TRA yampiga faini ya 3,500,000 dereva kisa kapakia tenga 27 za nyanya

TRA yampiga faini ya 3,500,000 dereva kisa kapakia tenga 27 za nyanya

Siku chache zilizopita niliandika kueleza ugandamizwaji unaofanywa na TRA uliomuhusu dereva mmoja wa semi ambae alipigwa faini ya 3,000,000/= kisa kapakia tenga 20 za parachichi na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo kwani mzigo ule haukuhusu ofisi,ilikuwa ile kawaida ya madereva kujiongezea kipato kwa vimizigo vya njiani ambacho kilimponza akapoteza ajira.
Boss wake alifanya vyema pia.
Si jambo la busara sana kumwibia boss wako.
Pia si busara kuziba riziki za dereva guta, bajaji, kenta ama fuso.
 
Enzi hizo, watu walikuwa huru sana kujiongeza. Hazina ikaishiwa hela kabisa. Nakumbuka Walimu wetu walipata shida sana kwenye mishahara. Kunusuru ikabidi "Sur tax" ianzishwe kwenye magari.
Sasa kwenye vyakula tena vinavyoharibika haraka lazima pawe na utaratibu maalum wa kuvishughulikia, wote tunajenga nchi moja, lakini nchi haiwezi kujengwa na watu wenye njaa au afya mbovu, hilo lieleweke kwa uzuri kabisa.
 
Msipende kuchangia kwa mihemko basi.. Mwenye gari anafanya biashara ya usafirishaji hivyo anatakiwa atoe risiti ya mauzo yake ya huduma ya usafiri. Na kwa magari lazima uwe na EFD na iko wazi faini ya kutotoa risiti za EFD ni 3M - 4.5 M so hapo mi naona wamempa nafuu kabisa kama ofisa nakuwa mimi nanyooka na 4.5M.
Kwani asili ya uchawi ni nini? Jiangalie na ujitafakari, hiyo roho uliyonayo si nzuri 😂😂
 
Kwani asili ya uchawi ni nini? Jiangalie na ujitafakari, hiyo roho uliyonayo si nzuri 😂😂
Huyu mwache kama alivyo,ila kwenye utawala huu hakuna atakaebaki salama,hata yeye kama si leo basi kesho,ninaimani siku moja atakumbuka huu mjadala unamaana gani.
Utawala huu unatesa raia kuliko mkoloni.
 
Siku chache zilizopita niliandika kueleza ugandamizwaji unaofanywa na TRA uliomuhusu dereva mmoja wa semi ambae alipigwa faini ya 3,000,000/= kisa kapakia tenga 20 za parachichi na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo kwani mzigo ule haukuhusu ofisi,ilikuwa ile kawaida ya madereva kujiongezea kipato kwa vimizigo vya njiani ambacho kilimponza akapoteza ajira.

Sasa huyu ni muendelezo wa vitimbi vingine kwani dereva mwingine amepigwa faini ya 3,500,000/= kisa kapakia tenga 27 za nyanya na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo. Dereva huyu analazimika kukatwa hii pesa na ofisi kwenye mshara mpaka deni litakapoisha.

Kwakweli kama hizi ndio sheria zilizotungwa kwa ajili ya kutetea wanyonge basi hiki ni kituko.

Hivi mshahara wa Rais ni sh ngapi, mawaziri pesa ngapi, wabunge je? Hawa hawatusikii kwakuwa wao wanalipwa pesa ndefu, hivi dereva mwenye mshahara wa laki tatu kwa mwezi atakatwa hilo deni mpaka lini?

Ushauri wa bure ni kwamba;hii miradi mikubwa ilioanzishwa nchini inasababisha mateso kwa raia,ni bora tukarudi kwenye mgao wa umeme kuliko haya maisha ya karaha tunayoishi sasa.

Kwakweli nachuma dhambi ila kama Mungu anasikia vilio vyetu basi.
Safi sana, hatutaki wababishaji hapa Tanzania.
 
Inakuwa risiti ya bei gani?
Kwa mfano una semi imepakia mahindi junia 300 kutoka simiyu kuja dar,yule mwenye mzigo atakatiwa risiti ya ushuru kila junia tsh 1000 ,sawa na 300,000, hizo anatoa mwenye mzigo na lazima awe na leseni ya kuuza na kusafirisha mazao,anakua anatemb
ea na copy,
Mwenye gari,tuseme makubaliano na mwenye mzigo ni milioni 2 kusafirisha hadi dar,
Hivyo atatia risit ya EFD ya transport, ambayo makato yake ni ya VAT,,about kama tsh laki 3 na ushee,zitakatwa katika hiyo milioni 2 ya transport,,zinazobaki ndo pesa za Transporter
 
.... Si busara wala hekima kuficha elimu ya sheria kwa wahusika ili uwavizie kuwatoza faini! ...
... ndio wanatoa elimu kwa staili hiyo! Wakiitoa kupitia channels au means nyingine haisambai vya kutosha au kufika vizuri kwa walengwa. Kwa njia hii ya "kuumiza" inafika kwa haraka zaidi ndio maana hata sisi tumeweza kuipata kupitia JF.
 
Watendaji wa vijijini siku hizi wana EFD machine?
Tangu lini?
Je ni Wote nchini au wa mijini tu?

Unajua nature ya kazi za dereva wa masafa marefu?

Je ni rahisi kwake kutafuta mtendaji wa kijiji alipo apatiwe risiti?
Mzee,nenda kijiji chochote ndani ndani ukapakie mfano njugumawe,,utashangaa kabla fuso haijajaa mdada huyu hapa na EFD machine,anasubiria hela,yaani haina kukwepa,
Au nasema uongo nduguzanguni..?
 
Sawa huo ushuru wa kulipia elfu 1000 kwa gunia ni kawaida.
Ila wao tra hawakutaka hizo risiti. Walitaka risiti zao.
Kama mzigo unatoka shamba thamani ya hizo gunia unazijuaje? Na mzigo ulikuwa unaenda sokoni
Hiyo risiti aliyopigwa faini,haihusiani na mzigo,,hiyo ni ya Transporter,,yaani mwenye gari kafanya biashara lazima alipe kodi,
Mwenye nyanya analipa ushuru
 
... ndio wanatoa elimu kwa staili hiyo! Wakiitoa kupitia channels au means nyingine haisambai vya kutosha au kufika vizuri kwa walengwa. Kwa njia hii ya "kuumiza" inafika kwa haraka zaidi ndio maana hata sisi tumeweza kuipata kupitia JF.
Duh! Kwa utaratibu huu wa elimu yao hiyo, dereva ameadhibiwa wakati amevunjiwa" haki yake ya kikatiba ya kuhabarishwana kuelimishwa" bila vikwazo!

Si sawa hata kidogo kumnyima raia "haki yake ya kikatiba" wakati huo huo unatunia kunyima haki yake hiyo kumuadhibu.
 
Ni kweli lakini nini kinatathmini ukubwa upi unatosha?

Thamani ya matenga yote yakija sokoni na kuuzwa haizidi 700,000 hii inamaanisha hata 700,0500 ni kubwa.

Sasa kitathmini cha ukubwa wa adhabu ifike 3,500,000 ni kipi?
Faini haihusiani na nyanya,Transporter ndio kapigwa faini
 
Faini zitakuwa nyingi sana kwa sababu watu hawajui kuhusu kodi. Inatakiwa elimu kubwa itolewe kwa watu wote.
 
Hili ni Kati ya masuala tata sana.
Kodi muhimu na kodi hii ipo kisheria.

Lakini upande wa pili wa shilingi kodi hizi kwenye usafiri wa mazao ya chakula utaongeza ugumu wa maisha na kushusha kipato cha wakulima wa mazao ya chakula, matunda na mboga mboga, maana madereva sasa hawatathubutu kubeba mizigo midogo kama hiyo njiani. Mazao yatawaharibikia na masokoni kutakuwa na upungufu wa bidhaa kisha bei zitapanda kama ilivyouzwa 1kg ya vitunguu kwa 10,000/- wakati wa Corona.

Lakini tujiulize, kama mwenye mgahawa anatakiwa atoe risiti ya EFD akiuza kitu cha chini ya 30,000 mfano kahawa cupuccino au juice au kuku nusu au Samosa(sambusa) kwanini mwenye kusafirisha mzigo na kutoza 70,000/- au 100,000/- asitoe risiti ya EFD?

Hapa madereva waongee na matajiri wao watembee na EFD na hii pesa ya mizigo ya juu kwa juu wapewe commission kubwa nje ya mishahara yao ili kuwaongezea kipato na kupunguza ugumu wa maisha.

Au
Njia ya pili ambayo mmiliki wa gari si lazima ahusishwe au ajue gari yake ilibeba mzigo wa juu kwa juu.

Kuwe na maafisa wa TRA ambao si wala rushwa wakikutana na mzigo kama huo wanakata kodi halali (yenye uwiano sahihi) kwa huo mzigo, wanatoa risiti ya EFD na gari inaendelea safari.

Kurahisisha zoezi hili na kuepuka udanganyifu wa madereva kuhusu bei walitoza kusafirisha mizigo inabidi TRA waweke vituo vidogo kama check-points au mfano wa vile vya maliasili barabarani kila Kijiji au umbali flani ambapo hapo wenye mizigo na madereva watapakilia hii mizigo na mbele ya hao afisa wa forodha.

TRA inaweza kuweka hata mawakala kwenye vituo hivi kupunguza gharama za kuajiri watu wengi.
Hakuna haja ya ku- centralize kila kitu.

Hivi vituo pia vinaweza kuwa kama vile masoko ya madini Kila wilaya.
Mkulima kazi yako kutoa mzigo wa mazao shamba na gari ndogo kisha kufikisha kwenye vituo hivi. Iwepo na miundombinu ya kusaidia baadhi ya mazao haya yasiharibike yakisubiria usafiri.

Serikali isihusike kabisa kupanga bei ya usafiri wa hii mizigo, hiyo iwe mapatano ya mwenye mzigo na dereva.

Nafikiri haya ndiyo mawazo yangu ambayo si lazima niwe sahihi.
Hujawahi kufanya biashara acha kujidanya
 
Dereva ni mwizi na mketa hatari, hapo gari likingongana au pindikuwa, bima inakufa na hailipi, na mwenye mali aliyekodisha gari atamdai mzigo wake mwenye gari. Hao madereva kwa uroho wao wanamharibia kazi mwenye gari kwa sababu ya uroho, na hali madereva wanapewa , malipo ya milage.
 
Back
Top Bottom