TRA yafafanua ongezeko la ushuru wa magari

TRA yafafanua ongezeko la ushuru wa magari

Tuwakomalie wabunge wabadilishe hizi kodi za enzi za ujamaa kwenye magari. Japo unasema unalinda mazingira lakini kodi kubwa hivyo kwenye mtumba una viwanda vya magari?
Gari ni kitu kinachosaidia kukuza uchumi. Ingekuwa ni amri yangu ningeweka kodi karibu na sifuri. Kwenye magari ya kazi kama pickup na fuso watu wangenunua bila ushuru hata mia, ikiwezekana nawapa na hela ya asante😀😀

Kulalamika haya mambo haitusaidii kitu. Inabidi wabunge, wanasheria nk walifanyie kazi.
Hakuna wabunge wanaoweza kufanya hivyo
 
Nimeangalia bforward ist ya 2002 ya milioni 5.1 na visenti vyake mpaka dsm bandarini ushuru wake ni milioni 5.6 na visenti nyake. Kweli kagiza gari kwa sasa ni anasa.
Yan mm nimetoka kuagiza gari mwez uliopita...mpk kufika bansarini ilikuwa 5.4 milion

Kodi sasa,ilikuja 6.7 milioni hapo bado warfage cjui,port habdling charges na shipping charges ambayo ilikuja kama laki 7 hvi..jumla ni kama 7.3 milion mpk naikamata gari.. AJABU
 
This is not Africa but TANZANIA.

Ukienda Zambia hapo Kuna Gari zinatozwa Kodi milion 2 ila bongo gari Hilo Hilo Kodi Yake ni milion 12
Umimi na ubinafsi ndio shida gari au transport ni kilainishi cha maendeleo na si fahari tushushe shuru tuvune zaidi kwenye madini yetu tukivuna tu chuma chetu vizuri cha liganga ukawa ni mgodi wa serekali tukaomba tu teknolojia ya uimarishaji chuma kutoka kwa wachina tanzania itakuwa ya kipekee afrika na duniani #Tusiwape wageni kila kitu, huu uwe ni mgodi wa taifa letu. [SIONI UBAYA HATA TUKAUZA NDEGE 2 TUKAINGIZA PESA KWENYE MGODI WETU] National iron minings
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetolea ufafanuzi taarifa juu ya kupanda kwa gharama za kodi za magari yaliyotumika yanayoingia nchini.
Ufafanuzi huo umekuja wakati kukiwa na malalamiko ya wafanyabiashara ya magari wakidai kuwepo kwa ongezeko la kodi za magari ya mitumba.

Taarifa ya TRA iliyotolewa katika gazeti la Mwananchi leo Ijumaa Januari 8 imekuongezeka kwa ushuru wa baadhi ya magari kuanzia Januari mwaka huu kutokana na uthaminishaji uliozingatia bei halisi za magari hayo, huku pia magari mengine yakishuka bei.

“Kimsingi ongezeko hilo limetokana na bei halisi ya magari husika na hivyo haimaaishi kwamba TRA imeongeza ushuru wa magari,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

TRA imesema kuwa magari yaliyotumika hutozwa ushuru wa bidhaa kutokana na umri wa gari ambapo umri wa gari huhesabiwa kwa kufuata mwaka wakalenda.
Kwa upande wa magari madogo yenye umri wa maika minane hadi tisa pamoja na kodi nyingine hutozwa ushuru huo wa bidhaa kwa asilimia 15 na gari yeye umri zaidi ya huo hutozwa kwa asilimia 30.

“Hivyo ikiwa mwagizaji aliagiza gari binafsi lenye umri wa miaka tisa mwaka 2020 na likaingia nchini mwaka 2021 itatozwa ushuru wa bidhaa kwenye umri wa asilimia 30 badala ya asilimia 15 ambayo ingetozwa ikiwa gari yake ingewasili kabla ikiwa gari yake ingewasili kabla ya mwaka huu,” imesema TRA.

Mamlaka hiyo imefafanua kuwa kutokana na sababu hiyo waigizaji wa magari yenye umri huo waliagiza mwaka 2020 na kuingia mwaka 2021 ni wazi kuwa kodi kwenye gari aliloagiza itaongezaka hivyo wakasema hakuna kiwango cha kodi kilichoongezwa kwenye magari.

TRA imesema katika taarifa hiyo kuwa uthaminishaji wa bidhaa hufanyika kwa mujibu wa kifungu cha sheria ya forodha ya Afrika Mashariki ya mwaka 2004 iliyorejewa mwaka 2019 kikisomwa pamoja na jedwali la nne la sheria hiyo.

Binafsi nahisi kupima ubora wa gari kwa kuzingatia miaka ni technologia iliyopitwa na wakati
Haiingii akilini eti mtu aagize gari ndogo (mf: premio ) ya mwaka 2005 lenye kms 30,000 ionekane imechakaa au itachafua mazingira kuliko Premio ya mwaka 2013 iliyo tembea kms 320,000+ ambayo kwa mafundi wanao jua magari vizuri wanajua kuwa Engine ndogo ikifikia hizo kms zaidi ya laki tatu imesha chakaa, na inaweza kutoa moshi kama trekta......
Lakini pia hii yaweza kushawishi watu kuagiza magari chakavu kwa kuangalia mwaka na sio ubora....
 
Komoa komoa tu sasa hadi akili zitukae sawa.Kweli nimeona maana na umuhimu wa wabunge wa upinzani sasa
 
Bongo pagumu sana....
ukienda Botswana,South Africa,Lethoto, Swaziland.....
vijana wanaendesha magari mazuri sana ya kisasa....ie BMW,Benz Jaguar etc....
lkn ukija bongo vijana wengi wanaendesha gari za ajabu ajabu.....Toyota IST,duet....carina,rav 4 Vanguad Noma sana!!
Bongo kwenye vyanzo vingi vya mapato bado tunaminyana kwenye kodi za used vehicles. Huku ni kukosa ubunifu
 
Kuna gari hapa honda CR-V ya 2010, bei yake na usafiri jumla inafika kama mil. 12, ukiingia kwenye kikokotoo cha kodi cha TRA kodi pekee inafika mil. 22. Sasa mtu unajiuliza, huu ubunifu ambao kodi inakuwa mara 2 ya thamani ya bidhaa upo bongo pekee au na kwingineko duniani. Ukiwauliza wanakuja na blah blah za uchakavu, let say gari ya 2010 ambayo imetembea km. 10,000 utasemaje imechakaa zaidi ya gari ya 2015 iliyotembea km. 300,000. Yaani unawezaje kupima uchakavu kwa kuangalia umri wa gari tangu ilipotengenezwa badala ya kuangalia namna gari ilivyotumika. Waache mambo ya ajabu, haya magari kabla ya kusafirishwa yanakaguliwa na kuthibitishwa kwamba yana hali nzuri na bado serikali inaweza kufanya ukaguzi wa kila mwaka kuona kama yanaendelea kukidhi ubora, naona furaha ya watawala imekuwa kuwafanya wananchi waishi maisha magumu. Ndo maana wanajiita watawala na siyo viongozi....shit!
 
Amesema kama uliagiza 2020 lakini gari imefika 2021 basi hapo ushuru unabadirika kutokana miaka toka itengenezwe hiyo gari imeongezeka
Ndo ufafanuzi wa taarifa zinazozagaa kuwa wameongeza ushuru???

Nimekuuliza umeona hiyo taarifa inayozagaa yenyewe?? Ungekua umeiona ungenielezea vizuri kwamba gari ya 2013 ina Kofi ya uchakavu sh ngap mwaka 2020(December) na imeongezekaje kuwa hiyo mpya 2021(January)

Na kodi ya uchakavu ni kwa gari za miaka kumi au zaidi.

Ningeposti hilo jedwali sema nashindwa kuambatanisha picha kwa simu yangu hapa

Hapo ndo ungeona kaongea vitu visivyoeleweka/visivyohusiana na huo ufafanuzi wake
 
Ndo ufafanuzi wa taarifa zinazozagaa kuwa wameongeza ushuru???

Nimekuuliza umeona hiyo taarifa inayozagaa yenyewe?? Ungekua umeiona ungenielezea vizuri kwamba gari ya 2013 ina Kofi ya uchakavu sh ngap mwaka 2020(December) na imeongezekaje kuwa hiyo mpya 2021(January)

Na kodi ya uchakavu ni kwa gari za miaka kumi au zaidi.

Ningeposti hilo jedwali sema nashindwa kuambatanisha picha kwa simu yangu hapa

Hapo ndo ungeona kaongea vitu visivyoeleweka/visivyohusiana na huo ufafanuzi wake
Hiii ?
JamiiForums-1433421304.jpg
 
Bhana kodi imepanda kweli aisee....yani gari niliyotoka agiza mwaka jana december kodi yake imeongezeka kwa Laki 8..
 
Back
Top Bottom