Tetesi: Tozo Mpya Kutuma fedha kwa simu kufa, Watanzania walia

Tetesi: Tozo Mpya Kutuma fedha kwa simu kufa, Watanzania walia

Kwa hiyo unashangilia kukomolewa? Kumbuka tutakoma wote, hakuna cha huyu mtoto wa mjomba au wa shangazi.
Wala sikomolewi , shughuli zangu zinahitaji uimara wa barabara sasa mkuu bila hivyo nitazidi kupata hasara.

Kukatwa hicho kiasi kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ni sawa kwangu
 
Naona vibanda vingi vya mawakala wakifunga biashara zao

Time will tell..
 
Hawa wapuuzi wanaojipangia kodi tu kiholela holela inatakiwa na wao waanze kulipwa laki 5 au laki 6 ili wakati wanatunga sheria zao za kindezi kama hizi waone athari zake!

Sehemu pekee ya kuimpose kodi ni kwenye vitu ambavyo ni optional sio vitu vya lazima kwa kila mtu kutumia kama miamala!

Wekeni hizo sh.100 kwenye viwanja vya mipira watu wanajazana karibia elfu 60 kila mechi ikichezwa they can get alot of money from such activities!

Waweke tozo hizo kwenye vitu kama highspeed roads ambako sio lazima mtu kutumia! Wajenge autobahn waweke tozo waone kama watu hawatalipa😅

Kodi zinatakiwa ziwe fun to pay ujiskie raha tokana na convenience unayopata sio unatozwa kodi kwenye kitu ambacho hakiburudishi zaidi unaumia tu. Sijui hawa watu wanafikiria kutumia matako!

Wasajili malaya wawape maeneo maalum waanze kulipia kodi watu watalipia tu wala hawatanung’unika. Ile ni starehe mtu hawezi umia!

Waweke kodi kwenye vinywaji kama bia! Watu watazinywa tu bila kujali kodi ni sh.100!

Shida ya wenye mamlaka hawataki ku diversify kodi hizi wanataka zote warundike sehemu moja! Simu itozwe kodi kwenye vocha,internet, voice na sms, line itozwe kodi, bado serikali wabandike kodi juu tena!?

Mafuta yakiingizwa yalipe kodi, leseni ya sheli inatakiwa ilipe kodi, mjazaji mafuta alipe kodi ya reli na sasa ya uzalendo 😅😅😅
inasikitisha sana ila wanapata nguvu kwaamna wanapigiwa makofi na Covid 19 na genge lao.
 
Ujinga wa kuazisha miradi mingi kwa wakati mmoja wakati uchumi wetu ni wakuokoteza ndio sababu ya hili tatizo.
JPM alikua anatoa wapi hela za kulipia miradi hii? Tena kwa muda bila kuwachelewesha kandarasi! Jana wa machinjio ya Vingunguti mpya TBA sijui ilikua wafungue 1.7.2021 kwa amri ya waziri mkuu ila wamesema walikwama wakidai hawajalipwa almost 3b plus ya kumalizia kufunga AC na bwawa la kutunzia mbolea ndio maana wakasimama.

Zamani hela zilikua zinatoka wapi

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Wala sikomolewi , shughuli zangu zinahitaji uimara wa barabara sasa mkuu bila hivyo nitazidi kupata hasara.

Kukatwa hicho kiasi kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ni sawa kwangu
Tatizo haziimarishi chochote,labda kuimarisha mifuko ya wachache hazina: wanaiba sana
 
Tatizo haziimarishi chochote,labda kuimarisha mifuko ya wachache hazina: wanaiba sana
Kwa nini Mzee? Umeshaambiwa pesa inaenda Tarura bado unabisha sasa sijui unataka nini?

Ungekuwa kwenye sekta ya ujenzi hususani mkandarasi ungekubaliana na mimi,hivi navyoongea baadhi ya mikoa wakandarasi wameshazidiwa na Kazi ,Kazi ni nyingi sana za barabara,fungua kampuni miaka ya mama kazi za barabara ni nyingi sana
 
Mama anakaribisha wawekezaji kwa kasi,mama anafungua nchi na kazi iendelee.
Magufuli aliwabana sana matajiri sasa mama anawafungua matajiri wafunguke wawezavyo.
 
Hayo ni matokeo ya SGR na Nyerere dam.----- lazima tutaipata.
Malizia chini ya kiongozi dhaifu samia ,,,maana chini ya magu mambo kama haya ya kutwisha mzigo zaidi wananchi tulikuwa tumesha ya ya sahau hata kwa wakulima
 
Kazi kubwa ya CCM huwa ni kutengeneza matatizo, ili baadaye ije itatue matatizo iliyokwisha yatengeneza...

Comes general election, mnaambiwa tumetatua kero hii, mara kero ile...mnatoa kura kiulainiiiii
 
Mitano mingine kwa Maza,si mnaona wenyewe anavoupiga mwingiiii kama Gaucho..!
 
Back
Top Bottom