TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete

TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete

View attachment 3057277

TAARIFA KWA UMMA
HITILAFU YA UMEME KATI YA KILOSA NA KIDETE

Dar es Salaam, Tarehe 31 Julai 2024

Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete na kusababisha treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) siku ya tarehe 30 Julai 2024.

Pia soma: Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme

Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system). Hitilafu ilisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku.

Mafundi wa TRC walifanikiwa kutatua changamoto na kurejesha umeme saa 6:30 usiku na treni kuendelea na safari kuelekea Dodoma, na kuwasili Dodoma majira ya saa 7:57 usiku.
Shirika la Reli Tanzania linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
Tunawambia hapa.. ilindeni hiyo SGR....
Wachawi washaingia kazini. Take Care..
 
TRC mmepata changamoto ila mna la kujifunza , sasa kaeni mkao wa kibiashara kuhakikisha umeme upo mda wote pamoja na ulinzi wa miundombinu .

Hujuma zipo kweli.
Kwenye ulinzi wawachukue Suma jkt wapambane na hao ngedere pori.......Hapa mfano tungekuwa na ugomvi na majirani zetu kama Kenya ama Uganda tungewasingizia wao ila hatuna ugomvi nao tunabakia kuwalaumu Ngedere
 
Sawa, lakini to me, kulitakiwa kuwe na battery banks ambazo zinakuwa charged all the time na rectifiers wakati umeme upo. Umeme ukikatika, the DC current zitoke kwenye batteries, ziwe inverted to AC then zikaendeshe machines zinazoendeshwa na hizo overhead catenary system. Ni kama hiyo desktop computer yako na UPS uliyonayo..!!
Hatukutakiwa kuishia kwenye lighting system pekee..!!
Ndomaana india wana treni za umeme ila nyuma ya locomotive kuna dizeli generator, naamini umeshajua kwa nini wameweka.
20240731_095839.jpg

20240731_095855.jpg
20240731_095910.jpg
20240731_095945.jpg
 
Kimbinyiko, shabiby, BM, Abood n.k haya mabasi ni ya vigogo wakubwa waliowahi shika madaraka makubwa ya nchi kuanzia spika, marais, wafanyabiashara wakubwa weupe kwa weusi mabasi haya na mengine yanayotamba ktk safari za dsm, moro, dom ni hatari sana kwa ustawi wa sgr hasa kwa safari za dsm moro hadi dom
 
Kidete mpk kilosa ni km 59km.
Sasa train kama lina battery kwa speed ya 160km/h linamaliza hizo km chini ya dkk 23 hivi.
Sasa battery linashidwa kitumza umeme wa dkk 23 kweli.
 
😀 😀 😀sababu umeme wa kuendesha ile engine ni kubwa sanaa huwezi uzalisha kwa kutegemea betri labda waweke na engine ya kutumia mafuta kama back up.
Hayana battery yale , battery zilizopo ni kuweka mabehewa taa isizime
 
Kwenye ulinzi wawachukue Suma jkt wapambane na hao ngedere pori.......Hapa mfano tungekuwa na ugomvi na majirani zetu kama Kenya ama Uganda tungewasingizia wao ila hatuna ugomvi nao tunabakia kuwalaumu Ngedere
Acheni ubinafsii,hivi aliyewafata bundi na ngedere ni nani
Waliyojenga reli ndiyo wamewafata hao maporini huko
Ambako ndiyo nyumbani kwao
Sasa muwafukuze waende wapi
Acheni ubinafsi nyie wanadam

Ova
 
View attachment 3057277

TAARIFA KWA UMMA
HITILAFU YA UMEME KATI YA KILOSA NA KIDETE

Dar es Salaam, Tarehe 31 Julai 2024

Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kufuatia hitilafu ya umeme iliyojitokeza kati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete na kusababisha treni ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili (2) siku ya tarehe 30 Julai 2024.

Pia soma: Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme

Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system). Hitilafu ilisababisha umeme kukatika kituo cha kupoozea umeme namba 7 (Godegode) ambayo kitaalamu hujulikana kama (Instanteneous Overcurrent Protection Trip) majira ya saa 4:20 usiku.

Mafundi wa TRC walifanikiwa kutatua changamoto na kurejesha umeme saa 6:30 usiku na treni kuendelea na safari kuelekea Dodoma, na kuwasili Dodoma majira ya saa 7:57 usiku.
Shirika la Reli Tanzania linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
Bundi wanasingiziwa tu
Kwani kipande cha Dar na Morogoro hawapo?
 
Kwenye ulinzi wawachukue Suma jkt wapambane na hao ngedere pori.......Hapa mfano tungekuwa na ugomvi na majirani zetu kama Kenya ama Uganda tungewasingizia wao ila hatuna ugomvi nao tunabakia kuwalaumu Ngedere
Hivi ngedere wanazurulaga usiku?
 
Waende wapi usiku wale wanatembea wakiwa wanaona usiku ni kujificha tu mara chache sana labda eneo lao liwe na uvamizi ndio utawaona kuhama usiku..
Sasa ngedere wamehusikaje kwenye uharibifu unaosemwa? Na kama wamedanganya kwa ngedere, nina sababu gani ya kuamini kuwa bundi ndo wamesababisha uharibifu?

1. Je waliwakuta bundi wamefia kwenye nyaya za umeme?
2. Wamewakuta ngedere wamefia kwenye nyaya za umeme?
 
Back
Top Bottom