Tuacheni unafiki, Le Mutuz alikuwa ni mtu wa ovyo na mfano mbovu kwa vijana

Tuacheni unafiki, Le Mutuz alikuwa ni mtu wa ovyo na mfano mbovu kwa vijana

Kuna mmoja alikuja kuwa kiongozi mkubwa nchini, lakini alipokuwa in 40s -50s alikuwa mteja mzuri sana Ohio Street; je na yeye unamweka kwenye kundi la watu wa ovyo sana?
Kama mtu alipenda umalaya na kujisifia au kuona ufahari kufanya umalaya, kwanini tusimseme?
Kwanini tusionye vijana wasije kuiga tabia zake?
 
Usimuhukumu mtu bila kujua,siku nikiweka Siri ya familia ya Mzee malecrla hapa hata wewe ungekuwa zaidi ya lemutuz.
Lemutus alikuwa na msongo wa mawazo,alijua tu atakufa siku si nyingi
Mkuu tuwejee plsss
 
Acha nichambue kwa ufupi tabia za marehemu ulizoorodhesha:-


1. Mpenda sifa popote.
Hii ni hulka ya kila binadamu kwa wakati wake na nafasi yake kwa hiyo hoja yako hapa haina mashiko

2. Mpenda pombe.
Le Mutuz hakuwa mlevi wa pombe na sijawahi kumuona akinywa pombe naye pia alishasema mara nyingi kuwa hatumii pombe wala sigara

3. Mpenda umalaya.
Le Mutuz hakuwa malaya kama unavyofikiria ila alikuwa na hulka ya kujirusha na wanawake, kupiga picha n.k ila sio kuwalala. Alikuwa na wanawake lakini kwa level ya kumuita malaya.

4. Mpenda maisha ya kujirusha na kuponda raha.
Hii tabia alikuwa nayo na naichukulia kama tabia za watu wengine tu wanavyopenda kuride pikipiki, kuendesha magari, kujenga majumba mazuri n.k. No offense at all.

5. Mpenda kujipendekeza kwa watu maarufu (chawa)
Hii tabia alikuwa nayo lakini sio kosa kujipendekeza kwa mtu ikiwa huvunji sheria.

Yote kwa yote marehemu hasemwi vibaya, tuache apumzike.
Hapo namba nne mara nyingi zile vyakula na hotel yalikuwa matangazo ya biashara, aliwahi kuniambia yeye mwenyewe. Ndugu yangu alimlipa laki Tano kwa tangazooja la chakula na hiyo ilikuwa 2019
 
Huu ndio ukweli halisi. Leo mutuz alikuwa ni mshenzi mwenye umaarufu. Huyu ni chawa mkongwe, na kwa muda mwingi aliishi kwa kujikomba na kujifanya mjuaji. Alikuwa ni mfitini sana.
Naunga mkono hoja

Mhuni lazima achanwe tu hata kama kafa. Ndiyo maana mm namchana dikteta jiwe mpk kesho na mpk siku yangu ya mwisho
 
Kwanza, ninapenda kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, washikaji na wanaJF walioguswa na kifo cha William Malecella. Mungu awape faraja katika kipindi hichi kigumu cha majonzi.

Sasa, twende moja kwa moia kwenye mada, kupitia mada hii, bila kuficha wala kumumunya maneno, William Malecela (Le mutuz) alijulikana na kufahamika zaidi kama mtu wa ovyo kwa sifa hizi (sifa ambazo alikuwa akijivunia nazo hadharani mitandaoni na mitaani);

1. Mpenda sifa popote.
2. Mpenda pombe.
3. Mpenda umalaya.
4. Mpenda maisha ya kujirusha na kuponda raha.
5. Mpenda kujipendekeza kwa watu maarufu (chawa)

Le Mutuz japokuwa alikuwa na umri wa zaidi ya miaka 50, akijaliwa kuwa na watoto, akipambana kwa namna mbalimbali kutafuta kipato, huku akitokea kwenye familia ya mzee Malecela yenye heshima kubwa sana kisiasa na kijamii ndani na nje ya Tanzania, lakini mienendo na tabia za Le mutuz zilikuwa zenye kutia aibu na kinyaa, akiishi kama kijana aliyepevuka juzi, aliyekosa malezi yoyote ya kijamii na kidini.

Japokuwa hayo yalikuwa ni maisha yake binafsi (sio busara sana kuyahukumu) lakini ni vyema kusema ukweli na kuweka angalizo muhimu kwa vijana ambao ndio wamejaa mtandaoni kuwa makini na kukwepa kuiga au kujifunza kupitia maisha binafsi ya Le mutuz ambayo yalijaa anasa na uchafu mwingi.

UKWELI USEMWE KIKAMILIFU.
Hapo no 4 ,alimpitia mkeo nini?
 
Alikuwa hakubaliani na uzee. Yaani kama kuna kitu kilikuwa kinamfedhehesha kwenye maisha yake, basi ni umri mkubwa aliokuwa nao.
Tukiwafata ndugu zako na wale wanaokujua vizuri tukawauliza kuhusu wewe, watasema unaishi kama malaika? Au kwasababu haufahamiki basi unapata mafasi ya kufungua hilo kopo lako juu ya maisha ya watu wengine?

Ushenzi kabisa huu, aliyekuzaa kapata hasara sana.
 
Back
Top Bottom