TRA, inakuwaje ushuru wa kuingiza gari ni mkubwa kuliko bei ya gari lenyewe?

TRA, inakuwaje ushuru wa kuingiza gari ni mkubwa kuliko bei ya gari lenyewe?

~ Roho za kwa nini haziwezi kutuacha salama...wanaona watu wa kawaida wakimilika magari watafaidi sana na kula nao sahani moja,hapo Botswana ushuru wao upo chini...wanatumia bandari SA...unaambiwa hata mama ntilie anamiliki chuma yake inampeleka kijiweni na kumrudisha nyumbani,bot ni afrika sio ulaya.
 
Mkuu huo ndo uhalisia na hilo ndo tatizo lililopo maana haiwezekani Legacy BM9 au VW Jetta ya 2009 ziwe na CIF kubwa maana hawa washamba wakiona muundo wa gari zuri tu wanaweka CIF $9000-11,000, Subaru Forester SG9 au SH9 ushuru 17,000,000 na kuendelea hadi unashangaa
Sio na karoho ka korosho kama kawaida ya mbongo?
 
Tatizo kubwa ni kwamba kwenye kitengo cha Valuation ya magari wamewawela watu waliotoka shamba hivyo kufanya makadirio makubwa ya magari ya kawaida sasa mtu katoka ileje au misungwi kaja mjini chuo kikuu anaambiwa afanye valuation ya VW Touareg au VW Jetta ya 2009 matokeo yake anafanya kodi ya gari ya CIF $3000-4000 kodi yake ina kua 18,000,000 yani faida kubwa inapata serikali zaidi hata ya wanaouza gari
Siyo swala la mtu katoka wapi, hiyo ni sera ya serikali hata ukienda wewe hapo TRA utatumia formula hiyo hiyo
 
Hoja dhaifu kabisa Tanzania nchi changa bado tunahitaji nondo kwa ujenzi wa miundombinu so hayo magari yakichoka kabisa tunayeyusha kupata nondo
Kuna viwanda vingapi vya kuyeyusha magari skrepa kuwa nondo ?
 
Hii ishu nakumbuka last week nlikua namwagizia mshkaji vits ya mwaka 2003. Yaan gar inatoka kule mpaka inaingia bongo ni dola 1700. Ila huku ushuru wake ni milion 4 na upuuz mpka unajiuliza kisa nin kutufanyia hvi.
 
Hiko kitu hakipo, ila wewe upo na shida ya uwelewa wa kikotoo cha kodi ya magari. Kikotoo kimewekwa kwenye standardization ambayo kwa kila CIF (cost of insurance and Fright) matokeo yake ya kodi hayawezi kuzidi gharama za manunuzi.

Sasa shida inakuja umepata vipi gari kupewa gari bure, kununua gari mnadani, umenunua gari mkononi kwa mtu. Kwahiyo ikiwa gharama ulizotumia kuipata hyo gari zipo china kutokana na makadilio yaliyowekwa kwenye kikokotoo lazima italeta matokeo ya kodi kua kubwa zaidi ya Gharama za gari.

Note; Sheria ya kodi inasema, kodi inakua calculate kwenye CIF *whichever is higer* kati ya makadilio ya CIF kwenye TRA calculator na gharama halisi za gari hadi inafika port(CIF).

Pia, first method ya calculation za kodi ya forodha zinafanyika kwenye gharama halisi( actual transaction value) ila hii kwenye magari inakua applied endapo utatoa Reasonable evidence kua hiyo gari umeipata kwa hiyo gharama kwasababu makadilio ya gharama yalishafanyika na kupata Tools ya kutafuti kodi( TRA calculator).



Sent using Jamii Forums mobile app

Umeongea nini sasa? Amekuambia hadhani kua ni realistic kulipa kodi ya kiasi hicho kwa gari la aina na mwaka huo, issue ni je hizi gharama za kuingiza gari kuwa kubwa karibia au zaidi ya thamani ya kuliagiza zinaleta maana? Taking aside issue za dumping fee!
 
Hakuna kiwanda cha magari bongo lkn tozo ya magari imeegemea misingi ya protectionism
Kabisa!
Sijui kwa nini tuna copy na ku paste kila kitu bila kufikiri.

Kama tungekuwa na viwanda halafu tunaweka restrictions za magari kuingia kwa kuweka kodi kubwa hapo Sawa. Lakini kwetu ni tofauti kabisa.

Pia si katika magari tu, bidhaa nyingi zinazalishwa nje na kuuza kwetu bei ndogo wakati vilivyozalishwa ndani bei kubwa kwa sababu ya msululu wa Ushuhuru na kodi.

Sisi ni pumba hasa yaani....!
 
Kuna viwanda vingapi vya kuyeyusha magari skrepa kuwa nondo ?
Hata kama hakipo je hatutakuja kuwa nacho kabisa? Je wanaonunua na kuexport scraper huoni kuwa watakuwa na wigo mpana wa kupata mzigo? Yaani huoni hizo fursa za multiplier effects za kiuchumi? Tatizo bongo tunaongozwa na watu wenye akili ndogo?
 
Kabisa!
Sijui kwa nini tuna copy na ku paste kila kitu bila kufikiri.

Kama tungekuwa na viwanda halafu tunaweka restrictions za magari kuingia kwa kuweka kodi kubwa hapo Sawa. Lakini kwetu ni tofauti kabisa.

Pia si katika magari tu, bidhaa nyingi zinazalishwa nje na kuuza kwetu bei ndogo wakati vilivyozalishwa ndani bei kubwa kwa sababu ya msululu wa Ushuhuru na kodi.

Sisi ni pumba hasa yaani....!
Mabeberu weusi ni wabaya maramia afadhali ya beberu mweupe
 
Nenda kaangalie Subaru Legacy BM9 ya 2009/2010/2011/2012 uone gari ni $3500-5000 ushuru wake ni 22,000,000-25,000,000 mzee
Huyo haelewi kuwa pamoja na kodi ya umri la gari 30% bado ni affordable kuliko gari lenye umri chini ya miaka 8 ambalo halitozwi kabisa kodi ya umri
 
Back
Top Bottom