TRA yakusanya Trilioni 22 mwaka wa fedha 2021/22, Nauliza tena Nani kama Samia?

TRA ieleze pia kati ya hayo makusanyo serikali imelipia kiasi gani kupitia wakandarasi walioingiza malighafi za ujenzi wa reli,bwawa la Mwalimu Nyerere,kodi kutokana na manunuzi ya wakandarasi kutokana na fedha ya mkopo wa COVID 19 ambao ulijenga madarasa na vituo vya afya nchi nzima...tunaweza kutoa sifa kama hizi halafu wananchi wasione impact ya makusanyo kwa sababu sehemu kubwa ya fedha imetokana na fedha za serikali yenyewe.
 
Hakuna wa kushindana na Samia mkuu,ameshawaacha midomo wazi..

Mwaka ujao tunataka TRA wakusanye Til.25 yaani til.2 kila mwezi ita make sense na I hope itakuwa hivyo nikiangalia trend ya mwezi Juni.

Kwa makusanyo hayo ni wastani WA Til.1.85 kwa mwezi ambapo ni mbali Sana na kufikia Til.2 kwa mwezi.

Hata hivyo ni mafanikia makubwa kwa Mwaka mmja kutoka wastani WA Til.1.5 hadi Til.1.85 ongezeko la Bil.350 kwa mwezi..
 
Huoni impacts au una shida mahala? Kipi huoni kama impacts?

Bajeti ya Serikali inapopangwa huo inaonyesha makusanyo na wapi zitatumika,kwa hiyo ni wajibu wako kufuatilia kama fedha zilitumika kama ilivyokusudiwa..

Kwangu mimi ni sahihi kwa sababu Kwa mujibu wa Bunge, serikali uliganikiwa kutekeleza bajeti yake kwa 95%..
 
Watwambie kabisa na makusanyo ya miamala wanazokata kama vile kutukomoa ni shiling ngapi na kazi zake maana wanakamua mpaka damu, maana siku hizi kodi zinakusanywa mpaka kwenye vibaraza vya watu, mtu kuchukua tu pesa kwenye ATM na ni eneo la bank utawaona hao kodi mia kidogo.
 
Ukitulia utanielewa ndugu, TRA waseme kwenye ripoti yao kodi imekusanywa kutoka wapi?ununuzi uliofanywa na serikali katika ujenzi wa SGR na Bwawa la Mwalimu na pia ulipaji wa madeni makubwa ya wakandarasi wa hii miradi ya mikakati baada ya kupata mikopo nafuu na uendelezaji wa awamu nyingine mpya za SGR na ujenzi mkubwa uliofanyikq nchi nzima kutokana na fedha za Covid 19 nk vina impact kwenye kiwango cha kodi kilichokusanywa lakini inawezekana tax base imepungua au hata makusqnyo ya kodi za biashara za ndani.kupanda bei kwa bidhaa mbalimbali pia kumeongeza kiwango cha kodi ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta ya nishati na kula...kodi itakayoleta impact itatokana na uwekezaji kqtikq viwandq,utalii,nk...ndiyo maana kuna kipindi huko nyuma kulikuwa na sheria ya kuzuia manunuzi ya serikali kukatwa kodi. Sijui kama unanielewa.
 
Lipa kodi kwa maendeleo yako
 
Mshahara wa mtu ni siri yake we uujue ili iweje? mbonq husemi mshahara wako hapa
Huyu ni mwajiriwa kodi za wananchi ndio zinamlipa mshara, hela ya matibabu,malazi , usafiri na kiinua mgongo akistaafu iweje iwe siri?
 
Huyu ni mwajiriwa kodi za wananchi ndio zinamlipa mshara, hela ya matibabu,malazi , usafiri na kiinua mgongo akistaafu iweje iwe siri?
Mimi sio public figure na sijaajiriwa mimi najilipa kila siku kwa kazi zangu.
 
point kubwa kabisa hii! huwezi kujisifu unakusanya kodi huku miradi mingi imesinzia hizo pesa zinaenda wapi. tujue tuanze kusifia serikali
 
Ukiweka mazongira mazuri ili hata machinga walipe kodi kidogo kwa mwaka..tunaweza kusanya ttrillion 36 kwa mwaka bila hata mtu kuumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…