Roca fella
JF-Expert Member
- May 13, 2023
- 2,077
- 4,152
CCM OYEEEEEE
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Duh ukoo imebidi uingilie kati? Umehisi ndugu yao anafanya uhujumu?Kamati ya Wana Ndugu wamekaa asubuhi ya leo kumuuliza Ndugu yao Bundi kama alifanya hilo tukio.....amekana with evidence
Kwahiyo Kadogosa ametudanganya au ameleta vichwa ambavyo havina specs zilizotakiwa? Maana kama umeme ungezima, tungetegemea automatic switch on kwenda kwenye nishati nyingine, ili safari iendelee.
Dar es Salaam, Tarehe 31 Julai 2024
Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete na kusababisha treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) siku ya tarehe 30 Julai 2024.
Pia soma: Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme
Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system). Hitilafu ilisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku.
Mafundi wa TRC walifanikiwa kutatua changamoto na kurejesha umeme saa 6:30 usiku na treni kuendelea na safari kuelekea Dodoma, na kuwasili Dodoma majira ya saa 7:57 usiku.
Shirika la Reli Tanzania linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
Waongo wamejaa viti vya mbele. Wanakula hela za walipa kodi. Wnatuona wote hatujui isipokuwa waoKwani si walisema train yenyewe, moja ya mabehewa ina power backup system?
USIANDIKE SHUTUMA KUBWA KAMA HII BILA KUWA NA USHAHIDI,TUKIKUOMBA MAHAKAMANI UTASIMAMAA KUTETEA KAULI YAKO?Wakina Shabiby wameanza hujuma
Inawezekana siyo hujuma, labda ni matokeo ya ujinga na uzembe.Kumekucha!
Wameisha anza hujuma zao. Wanafikiri watanzania hawana akili na hawakumbuki kauli zao wanazoziongea mbele ya waandishi wa habari.
Tuliambiwa tren zetu zina mifumo miwili,
1) umeme
2) mafuta
Ukikatika umeme injini inapiga kazi kwa mafuta.
Na walisema haitakuja kutokea umeme ukakosekana kwenye tren hiyo. Ukikosekana maana yake inchi nzima iko gizani.
Sasa tunawauliza kwa nini wasitumie diesel baada ya umeme kukatwa?
Na je wamewalipa fidia abiria kwa hasara waliyoipata?
Hawa wanahujumu mradi kwa makusudi.
Nimecheka sana....Ngedere tu anazuia safari je binadamu akiwa na nia mbaya si ndo inakufa siku mbili tu waongeze ulinzi
Tujiulize hakukuwa na Proactive mechanisms zote kuwa jambo kama hilo linaweza kutokea au tulisubiria matokeo ndiyo tuweke hadhari?..Inawezekana siyo hujuma, labda ni matokeo ya ujinga na uzembe.
Nimejipa wakati nisome michango yote katika mada hii. Huu ndio mchango muhimu kuliko zote nilizo kwisha soma hadi sasa.Shida ni kwamba wanashidwa kufanya uchunguzi wa kina kujua nini kinatokea, kitu kama hichi kikitokea kama china au India muhusika anashughulikiwa kweli kweli
Inavyo elekea hata tatizo lililo sababisha ni la kubuni tu, hawana uhakika. Katika hali ya namna hiyo hawawezi kuwa na "suluhisho la kudumu."Wamepata suluhisho la kudumu au tutegemee kuombwa radhi tu?
Sasa kwa nini wanajichosha kufanya press conferences?Such a waste of time and calories!Inavyo elekea hata tatizo lililo sababisha ni la kubuni tu, hawana uhakika. Katika hali ya namna hiyo hawawezi kuwa na "suluhisho la kudumu."
Ngedere bundi ile fiksiSidhani kama zile waya zinaweza kuchezewa na ndege au hao ngedere sidhani ni waya ngumu harafu zimebana sana na pia zina umeme...
Ni kawaida sio malaika hao. Swala ni kujipangaOohooo tena?