Treni ya kwanza ya abiria kutoka Dar es Salaam yawasili Moshi ikiwa na abiria 294, ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM

Treni ya kwanza ya abiria kutoka Dar es Salaam yawasili Moshi ikiwa na abiria 294, ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM

Mabehewa 20 × abiria 80 = abiria 1600
Capacity 1600 - waliosafiri 294 = loss (1306 × nauli per person)

Tusikate tamaa tutangulize uzalendo tusafiri kwa reli yetu hata kama ni narrow gauge
These numbers are so scaring! I hope TRC watafanyia kazi (wanajua wanachofanya!). Tuwape muda.

Muhimu tu tufike mahali tuache kuchanganya kanuni za biashara na siasa.
 
Treni ya kwanza ya abiria kutoka Dsm imewasili mjini Moshi saa 5 asubuhi na kupokelewa na maelfu ya wakazi wa Moshi.

Treni hiyo imewasili ikiwa na abiria 294 ambao wameipongeza serikali kwa kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM baada ya usafiri huo kusimama kwa takribani miaka 21. Pia abiria wamesema usafiri wa treni ni wa uhakika na hakuna mambo ya kuchimba dawa au kula magengeni kama ilivyo kwenye mabasi.

Baadhi ya abiria wameomba kwa kipindi hiki cha sikukuu wawekewe miti ya Krismas na zile taa zake kwenye kila behewa.

Source ITV habari!

Kwani kila kitu ni utekelezaji wa ilani? Haya kesho kukicha andika kwamba jumapili ya leo kumekucha ikiwa ni utekelezaji wa ilani. Mbona hii ni too much, kwani haya si yanafanyika kwa fedha za wananchi, mbona mnayafanyahaya kama ni fadhira vile. Huu nao ni upunguani
 
Usisahau ni narrow gauge rail (reli nyembamba), haiwezi kwenda kwa kasi, mpaka reli iwe pana na axel za mabehewa yote yabadilishwe na mengi mengine.

Hata kwa sasa mabasi yanachukua zaidi ya masaa 10
Sio kweli apo kwenye mabasi unadanganya..
 
Tehe tehe,pinga pinga hamkosi la kusema
Treni ipo fully booked mpaka 31 dec
Hakuna mchagga atakusikiliza wewe wakati anafika moshi kwa 15,000
Waendao moshi miezi ya december ilikua ni kilio na kusaga meno,hayo masaa ulioyataja ndio walikua wanayatumia kulala ubungo kusubiri basi lije halafu nauli ilikua 90,000
Kula "like" mkuu
 
Treni ya kwanza ya abiria kutoka Dsm imewasili mjini Moshi saa 5 asubuhi na kupokelewa na maelfu ya wakazi wa Moshi.

Treni hiyo imewasili ikiwa na abiria 294 ambao wameipongeza serikali kwa kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM baada ya usafiri huo kusimama kwa takribani miaka 21. Pia abiria wamesema usafiri wa treni ni wa uhakika na hakuna mambo ya kuchimba dawa au kula magengeni kama ilivyo kwenye mabasi.

Baadhi ya abiria wameomba kwa kipindi hiki cha sikukuu wawekewe miti ya Krismas na zile taa zake kwenye kila behewa.

Source ITV habari!
Unasafiri Siku 2 kutoka Dar hadi Moshi, safari ya Masaa 8???🤣🤣
 
Moja kati ya faida ya upinzani...kama upinzani ingekua haujakomaa Arusha na Moshi hii reli isingelifufuliwa.
Serikali ya ccm inaumiza kichwa wafanye nn ili wapiga kura wabadilishe mwelekeo kwenye chaguzi zijazo..Mwisho wa siku watu wanapata maendeleo.

Action and Reaction are equal and opposite.

NOTE; MOSHI NA ARUSHA ENDELEENI KUCHAGUA UPINZANI MUPATE MAENDELEO.
Vipi kuhusu Dar-Dodoma-Tabora-Isaka ambao reli yao imeboreshwa sambamba na hii ya Dar-Moshi,
Wachague upande gani?
 
This is good news, haya ndio maendeleo ya huduma tunayoyazungumza.
P
Mkuu naomba elimu kidogo!
Hivi CCM ndiyo inatekeleza Ilani au Serikali inatekeleza majukumu yake?
Je,unaweza kutekeleza Ilani bila kua na fedha?
Je ,CCM inavyanzo vipi vya kupata pesa ya kutekeleza ayo tunayo ambiwa?
Mwisho,uoni kua huu ni ulaghai,uongo na uhuni kutumia pesa za watanzania alafu mwisho kujinadi kua unatekeleza Ilani ya chama?
 
Back
Top Bottom