Tuacheni unafiki, Le Mutuz alikuwa ni mtu wa ovyo na mfano mbovu kwa vijana

Tuacheni unafiki, Le Mutuz alikuwa ni mtu wa ovyo na mfano mbovu kwa vijana

kwa hyo vice versa ya hiyo orodha ya hayo uliomtuhumu nayo ndo unataka vijana waishi hivo
 
Usimuhukumu mtu bila kujua,siku nikiweka Siri ya familia ya Mzee malecrla hapa hata wewe ungekuwa zaidi ya lemutuz.
Lemutus alikuwa na msongo wa mawazo,alijua tu atakufa siku si nyingi
Kwa hiyo mtu akiwa na msongo wa mawazo ndio aishi kihuni?
Okay, marehemu alikuwa na msongo wa mawazo, sasa nyinyi mliojuwa hayo mliwezaje kumsaidia?

Le mutuz alikuwa mtu wa ovyo, vijana msiige maisha yake.
 
Angalau moja ya tuhuma naweza kumtetea. Alikuwa hanywi pombe kabisa. Hivyo hata mengine uliyondika yanaweza kuwa wrong!
Na mimi nimestuka kuona anasema alikuwa anakunywa pombe, hakuwa anakunywa pombe kabisa kabisa...Maisha ya public yalikuwa kinyume kabisa na the person, William wa a very respectiful person...Mungu amrehemu!
 
Na mimi nimestuka kuona anasema alikuwa anakunywa pombe, hakuwa anakunywa pombe kabisa kabisa...Maisha ya public yalikuwa kinyume kabisa na the person, William wa a very respectiful person...Mungu amrehemu!
Karibu watu wote tumemfahamu marehemu kupitia mitandao kama mponda starehe na wakati wote marehemu aliona hayo ndio sifa na ufahari. Mengine binafsi (mema na mazuri) aliyokuwa nayo marehemu hakutaka sana tuyajue na hatuna sababu ya kuyasema sasa wakati hayupo. Sisi tunaonya tu, vijana wasiige maisha ya marehemu, maana yalikuwa ni maisha ya ovyo kupindukia.
 
Acha nichambue kwa ufupi tabia za marehemu ulizoorodhesha:-


1. Mpenda sifa popote.
Hii ni hulka ya kila binadamu kwa wakati wake na nafasi yake kwa hiyo hoja yako hapa haina mashiko

2. Mpenda pombe.
Le Mutuz hakuwa mlevi wa pombe na sijawahi kumuona akinywa pombe naye pia alishasema mara nyingi kuwa hatumii pombe wala sigara

3. Mpenda umalaya.
Le Mutuz hakuwa malaya kama unavyofikiria ila alikuwa na hulka ya kujirusha na wanawake, kupiga picha n.k ila sio kuwalala. Alikuwa na wanawake lakini kwa level ya kumuita malaya.

4. Mpenda maisha ya kujirusha na kuponda raha.
Hii tabia alikuwa nayo na naichukulia kama tabia za watu wengine tu wanavyopenda kuride pikipiki, kuendesha magari, kujenga majumba mazuri n.k. No offense at all.

5. Mpenda kujipendekeza kwa watu maarufu (chawa)
Hii tabia alikuwa nayo lakini sio kosa kujipendekeza kwa mtu ikiwa huvunji sheria.

Yote kwa yote marehemu hasemwi vibaya, tuache apumzike.
 
Back
Top Bottom