TTCL ina deni la bilioni 403 ilhali mtaji bilioni 243

TTCL ina deni la bilioni 403 ilhali mtaji bilioni 243

Tulipokuwa tunasema serikali ya Magufuli ilikuwa inaendeshwa kwa kupika data, wapambe wake walikua wanateka watu wanaosema ukweli. Wajinga walipokuwa wanaona yale maigizo, walikuwa wanasema tuna bonge la rais maana mashirika ya umma yamefufuka. Ile sheria ya takwimu kuwa ni lazima uzipate serikalini, lengo lake ilikuwa ni kuzuia watu kujua ukweli ili watawaliwe kama makondoo.

Mifuko ya jamii inadai zaidi ya shilingi 4.t+, na hizo pesa zote zimechotwa kihuni ili kwenda kwenye white elephant projects ili kusaka political millage. Nenda sasa kaangalie wakuu wa hayo mashirika walivyo na mapato makubwa, huwa wanufaika wakipata tabu za ajabu kwenye madai yao .
ati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imesema Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limelemewa na deni la Sh403 bilioni ilhali mtaji ilionao ni wa Sh243.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Japhet Hasunga amesema hayo jana Jumatano Oktoba 20, 2021 baada ya kuipitia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2019/20 ambapo amesema wamebaini kuna viashiria katika Shirika hilo kutofanya vizuri kwakuwa lina mtaji hasi wa Sh132 bilioni na madeni makubwa kuliko mtaji wake.

“Hicho ni kiashiria kuwa bado shirika haliendi vizuri. Shirika letu linalipa hadi kodi lakini mapato yao hayajaingizwa katika vitabu vyao,” amesema Hasunga.

=====

Pamoja na nia njema ya JPM, mashirika ya umma yamekuwa yanakula pato la Taifa bila kuleta tija. Tubaki na Tanesco yenye maslahi mapana ya Taifa, haya mengine tukihitaji uzalendo tuwape wafanyabiashara wazawa wajaribu bahati yao.

TTCL ndio ina mkongo wa Taifa wa Data, pamoja na advantage hiyo kibiashara wameshindwa kabisa kutawala soko la internet, yaani mwingine ananunua kutoka kwao halafu anawagaragaza sokoni, tumeshindwa.
 
Hii ni janja ya kutaka kuliuza tena hilo shirika...PAC inajua wazi TTCL ilikopa kuwalipa wawekezaji feki na likamilikwa na serikali kwa asilimia 100...Hilo deni ni la serikali kutokana na makosa ya serikali yenyewe awamu ya nne kulibinafsisha kwa mkataba mbovu.ukiionsoa hilo deni TTCL linatengeneza faida na gawio juu...Hakuna kitu kibaya kama serikali itaiachia TTCL tena kwenye mikono ya wezi .Serikali ichukue deni lake
 
Sasa ni wazi ile pressure ya mwaka 2015 kuhusu kulipora shirika la umma inarudi kwa kasi kwa kutoa taarifa kuonyesha TTCL ni mufilisi ilhali ikijua madhara ya kuingia mkataba mbovu na wahindi na uamuzi wa kuwaondoa kwa maslahi ya Taifa uliigharimu Shirika fedha nyingi.

Wahindi waliacha mtaji wa bilioni 97 na madeni ya zaidi ya bilioni 300 na hapo walihitaji kulipwa walipoondolewa kutokana na mkataba mibovu. Serikali iwajibike kuchukua hili deni na wahusika wote waliokuwa kamati ya bunge 2014 na watumishi wa serikali walioshiriki wachukuliwe hatua. TTCL linafanya vizuri na linatengeneza faida.
 
Wakuu TTCL Walitoa Gawio,
Leo wanasema wana deni kubwa lisilolipika!

Kwanini hawakusema ukweli toka mwanzo?

Au ndio Unafiki Wa Viongozi Wetu Wa Taasisi za Imma Kujipendekeza Kwa Wanasiasa?
Screenshot_20211022-110247.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zilikuwa mojawapo ya chai za mwendazake mbele ya macamera, hamna hela yeyote waliyotoa! Jamaa alidanganya vitu vingi sana, ila cha kushangaza hadi leo hii bado kuna watu wanaamini aliyokuwa anayazungumza
 
ni sawa maana sijaona kama ttcl wana make business yoyote ile kwenye comminication industry
 
ni sawa maana sijaona kama ttcl wana make business yoyote ile kwenye comminication industry
Sijui kama umeelewa hoja ya mleta thread au uccm umekula ubongo wako. Hoja ni kwamba ttcl wakati WA ngosha walikuwa wanatoa gawio lakini Leo wanadai Wana deni lisilolipika. HATA atcl hivyohivyo lakini kumbe zilikuwa mbwembwe.
Hakuna shirika lolote la serikali lililowahi kufanya vzuri Zaidi ya kubebesha mzgo watanzania.

Maccm must go to hell.
 
Back
Top Bottom