TPDC yaingia mkataba na Kampuni ya Uingereza ya Baker Botts kwa ajili ya ushauri wa Kisheria

Si tetei ila tr 70 ni hela nyingi sana ku gamble, hao ulio wataja wana uzoefu wa maswala ya gas kiasi gani. Hao tpdc zaidi ya kununua crude oil wana jua vipi uchimbaji na usindikaji wa gas?
Hawajui ndio maana ilibidi watafutiee watalaaamu
 
Makamba mpaka hiyo wizara ni billionea.
Huyu jamaa mnamchukia bure tu....angalieni msijichumie dhambi.
Sasa mimi nimchukie January kwa kipi na wakati atushei chochote kwenye maisha zaidi ya umeme.

Wewe kwa akili yako timamu January akae kwenye negotiation ya dili ya trillion 80 bila kupata chochote,
 
Kwa hiyo mkisha ingia huo mkataba mna uwezo wa kuchimba? Mna mtaji wa tr 70? Ni kwamba una sema tuwa kwepe wazungu, ukweli ni kwamba hatuwezi
 
Kwa hiyo mkisha ingia huo mkataba mna uwezo wa kuchimba? Mna mtaji wa tr 70? Ni kwamba una sema tuwa kwepe wazungu, ukweli ni kwamba hatuwezi
kaka hatuongelei PPP tunaongelea wanasheria kuiguide serikali katika kuingia huo mkataba na kampuni za oil and Gas.Transactional lawyers. kwamba sisi hatuwezi hata hilo, mpaka tu hire foreign consultants.coz katika negotiation za mikataba wanasheria wa pande zote wanapambania rights za upande wao.
 
Hii chuki binafsi husda husda na kutosikiliza na kuyaelewa mambo kisha ukachangia. Serikali inataka kuingia kwenye biashara ya gesi na haijawahi kwa sababu hizo hizo za kuhofia kuingia bila tathmini ya kina na kuingia kwa uangalifu zaidi. Inshort hiyo mialamala haijawahi kuifanya na ndipo wamemtaka mtaalamu mshauri apitie hizo bei kuanzia kuzalisha mpaka process ya mwisho na kutuonyesha mbivu na mbichi kwenye eneo la gesi. Kisha sasa serikali inapeleka team yake kuzioitia ikiwa na uelewa wa dunia ikoje kisha wanarudi tena mezani wanajadili wapite njia gani hadi kufikia nani afanye nini na alipe nini ndipo tuje na lugha MKATABA WA GESI! Mh. Makamba ataendelea kuwa the best visionary leader tu hata umpige jiwe gani!
 
Uko na hiyo haki ya kuelewa hivyo ulivyoelewa mkuu so sitakulebal kama wewe ulivyonilebal. Muhimu Mungu atupe uzima tu ili mambo yakiwa revealed sote tuwe mashahidi.
 
Yaani hao hao kina Karl Peters ndiyo hao hao wakupe ushauri wa kisheria kuhusu raslimali zako.

Hii inathibitisha pasi shaka kwamba Tanzania tunao kina chief Mangungu wasomi waliosomea umangungu wa kiwango cha phd
 

London​

Level 30 20 Fenchurch Street
London EC3M 3BY
United Kingdom
P:+44.20.7726.3636
F:+44.20.7726.3637

Zama zile zinarudi kwa kasi sana na hatutaki baadae tuanze kulaumiana kwamba kampuni ni hewa na wala haina ofisi. Sisi wanajamii forum kwanini tusimpeleke Mzee wetu nguli Pascal Mayala akathibitishe kama kampuni tajwa ni halali na ina ofisi pale London?. Hili wazo likikubalika tutamchangia fedha za nauli pamoja na malazi kwa siku zote akiwa London. Japo sina uhakika kama amechanja au laah.
 
Kuna Mawaziri wamewekwa kwenye Wizara kimkakati, mmoja wapo ni huyu Kijana January na huyu Mtoto wa Msoga;
Ya January ndo hayo yanaanza kujiinua, tusubiri na ya Ridhiwan..... nawaza vile Ardhi itakavyochezewa stay tune........More to come!!
Mungu Ibariki Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…