatement half Man half God Paradox
Niite Vina just for lack of the better words
Literally, yet metaphorically undebatable"

"Sikutaka kutoka niliingia chaka
Nikatulia nikaisoma dunia utafikiria NASA
Nikawa fear factor, nikashika njia
Wabia wakanihofia kama wanavyoihofia Cancer"

View attachment 3122576
Kama unaongelea bilingual naungana na wewe ila kama ni kuongelea wasanii ambao style yao ilibamba na kufanikiwa kufikisha message kwa jamii! Huwezi muacha Jay hapo!
 
Mkuu ukimsikiliza Kendrick Lamar unaona amepoa au hajapoa? Hao kina BIG na Jay z wanafanya hiphop zaidi, ila kwenye rap hapana
Yeah nakubaliana na Ww kuhusu Jigga na Big kutokuwepo kwenye rap lyricism haswa but mantiki yangu ilikua kwamba mkali wa rap anatakiwa awe na flows nzuri zisizochosha.....

Kendrick anajua but kwangu dizain flan simkubali.... But frankly speaking huyu dizasta vina humwoni km Hana flows nzuri na anachosha?
 
Wazee vipi kuhusu Albert Mangwea RIP na Godzilla RIP
Hamna hata mmoja anaingia kwenye iyo list ya The best rappers?
Mamgwea ni mkali, ila kidogo yupo kwenye Bongofleva, sio mwandishi mzuri na hana mistari kwenzi ya rap. Anajua kuflow tu.Godzilla hana tofauti sana, Ila ni best freestyler
 
Inaonekana umezaliwa around mwaka 2000, jaribu kupata nafasi ya kusikiliza kazi za wasanii kabla hujazaliwa.
Pfofesa Jay alifanya wazazi wetu waanze kusikiliza muziki wa kufoka foka baada ya kusikia wimbo wake wa chemsha bongo.
Sugu alianza kuimba harakati zilizokosoa maovu ya Serikali kupitia Album yake ya Muziki na Maisha.

Hiyo ni mifano michache tu ya wasanii wanaopaswa kuwa kwenye kundi la G.O.A.T, hao uliowataja ukiondoa fid q hawastahili kuwa kwenye hilo kundi.

Mimi binafsi naona kama kuna wasanii watatu wanapaswa kupewa tuzo za u GOAT kwenye sanaa ya muziki Tanzania ni :
1. Profesa Jay
2. Sugu
3. Afande Sele
Nimeshatolea ufafanuzi hapo juu mkuu, Hao ni wasanii wa Bongofleva/hiphop kiasi, Ila sio Rappers. Rappers wengi wana IQ kubwa na uandishi wao upo more complicated
 
Mwana FA huyuhuyu aliyeimba bado niponipo, mwanaume suruali, mabinti? Nitajie punchline moja tu kwenye hizo nyimbo! Prof jay nineshazungumza hapo juu, Afande sele hao ni bongo fleva
Nilikuambia huwezi judge ubora wa msanii kwa nyimbo mbili au tatu.. angalia catalogue yake nzima..
Pia, kwako punchline ni nini?

Kwa mfano FA anaposema 'umimegewa demu wako nawe tafuta mnyonge ummegee, haipunguzi maumivu inarudisha hadhi ya kiume'. Je, hiyo ni punchline au siyo?
 
Nilikuambia huwezi judge ubora wa msanii kwa nyimbo mbili au tatu.. angalia catalogue yake nzima..
Pia, kwako punchline ni nini?

Kwa mfano FA anaposema 'umimegewa demu wako nawe tafuta mnyonge ummegee, haipunguzi maumivu inarudisha hadhi ya kiume'. Je, hiyo ni punchline au siyo?
Catalogue zao haziwaonyeshi kuwa rappers,na waandishi bora, bali zinawaonyesha kuwa wasanii wa bongofleva. Tofauti na Catalogue ya Fid q
 
Kama unaongelea bilingual naungana na wewe ila kama ni kuongelea wasanii ambao style yao ilibamba na kufanikiwa kufikisha message kwa jamii! Huwezi muacha Jay hapo!
Jay ni bilingual pia, Zamani alikua ana rap kwa English..isikilize fascinating rhythms ngoma ya 1997
 
Nimeshatolea ufafanuzi hapo juu mkuu, Hao ni wasanii wa Bongofleva/hiphop kiasi, Ila sio Rappers. Rappers wengi wana IQ kubwa na uandishi wao upo more complicated
Tupe tofaouti ya rapper na hip hop kiuimbaji huyo songa nae alishafanya story telling nying tu. Na kuimba kabisa, mimi nafikiri wewe umedata na ile style tu Stanza ambayo imetumiwa sana na Tamaduni, at list ungemueka NAsh Maalim juu kuliko songa ningeelewa lakini art aliyonayo prof hasa kwenye kutembea clean kwenye beat na utunzi hafananishwi hapa bongo labda marehemu Ngwair angekuja kumfikia. Prof ni rapper ni mtunzi na entertainer vile vile ni complete package inaweza kushindanishwa kwenye nyanja zote za rap na hiphop sanaa hio. Ndio msanii nimewahi kuhudhuria show yake miaka hio akichana nusu verse anasikia mashabiki then dk nzima akijakuendelea anaikuta nyimbo katikati ya verse ya mwisho na haruk mstari na hapo ni beat tupu anaiiunga. Mpeni maua yake jamaa anakipaji na hakuna mwandishi wa kumgusa
 
Bongo wanahiphop watatu wa muda wote ni
1. Jay
2. Fid
3. Langa
 
Back
Top Bottom