DOKEZO TRA, kodi za kuingiza Magari ni kichefuchefu kwa Wananchi

DOKEZO TRA, kodi za kuingiza Magari ni kichefuchefu kwa Wananchi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mie naweza nikaongea lugha nyingine ya kitalaamu kuwa why Kodi kubwa. Inawezakana serikali Ina discourage private ownership ya vehicles ,why Ina discourage?

Sababu ya barabara aka level of services like A,B,C,D,E and F. Sasa uwezo wa serikali kujenga road Kama ya kiwango Cha LoS A Ni gharama mno yaani mno kwanza hatuna uwezo.

Wakiweks ushuru chini gari zitajazana road mno itapelekea tutakuwa na LoS E or F ambayo utakuwa unasafiri hata km 200 kwa saa nne badala ya mbili ama tatu.

Kuna namna ya watu husika ama mamlaka ku discourage kila nzi kumiliki gari like kuanzisha toll roads, high parking fees, muda huo huo inatakiwa public transportation iwe nzuri kinyama ndicho inachojitahidi kwa DART sema Naona wanashindwa Mana bado Ni karaha kwa wwsafiri.
Hebu waza gari moja inabeba watu mbili na je hao Mia mbili kila mmoja angekuwa na gari lake huko road kungekuwaje.

Nchi yetu ama zetu unapoambiwa Ni masikini Ni ukweli Mana ukitaka ushuru uwe chini mno hata 20% ya Bei uliyonunulia.

Inatakiwa tuwe mpaka na njia nane ama multi lanes roads, hii road unajua inaweza jengwa kwa Bei gani tutajiuza mpaka sie utumwani ndipo tujenge hii roads Mana madini Kuna watu wanakula perse mpaka vizazi vyao. Labda magufuli angeipokea nchi tokea kwa nyerere akomae na mwendo ule ule nchi iwe na hela na akae madarakani mpaka muda huu yaani zaidi ya miaka 50 ndipo tungeweza Ila kwa Hali hii bwawa linacheleweshwa ili watu wauze gesi zao Mana Wana hisa sio leo tusubirie kwanza.

Na tumeambiwa kuwa kuni na mkaa unaleta mapafu homa sijui Nini tutumie gesi ili kuwanenepesha akaunti zao,yaani we are like fodders to feed their bank accounts for their incoming generation.

Wakati miaka takribani Bilioni na mabilioni binadamu amekuwa alitumia kuni na mkaa.

Ila Sasa huyu kisa kiongozi anajua kuwa tunamuona Kama Mungu ana akili Sana kuliko yeyote. Kuna muda tajiri anawaza kuwa masikini Hana akili kabisa kisa ya yeye kumiliki pesa Ila sio wote lakini yaani Kuna watu wale wenye dharau.

Samahani kwa kuwachanganyia maada jamani tozo zimetuvuruga kinyama yaani huyu maza inabidi nimtumie maza alfu kumi kwa Basi Mana kwa tozo atapokea Kama alfu tano ya kutuma na kutolea.

Mana mchumia tumbo degree 12 Hana uwezo wa kuzalisha vyanzo vya uchumi ama uwekezeji ili akusanye Kodi Bali anacheki Ni wapi pa kukwapua huyu asiwe nacho kabisa.

Kama sio kuwa wanatengeneza tatizo halafu wanalitatua ili watt wamkubali baba na mama kuwa wako nondo I don't know.
Kama walivyoua reli ya Arusha wakaja wakaifufua wakajisifu kwa wananchi kuwa Ni wajanja nipeni mrija nizidi kuwannyonya damu mbakie skeletons...

I am lost
Umeanza vizuri umemaliza vibaya,
Nikukumbushe tu tozo alianza kutuwekea magufuli sh 100 kwa kila lita 1 ya mafuta ya taa, disel na petrol na na baadae ikawa 200, unanunua mafuta ya taa kwa ajili ya kujimulikia na familia yako lkn unamlipia na kodi mwenye gari, hii ndio ilitakiwa kukemea vikali sana lkn kwa kua kuna watu waliamini magu hua hakosei na hana baya ikitokea kakosea au kafanya baya unarudi kwenye kanuni ileile kua magu hua hakosei ndio maana hamkupiga kelele kuhusu hii tozo, wenye magari halipii tena kodi gari yake ila wamemuwekea kwenye mafuta ila tunasahau mafuta sio kwa ajili ya magari tu....

Kwa kua hamkuona baya kwa magu nami naungana na mama kua anaendelea alipoishia magu na kudumisha alivyovianzisha na kuviboresha ikiwa na pamoja na tozo. Ila tuwe wapole tu

Kuhusu kodi za magari wengi humu hawana uelewa, mtu unaagiza gari ya mwaka 2013 now tupo 2022 na ilishatumika ina km laki na ushee huko yaani tunaleta skrepa huku kwetu afu watuwekee kodi ndogo? Hata watoto wetu wa o level wangeenda shule kila mmoja na gari yake, ile kodi ya uchakavu ndio hua ni kubwa nenda kaagize gari mpya kabisaaa uone kodi zake zipoje ndio urudi hapa kuja kuilaumu serikali.

Hivi mshajiuliza gari umeitumia miaka 10 na ushee afu unamuuzia mtu hiyo itakua gari au skrepa?
 
Gari chakavu lazima watu watakufa kila siku na wataleta visababu kibao kumbe kodi inachangia hadi basi la abiria mtu anabembeleza used za miaka kibao kumbe kodi himilivu watu wataleta vyuma vipya, magari imara huokoa pia uhai wa watu
Wazambia walikua wanapiga picha wakiliona Scandinavia pale Lusaka leo hii wao wana bus zingine zinaenda vijijini huko na wametuacha mbali mno maana wapo kwenye series ya body za Iriza Q 10 wakati hizo Tanzania ni anasa kwa kodi yake wanaona wachonge chonge bus kwa kutumia nondo na flat bar...baadae wanashangaa ajali ndogo ila ina madhara makubwa kwa abiria wao hawajui hilo ukiona watu wameshindwa kuwapa wenye shule wapate punguzo ili watoto wapande bus nzuri za kwenda shule au michezo wao wanakomaa na kodi tuu kama vile Nchi ipo jangwani..
 
Mind set yeti bado ni ya kimaskini maskini..........mbali na ukubwa huo wa kodi urasimu/uzembe/ kutokujali ktk taasisi za umma ni janga kubwa. Amini nawaambia kuna walio tayari kulipa hiyo kodi kubwa nao wamepanginshwa foleni ndeeefu kwa sababu za kipuuzi kabisa!. ......utasikia kutoa kibali cha kufanya biashara hii ama Ile itabidi kusubiri mbio za mwenge zipite wilayani hii!, ....au inabidi kusubiri zoezi la sensa lipite,...subiri ziara ya mkuu wa mkoa iiishe,......
 
Kazi ya serikali ni pamoja na kusimamia rasilimali za nchi, kukusanya kodi na kuhakikisha kodi ile inatumika kuwahudumia wananchi ikiwamo kujenga barabara, hospitali, shule na vyuo vya ufundi, kulinda raia na mali zao, kurahisisha maisha ya raia kwa kuweka sera rafiki na himilivu kwa raia wake, sasa wale waliopewa dhamana ya uongozi wanapogeuka waongo, wezi wa kutupwa shida huanzia hapo maana hata sheria watatunga za kuwalinda wao wenyewe na kumkandamiza raia asiye na hatia
 
Wakiacha ten percent kwenye miradi uwezekano wa kujenga miundo mbinu na miundo msingi ya kisasa upo
 
Penye miti hakuna wajenzi, Tanzania ina kila kitu lakini ilikosa viongozi toka uhuru, viongozi ambao waligawa rasilimali zetu kwa matapeli waliokuja kwa jina la wawekezaji tena wakatunga na sheria za kuwalinda hao matapeli
 
Suluhu mojawapo ni kuwa na bunge 50% hao wanaosema watatawala milele na 50% upinzani.

Ila sasa sisi wenyewe wananchi ndio shida namba moja. Wacha tuendelee kulialia tu.

Kwa akili za mtu kama magufuli anaedhani mpinzani anarudisha nyuma maendeleo ndio akili za viongozi wengi huko chichiemu, hawajiangalii wao ndio wenye dhamana ya kila kitu wanaangalia wapi wawakabe Chadema ili hao chadema wasifanye siasa wakati muda wa kuwabana wanasiasa wa upinzani wanageutumia kubuni mambo mbali mbali maendeleo yangekua suala dogo sana
 
Umeanza vizuri umemaliza vibaya,
Nikukumbushe tu tozo alianza kutuwekea magufuli sh 100 kwa kila lita 1 ya mafuta ya taa, disel na petrol na na baadae ikawa 200, unanunua mafuta ya taa kwa ajili ya kujimulikia na familia yako lkn unamlipia na kodi mwenye gari, hii ndio ilitakiwa kukemea vikali sana lkn kwa kua kuna watu waliamini magu hua hakosei na hana baya ikitokea kakosea au kafanya baya unarudi kwenye kanuni ileile kua magu hua hakosei ndio maana hamkupiga kelele kuhusu hii tozo, wenye magari halipii tena kodi gari yake ila wamemuwekea kwenye mafuta ila tunasahau mafuta sio kwa ajili ya magari tu....

Kwa kua hamkuona baya kwa magu nami naungana na mama kua anaendelea alipoishia magu na kudumisha alivyovianzisha na kuviboresha ikiwa na pamoja na tozo. Ila tuwe wapole tu

Kuhusu kodi za magari wengi humu hawana uelewa, mtu unaagiza gari ya mwaka 2013 now tupo 2022 na ilishatumika ina km laki na ushee huko yaani tunaleta skrepa huku kwetu afu watuwekee kodi ndogo? Hata watoto wetu wa o level wangeenda shule kila mmoja na gari yake, ile kodi ya uchakavu ndio hua ni kubwa nenda kaagize gari mpya kabisaaa uone kodi zake zipoje ndio urudi hapa kuja kuilaumu serikali.

Hivi mshajiuliza gari umeitumia miaka 10 na ushee afu unamuuzia mtu hiyo itakua gari au skrepa?

Kodi ya Tanzania kwenye magari na bidhaa nyingine itakushangaza hata wewe hadi gari mpya kodi yake haishikiki
 
Mind set yeti bado ni ya kimaskini maskini..........mbali na ukubwa huo wa kodi urasimu/uzembe/ kutokujali ktk taasisi za umma ni janga kubwa. Amini nawaambia kuna walio tayari kulipa hiyo kodi kubwa nao wamepanginshwa foleni ndeeefu kwa sababu za kipuuzi kabisa!. ......utasikia kutoa kibali cha kufanya biashara hii ama Ile itabidi kusubiri mbio za mwenge zipite wilayani hii!, ....au inabidi kusubiri zoezi la sensa lipite,...subiri ziara ya mkuu wa mkoa iiishe,......

Rafiki yangu mmoja wa ujermani aliwahi kunieleza always your leaders are at the picnic, maana alikua kila akienda kutafuta huduma anaambiwa mara subiri muda wa chai, mara katoka kidogo, mara kaenda kukojoa, mara anakikao yaani wanapoteza muda bila sababu na muda ni mali na kwa kutokujali kwao muda wanazidisha umaskini kila leo hakuna mtu ambae hakujali muda aliwahi kufanikiwa hayupo,
 
Inasikitisha SANA. Watanzania tunaishi kama mashetani yani...Ukiwa Tunduma unashuhudia lundo la gari nzuri nzuri za aina tofauti tofauti na hizi yebo yebo zetu tulizozizoea kuziona hapa bongo zikivuka boda kwenda nchi jirani.
Pana dogo mmoja Mzambia akitaka gari nzuri ananiuliza alianza na Cayyene,akaja Paramela,Evoque,Mercedes yatch back sasa hivi yupo na autobiograph range rover ya 2020 ana duka la hardware hapo Lusaka akitumia akilichoka miezi kadhaa analiweka sokoni anaongeza hela au ikiwa sawa ananunua gari zuri zaidi alishangaa nilipopita Lusaka na gari ya 2014 mwaka 2020 namwambia ndio yangu ya kutumia tena nilimwambia nimejitahidi sana maana kodi zetu sio rafiki akawa anasikitika tuu..
 
Rafiki yangu mmoja wa ujermani aliwahi kunieleza always your leaders are at the picnic, maana alikua kila akienda kutafuta huduma anaambiwa mara subiri muda wa chai, mara katoka kidogo, mara kaenda kukojoa, mara anakikao yaani wanapoteza muda bila sababu na muda ni mali na kwa kutokujali kwao muda wanazidisha umaskini kila leo hakuna mtu ambae hakujali muda aliwahi kufanikiwa hayupo,
Unataka kulipa kodi tra mnaambiwa wapo kwenye kikao au mtandao mbovu unabaki kusubiri pana jamaa ni mtumishi wa Serikali hapa Tanzania nilimpeleka wizara wanayotoa vibali vya magari hapo Sunnside Pretoria tulipokewa na watu wawili na wanakimbizana balaa na customer care yao ipo juu balaa baadae namwambia hapa ni bure hatulipi kitu alishangaa sana..
 
Hii nchi yetu vitu vingi unaweza kudhani vinafanyika kwa lengo la kutukomoa kabisa

Yaani kuingiza gari hapa kwetu ni kama kufanya anasa kabisa na sio usafiri

Ukiandaa 10M kuagiza kigali basi uandae 10M ya kodi, kama vile hatuna bandari yetu

Tumekuwa watumwa ndani ya nchi yetu wenyewe
==
Ni changamoto kubwa sana
 
Unataka kulipa kodi tra mnaambiwa wapo kwenye kikao au mtandao mbovu unabaki kusubiri pana jamaa ni mtumishi wa Serikali hapa Tanzania nilimpeleka wizara wanayotoa vibali vya magari hapo Sunnside Pretoria tulipokewa na watu wawili na wanakimbizana balaa na customer care yao ipo juu balaa baadae namwambia hapa ni bure hatulipi kitu alishangaa sana..

Yaani ustaarabu wa wenye dhamana ni mdogo kupita kiasi hadi unashangaa hawa shuleni walisomea ujinga au uvivu
 
Kodi inawekwa Kubwa Ili kupunguza idadi ya waagizaji magari. Kodi Ikiwa chini Kila mtu atanunua gar na itakuwa fujo. Mfano nchi ya Vietnam usafiri wao mkubwa ni pikipiki maana gar yoyote utakayonunua Kodi yake Kwa TSH n 80M.

Hivyo wanaotumia magari ni ni kama anasa tu.

Hata watumishi wengi wa serikali huko Vietnam wanaotumia pikipiki.

TRA Wako sahihi
Poverty Minded leaders kama wewe hamkosekani.

Unaongelea pikipiki kwa nchi ndogo kama mkoa wa tanga?

Kuna nchi kubwa sana, usafiri wa gari ni muhimu hata hizo pikipiki ni anasa tu.

Unaweza tumia pikipiki toka dar kwenda morogoro achilia mbali kufika iringa, mbeya, mwanza n.k?

Usiwe mjinga kama viongozi wako, watu wakiwa na magari mengi, multiplier effects ni kubwa kuliko kuwa na magari machache.

Wape nafasi wananchi wawe na uhuru wa kufanya watakayo mradi hawavunji sheria.
 
Narudia kuandika tena,

Ifikie hatua muwe waelewa huwezi kujifanya una calculator ya kodi kwenye magari ambapo kodi yenyewe unatoza asilimia 80% hadi 100% ya manunuzi hii sio sawa.

Kwa mikodi yenu mikubwa ndio maana hamuwezi mkawa na walipa kodi wengi.

Mkumbuke kodi kubwa inawafanya kuathiri biashara ya mafuta kwa ujumla, biashara ya vipuri.

Hakuna sababu ya kodi asilimia 80 hadi 100 wakati ndani ya nchi hatuna uzalishaji wa magari au viwanda vya magari hakuna na kodi inakua ya kuumiza sio sawa.

Kweli mtanzania anunue gari dola 5000 kodi apigwe dola 4000 hadi 5000 halafu mtakuja na formular zenu za ajabu ajabu aibu sana hii.

Uchumi hauwezi ukakua kwa mtindo huo muelewe magari ni kifaa au chombo kinachorahisisha kuinua uchumi kwa namna moja au nyingine.

* Bandari Kuwepo Tanzania haimsaidii nafuu ya maisha mtanzania, kila bidhaa iko juu viongozi sio wabunifu wapo wapo tu.
Tuna janga
Hatuna viongozi
 
Kama una uwezo basi usilalamike. Ila hatuwez kuruhusu Kila mtu kumiliki magari Kumi lazima yawe machache wengine watumie usafiri wa umma.
Poverty Minded leaders kama wewe hamkosekani.

Unaongelea pikipiki kwa nchi ndogo kama mkoa wa tanga?

Kuna nchi kubwa sana, usafiri wa gari ni muhimu hata hizo pikipiki ni anasa tu.

Unaweza tumia pikipiki toka dar kwenda morogoro achilia mbali kufika iringa, mbeya, mwanza n.k?

Usiwe mjinga kama viongozi wako, watu wakiwa na magari mengi, multiplier effects ni kubwa kuliko kuwa na magari machache.

Wape nafasi wananchi wawe na uhuru wa kufanya watakayo mradi hawavunji sheria.
 
Back
Top Bottom