Trilioni 1.5 Bwawa la Nyerere limepotelea wapi

Kuruhusu maji kujaa kwenye shimo na geti la kuzuia maji hivi navyo tunaambiwa ni historia so lazima watu washuhudie so you don't see one of movies!.
I think it's s milestone which deserves President's attention. We all know the challenges that humongous project faces.
 
Si mpaka, hayo maji yatatoka wapi? Kuna wajinga humu wsnasema yatatoka mto Kilombero, hawa ni waliotoroka shule ambao hawajui unakotoka unaitwaje na unakoishia unaitwaje. Mito mapacha Ruaha siku hizi inatiririsha robo ya maji iliyokuwa ikitiririsha ndiyo sababu siku hizi hatusikii mafuriko mto Rufiji ambayo yalisababisha daraja la Mkapa kujengwa kwa upana uliopo.
Pesa zilizotumika kujenga bwawa la Mwalimu zingetumika kujenga mitambo ya umemejoto, umemeupepo na umemejua kwani vyanzo hivi vipo na vitakuwepo kwani havikabiliwi na uharibifu wa mazingira, umeme wa mabwawa umepitwa na wakati kama ambavyo tunashuhudia bwawa la Kariba(Mosiotunya)sic.
 
Sawa

Waahidi pia Kuwa mgao wa Umeme utakuwa historia!

Sio wanajaza maji tu halafu mambo ya Umeme kuzima kama kibatari yanabaki pale pale!
UtaambiwA "kunbe lile bwawa limetoboka kwa mbele hivyo maji hayakai yanaingia yanatoka"
Ataulizwa Mwigulu "nasema uongo ndg yangu?"
Mwigulu atajibu" Mtaalamu dokta mwenyewe anajua litajaa tu hivyohivyo.
Umeme ukikatika hamtawasha vibatari utarudi tu.
 
Yeye ndiye aliyeuweka kwenye Ilani 2015? Aliyefanya upembuzi yakinifu no nani? Aliyeanza kujenga nani? Aliyekamilisha nani? Ndio maana halisi ya kujenga nyumba moja.
Nionyeshe ilani ya 2015 inayosema watajenga bwawa la mwalimu Nyerere. Piga picha huo ukurasa ulete hapa.
 
Mkuu ni chuki tu za watu saiv wanahamisha magoli
 
Ulimsikiliza naibu Waziri wa Nishati? Msiwe wakurupukaji bado Serikali na huyo Mkandarasi wanajadiliana hawafikia muafaka maana Mkandarasi ana madai yake na contractor ana madai yake.
 
Abonyeze tu kukaa lisaa bila umeme ni hasara kubwa sana.
Msisahau kwamba kuanza kuzalisha Umeme haimaanishi umeme kuklacha kukatika labda kwa wale ambao watakuwa wameputiwa na njia mpya za usambazaji Ila wa zamani majanga yapo pale pale.
 
Najua mmeumia sana hamkutarajia angeweza!! Punguzeni chuki sukuma Gang Kila mtu anaweza fanya Kila kitu akipewa nafasi unlike mnavyoamini kuwa ni JPM pekee!!
Mbona hapo unaeumia kama ni wewe?

Mdau kasema waahidi pia kwamba mgao itakuwa historia siyo kujaza maji alafu mgao unabaki palepale!

Hilo ni tamanio la kila mtz hata nyie msoga gang naamini mnatamani iwe hivyo.
 
Project za JPM ndio zipi? Kwani alipotoa Hela za mkopo wa COVID 19 kujenga vituo vya afya na mashule ilikua ni project ya JPM?

Vipi mikataba ya kuchimba gesi huko Lindi?

Hata JPM alikuta Kinyerezi 2, Airport, blueprint za SGR, Mradi wa ziwa Victoria, Mwendo Kasi akaendeleza ila hakuna siku mlisema anafanya miradi ya JK!!

Miradi ipo kwenye mpango wa taifa wa miaka 5 so whether awe Samia au mwingine atapita hapo hapo Wala hakuna mmiliki wa miradi hiyo kama individual.
 
Watu mnasahau sana yaani.

Wakati ule anatumia hizo hizo fedha kuanza mamiradi makubwa kama hayo mnayokwenda kuzindua ulikuwa unaongelea chinichini anatumia fedha vibaya, leo unashadihisha kwa kusema miradi ya taifa siyo ya mtu, daah ... acha tuone panapovuja!.
 
Huelewi miradi almost yote ipo kwenye mpango wa taifa mfano kwa dar Kuna kipengele Cha decongestion dar es salaam ikazaa DMDP so mwendokasi, vivuko, flyovers zote zilikua kwenye master plan. Sasa inashangaza alipoingia JPM ikageuzwa kuwa ni "miradi yake" eti ubunifu wake!!

So whether inaharibu Hela or not hiyo ni debate tofauti. Nachoongelea miradi yote ipo kwenye mpango wa taifa so hata Mama Samia akistaafu Bado Kinyerezi 3 itajengwa, Barabara njia 8 to Moro itajengwa n.k.

So punguzeni kumtukuza JPM
 
HAPANA, mkuu napinga hakuna kumbukukumbu yoyote na sehemu yoyote jeshi la mtu mmoja aliwahi sema ni miradi yake, waliosema yake ni nyie mliomuona devil, sababu alikuwa mwenye uthubutu.

Mzazi kama una mipango endelevu ya family yako miaka nenda rudi huitekelezi, mke anakupiga chini anapata bwana mwingine mwenye uthubutu wewe unakuja kusema mwanamke kauza mipango yako, NO.

Ukweli alikuwa na uthubutu hasa na atabakinkiwa hivyo hata kama kuna mabaya aliyofanya but hukumu zetu ni midomoni tu but siri inabaki kwa sehemu moja tu.
 
Kwani JK hakufanya miradi Bomba la gesi, Barabara kuunganisha almost mikoa yote, Shule za kata Kila kona, Mwendokasi, Vivuko, kupanua airport, umeme wa Kinyerezi, Madaraja kma malagarasi n.k Sasa hayo yote sio miradi? Ila alipoingia JPM Kila anachofanya nyie mkawa mnasema ni ubunifu wake mara ameijenga as if JK hakujenga kitu!!!

Ndio nakuelewesha hapa kwamba miradi ipo kwenye mpango wa taifa sio maamuzi ya JPM au ubunifu wake. Pita YouTube uone Kila video ya Samia akizindua mradi utasikia "wa JPM huo anzisha Yako".... Mara "Huna ubunifu unaendeleza ya JPM Bado". Hii unaonyesha how white washed akili zetu zilivyo baada ya propaganda za yule Mbaba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…