Trafiki wawili wakamatwa baada ya kunaswa kwenye video wakipokea Rushwa hadharani

Trafiki wawili wakamatwa baada ya kunaswa kwenye video wakipokea Rushwa hadharani

Ila nahisi aliyechukua hiyo video na kuisambaza Sasa hivi anaumia moyoni mwake Kwa kuharibu vibarua vya watu.
Vitu vingine vidogo vidogo ni vya kuacha vipite tu.
Anaumia au anapiga dua asikamatwe maana wakimnasa hamna rangi ataacha kuiona.
 
Hakuna marupurupu wala nini
Ajali haziishi kwa ajili ya watu kama hawa
Dereva hana leseni, matairi mabovu, breaking system hazifanyi kazi
Kila leo watu wanakufa kwa sababu magari hayaangaliwi kwa sababu ya haya majitu yameacha kazi zao na kujifungulia mradi
Naomba msiwatetee hawa kwani wakifanya kazi zao kwa uangalifu hamtaona ndugu zenu wakifa kila leo
Mara Lori limeparamia watu, mara basi limeacha njia yote haya ni kutokuwa waangalifu
Kazi yao si kuangalia magari mabovu ccm na serikali yake ndo wamefeli
 
Hii itawafanya Traffic Police kuwa na Hasira zaidi tu ..Maana hapo ni kupambania familia zao
Hii ndo ile unakutwa na kikosa kidogo mnashndwa kusort out mnaishia kuumizana na 30K juu ya wao kuhofia kuchukuliwa Video..
 
Hakuna trafiki asiyepokea rushwa, wote wakubwa na wadogo wanapokea na kula, kuna huyu dada anayekusanya 2000 kila gari hapo China Plaza, kituo cha Sekondari ya Benjamini Mkapa katikati ya Kariakoo na Karume, karibu na kiwanda cha bia Brewaries kila jumapili, tukutane hapo jumapili tushuhudie pamoja.
Nakuhakikishia haji
 
Serikali inapopandisha Bei fa faini inatengeneza mazingira ya rushwa...upumbavu wa wizara fedha...wangeweka fain elfu tano...au 10 MTU akiona gari yake mbovu anaenda kupigwa kabisa kituoni anatembea...utaratibu huu tunatumia sana wenye gari za mizigo ukiwa unapita barabara ya trafiki wengi...unajipiga faini kila.ukifika kwao unawaambia mshalambwa wanakuacha...ukifika hapo lazima utoe elfu 2 au 5 la sivyo unalimwa 30k.. kuendelea... Kuna wakati nilikuwa na GARI mpya nikawa nakorofishana nao... Wakaandika no ya leseni kwenye note book...Kuna siku nilijichanganya nkakuta nimelimwa faini 2 juu kwa juu...asub wakaja napopaki wakawapa walinzi taarifa mwambieni huyo akijisahau fain itabeti....ndio kuangalia ais3ee...nilihama njia...Sasa kuwarekodi Hawa bila kurekebisha Sheria wataumia watu maana wanasimamia Sheria mbovu na kandamizi...
 

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema askari wawili wa Kikosi cha Usalama Barabarani walioonekana kwenye video wakifanya vitendo ambavyo ni kinyume cha maadili ya Jeshi la Polisi kwa maana ya kupokea rushwa, tayari wamekamatwa na wako mahabusu na hatua za kisheria zitafuata dhidi yao.
Pia, Soma: Hapa ni wapi? Trafiki wadakwa kwenye video wakichukua Rushwa mara kadhaa
Rushwa imetapakaa kila Mahali katika nchi hii ya Tanzania, hakuna kitu cha ajabu hapo. Ni Askari Polisi wachache Sana kupita kiasi ambao ni wasafi, Yaani hawajihusishi na Rushwa Wala vitendo vingine viovu vya uhalifu ama uvunjaji wa Haki za watu.

Kwa uzoefu wangu, kwenye kila penye Kituo cha Polisi jirani ya hicho Kituo lazima kuna Vijiwe vya kupokea rushwa au kuna Mawakala wa kupokea rushwa ili baadaye mzigo huo wa rushwa uweze kufikishwa kwa Askari Polisi anayehusika.
Mathalani, Mawakala ambao mara nyingi Sana hutumika kupokea rushwa za Maaskari Polisi na/au Mahakimu wa Mahakama huwa ni:-
1. Wapiga brashi Viatu ambao vilinge vyao huwa vipo jirani au pembezoni mwa Vituo vya Polisi.
2. Wauza Magazeti (ambao wapo katika vijiwe, fixed location).
3. Wahudumu wa Utoaji wa huduma Stationery au kupiga photocopies waliopo jirani na Vituo vya Polisi au Mahakama.
3. Askari wa Polisi Jamii au Askari Mgambo ambao wapo katika baadhi ya Vituo vya Polisi.
Mara nyingi sana Watu hawa (Polisi Jamii au Mgambo) hutumika kupokea rushwa za Maaskari Polisi na kuwapelejea wale Askari Polisi ambao wana Vyeo vya juu kidogo,
Kwa upande wa Mahakimu, wanaotumika kupokea rushwa zao mara nyingi ni wale Warumishi wa Mahakama wa ngazi za chini au wakati mwingine huwa pia kupitia kwa Mawakili.

Taarifa hii ni kutokana na Utafiti wa kificho Sana uliofanywa kuhusiana na masuala haya.
 
Kwahio mfalme ni askari traffic?
Je, unakumbuka yaliyompata Mwandishi wa Habari za uchunguzi wa ITV mara baada ya kuwaumbua Askari Polisi walipokuwa wakipokea rushwa kwa kuwapiga picha Kama hivi ilivyofanyika kwa hawa Traffic Officer? Je, unakumbuka aliyekuwa RPC Suleiman Kova alimfanya Nini Jerry Muro baada ya tukio hilo?
 
Je, unakumbuka yaliyompata Mwandishi wa Habari za uchunguzi wa ITV mara baada ya kuwaumbua Askari Polisi walipokuwa wakipokea rushwa kwa kuwapiga picha Kama hivi ilivyofanyika kwa hawa Traffic Officer? Je, unakumbuka aliyekuwa RPC Suleiman Kova alimfanya Nini Jerry Muro baada ya tukio hilo?
Hao ni wahalifu kama wahalifu wengine tu. It doesnt make any sense kum vice mtu anayesema ukweli.
 
Hii itawafanya Traffic Police kuwa na Hasira zaidi tu ..Maana hapo ni kupambania familia zao
Hii ndo ile unakutwa na kikosa kidogo mnashndwa kusort out mnaishia kuumizana na 30K juu ya wao kuhofia kuchukuliwa Video..
Hutakiwi kukutwa hata na hiko kikosa kidogo, otherwise gari usitoke nalo.
 
Aisee hii tabia ya kurekodi watu wanapokea elf mbili mnaita rushwa ni hatari sana

Hivi mnajua Rushwa kweli?

Wanaokula rushwa hata wanaonekana kwa macho?

Eyes on small coins,

Mtasema mnaanzia hapa, lakini i can tell you hii mediocrity ni ya level ndogo sana kama taifa
acha tuanze na hawa , wenzao walipiuliwa na watu walitaka kukemea hawa trafiki pamoja na vitengo walihusika kuzuia maandamano ya kukemea , acha waonje joto kias la hiyo adhabu km watachukuliwa kwel
 
Aliyerecord na kusambaza hajafanya poa, hao jamaa wanapiga sana kazi tena kwenye mazingira magumu sana, jua,mvua zao hao..mpaka unawaonea huruma.
Na hawana sehemu ya nyongeza zaidi ya humo barabarani...watu wanapiga mabilioni kila siku na allowances za kutosha...
Wawaache bana..
ww akili yako ndogo sn , hujui wajibu wa trafiki na kichwa chako kibovu unahis kaz ya trafik kuelekeza magari ? unapochukua elf 2 na kuacha roho za watu 50 mpk 80 zipo kweny gar lenye mapunguf hiyo ni kupiga kaz? NDIO KUNA GAZETI LILITANGAZA WATZ WANAONGOZA KWA UJINGA AFRIKA
 
Traffic wa Dar kiboko,wanabeba hadi mikoba!😁.

BTW: Hivi huu ni ushahidi usiotia shaka unaoweza kumtia hatiani mtu kuwa alikuwa anapokea rushwa kunako mahakamani?

Yasiwe yaleyale ya DC Bomboko na kesi ya makahaba Ubungo,mashahidi wa Jamhuri wakaishia kung'ata kucha tu.
hakuna trafiki hapokei rushwa , huu mfumo wa trafiku ni wa kukemea inbid trafiki afanye kaz kwa kuridhika maana alituma maombi akijua majuumu na ujira wake
 
Back
Top Bottom