Tufanye nini na hizi clip zinazopotosha Historia ya Tanzania?

Tufanye nini na hizi clip zinazopotosha Historia ya Tanzania?

Stux...
Uislamu umewatisha wengi katika uandishi wa historia ya uhuru wa Tanganyika.

Katika kitabu alichohariri John Iliffe kuna sura kaandika: Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114.

Katika kitabu hiki Kleist Sykes ananukuliwa akisema katika historia ya maisha yake na ndiyo historia ya kuundwa kwa African Asociation 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika !933 kuwa waasisi wangi wa AA walikuwa Waislam kwa kuwa Wakristo walikuwa wakionywa na kanisa wasijihusishe na siasa.

Unaniuliza kama Abdul Sykes alisukumwa na Uislam kugombania uhuru wa Tanganyika.

Swali lako lingekuwa hivi: ''Je, baba yake Abdul, Mzee Kleist alisukumwa na Uislam kuasisi AA na kisha Al Jamiatul Islamiyya?''

Wakati wazalendo wa Southern Province Suleiman Masudi Mnonji, Salum Mpunga na Yusuf Chembera wanaunda TANU Lindi wakajikuta wako Waislam watupu kwa sababu Wamishionari kutoka Peramiho walikuwa wanawatisha waumini wao kujiweka mbali na TANU wakidai kuwa TANU ilikuwa inatayarisha vita vingine vya Maji Maji dhidi ya Waingereza.

Hiki ni kisa cha kusisimua nimekieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Si mimi niliyelazimisha Uislam uwe mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa nini kiongozi wa juu kabisa wa Waislam Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru akiuza kadi za TANU misikitini wakati Kadinali Rugambwa hakuonekana popote katika harakati hizi?

Hizi ni changamoto za ukoloni.

Yapo mengi katika ''Islam as a field of enquiry'' tunayoweza kujadili.

Hapo ndipo nilipochukua ukurasa mmoja na kufanya utafiti kutaka kujua kwa nini ilikuwa hivi?

Hivi ndivyo nilivyojua kwa nini Uislam unawatisha watafiti wengi katika historia ya Tanganyika.

Wewe ukiwa mmoja wa hao.

Bado hakuna uhusiano wa dini na uhuru wa Tanganyika ni kulazimisha tu kuwa Uislamu ndiyo ulileta uhuru.

Ni hoja dhaifu sana ambazo kwa karne hii kuzitetea ni kupoteza muda. J K Nyerere alitengeneza misingi mizuri ya Taifa kwa kuondoa feelings za kikabila na kidini.

Wacha hizi utopia, hazina maana
 
Bado hakuna uhusiano wa dini na uhuru wa Tanganyika ni kulazimisha tu kuwa Uoslamu ndiyo ulileta uhuru.

Ni hoja dhaifu sana ambazo kwa karne hii kuziztetea ni kupiteza muda. J K Nyerere alitengeneza misingi mizuri ya Taifa kwa kuondoa feelings za kikabila na kidini.

Wacha hizi utopia, hazina maana
Stux...
Mimi kawaida yangu ni kusomesha historia hii kwa kueleza niyajuayo kwa ushahidi.

Umepata kuona picha yeyote Nyerere kapiga akiwa na viongozi wa kanisa wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika?

Mimi si mtu wa kubishana.

Kwanza nakusihi tusimwingize Nyerere katika suala la dini.

Hapana haja.
Unataka kujadili kitu usichokijua.

Ila ukipenda kujua msome Bergen (1981), Sivalon (1992) na Njozi (2002).

Rejea zote hizi zipo katika uzi huu nimeziweka na kueleza umuhimu wa vitabu hivyo.

Nimejizuia kuweka paper yangu "Islam and Politics in Tanzania," (1989) ambayo ipo hapa ikiwa unataka kulijua somo hili.

Paper hii inatengeneza Part Three "Conspiracy Against Islam," katika kitabu changu: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," Minerva Press London 1989.

Tanganyika haikupata kuwa na tatizo la ukabila.

Tatizo lililokuwa toka ukoloni ni kubaguliwa Waislam na wakoloni na baada ya uhuru kubaguliwa na serikali huru ya Tanganyika.

Ushahidi upo.
Soma rejea hizo utajua.

Wasomi wakubwa waliosimama kunipinga wote waliamua kukaa kimya hawakurejea baada ya kusoma rejea hizo.
 
Dudu...
Historia ya uhuru wa Tanganyika na historia ya Nyerere katika harakati hizo ni changamoto kubwa kwa wasomi na wanahistoria wetu.

Siwalaumu.

Inahitaji mtu shujaa kweli kweli kueleza historia hii kwa ukweli wake unaostahili.

Unaelezaje mchango wa Waislam maarufu waliounda African Association 1929 lakini wamefutwa katika historia ya TANU?

Unaelezaje kupigwa marufuku na serikali EAMWS na kuundwa BAKWATA wakati ilikuwa inajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968?

Unajibu nini utakapoulizwa nini ilikuwa nafasi ya Julius Nyerere katika matatizo yote haya?

Nimeandika kitabu na yote haya nimeyaeleza kama yalivyostahili kuelezwa.

Kitabu hiki naamini unakijua au umepata kukisikia kimebadili si historia ya uhuru wa Tanganyika na TANU bali hata historia ya Julius Nyerere.

Kitabu kinakwenda toleo la tano toka kuchapwa mara ya kwanza 1989.

Haya si mambo ya maskhara, kejeli na kufanya utani.
nyerere toka afariki ni muda gani?

EAMWS bado ipo?

kama ipo kwanini msijiunge mjenge hivyo vyuo?

umebaki kupiga soga mapipa basi kwenye vijiwe vya kahawa!

unajifaragua unajualikana duniani huko, umeleta juhudi gani kujenga hata chuo cha kufuguia kuku?
 
Stux...
Hakika yanaweza kuwa ni maradhi.

Hakuna jamii inayoweza kukubali kufutiwa historia yake khasa inapokuwa walioifuta wamefanya hivyo kwa kutaka kufifilisha dini ya wanajamii hiyo.

Kama sijaumwa na kitendo hicho nini kitaniuma?

Maradhi yaliyoikumba historia yetu yameponyeshwa na dawa hizo.

Ikiwa utapenda kuniita Mujahid hii kwangu ni sifa nzuri ninayoitamani niwe nayo.

Nimeandika vitabu kadhaa kuhakikisha kuwa historia hii haipotezwi tena kamwe.

Na wasomi wa historia ya Afrika wakaniunga mkono.

Historia hii imo katika Cambridge Journal of African History na Dictionary of African Biography (DAB) history ambayo Tanzania ilifutika kabisa.

Maradhi yaliyoathiri historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika yameponyeshwa na dawa hizo hapo juu.
unapondea hawa makafir lakini kila kukicha uko vyuoni kwao unazurura na kanzu lako kukubali mialiko.
 
Babu...
Tatizo ni historia ya uhuru ilifutwa na mimi nikaandika kitabu kuisahihisha.

Historia Sykes haijawa blah, blah.

Mimi baada ya kuieleza sasa iko katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kufanya hivi si chuki.

Chuki unayo wewe ambaenl umenitukana.
wewe sema umeandika kitabu chako sio kuisahihisha,ingekuwa kuisahihisha hicho kipeperushi chako ndo ingekuwa reference katika vyuo vya Tanzia!
 
Babu...
Kwanza si kweli kuwa huna dini.

Pili katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ukithubutu kutaka kukwepa Uislam tayari ushaipoteza historia yenyewe.
we mfia dini,nchi sio msikiti.Huwezi kumshusha nyerere hata udhikir uchi,nyerere ndo baba wa taifa hili na sio sykes wala wazee wako wa kimanyema,nyerere ni wa darja ya juu mno,itabaki hivyo mpaka unafukiwa kwenye mwanandani.

hutaki ndo' hivyo,unataka ndo' hivyo!
 
Stux...
Uislamu umewatisha wengi katika uandishi wa historia ya uhuru wa Tanganyika.

Katika kitabu alichohariri John Iliffe kuna sura kaandika: Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114.

Katika kitabu hiki Kleist Sykes ananukuliwa akisema katika historia ya maisha yake na ndiyo historia ya kuundwa kwa African Asociation 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika !933 kuwa waasisi wangi wa AA walikuwa Waislam kwa kuwa Wakristo walikuwa wakionywa na kanisa wasijihusishe na siasa.

Unaniuliza kama Abdul Sykes alisukumwa na Uislam kugombania uhuru wa Tanganyika.

Swali lako lingekuwa hivi: ''Je, baba yake Abdul, Mzee Kleist alisukumwa na Uislam kuasisi AA na kisha Al Jamiatul Islamiyya?''

Wakati wazalendo wa Southern Province Suleiman Masudi Mnonji, Salum Mpunga na Yusuf Chembera wanaunda TANU Lindi wakajikuta wako Waislam watupu kwa sababu Wamishionari kutoka Peramiho walikuwa wanawatisha waumini wao kujiweka mbali na TANU wakidai kuwa TANU ilikuwa inatayarisha vita vingine vya Maji Maji dhidi ya Waingereza.

Hiki ni kisa cha kusisimua nimekieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Si mimi niliyelazimisha Uislam uwe mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa nini kiongozi wa juu kabisa wa Waislam Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru akiuza kadi za TANU misikitini wakati Kadinali Rugambwa hakuonekana popote katika harakati hizi?

Hizi ni changamoto za ukoloni.

Yapo mengi katika ''Islam as a field of enquiry'' tunayoweza kujadili.

Hapo ndipo nilipochukua ukurasa mmoja na kufanya utafiti kutaka kujua kwa nini ilikuwa hivi?

Hivi ndivyo nilivyojua kwa nini Uislam unawatisha watafiti wengi katika historia ya Tanganyika.

Wewe ukiwa mmoja wa hao.

wacha kumfananisha kadinali Rugambwa na wazee wako wacheza bao wasio na elimu.Rugambwa ni habari nyingine.
 
we mfia dini,nchi sio msikiti.Huwezi kumshusha nyerere hata udhikir uchi,nyerere ndo baba wa taifa hili na sio sykes wala wazee wako wa kimanyema,nyerere ni wa darja ya juu mno,itabaki hivyo mpaka unafukiwa kwenye mwanandani.

hutaki ndo' hivyo,unataka ndo' hivyo!
Lukubuzo...
Unaandika hasira zimepanda.
Hasira zinazuia ubongo kufikiri vyema.

Sijapata kumdogosha Mwalimu na laiti ningeandika kitabu changu na kujaribu kushusha heshima ya Nyerere leo kitabu changu kingekuwa hakipo sokoni na wewe na mimi tusingekuwa hapa tunajadili historia ya uhuru wa Tanganyika.

Hakuna anaepinga kuwa Nyerere ni Baba wa Taifa.

Wala haitakuja ikawa Abdul Sykes aitwe baba wa chochote.

Historia ya Abdul Sykes na ya baba yake Kleist ni nyingine kabisa.

Kleist Sykes aliasisi African Association 1929 baada ya kukutana na Dr. Kwegyir Aggrey kutoka Achimota College Ghana.

Hivi ndivyo mimi ninavyosomesha historia ya uhuru wa Tanganyika.

Huanza kwa kuwaambia wanafunzi wangu waanze kwa kumsoma Kleist katika Dictionary of African Biography (DAB) kisha katika kamusi hilo hilo huwaambia wafunue ukurasa wenye historia ya Dr. Aggrey wamsome.

Baada ya hapo wakiwa washawajua wazalendo hawa ndiyo nakuja kwa Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Chief David Kidaha Makwaia na Julius Nyerere.

Nimefanikiwa hata kuwasisimua walimu wa miaka mingi wa historia ya Tanganyika.

Hakuna leo mwalimu wa historia ya uhuru wa Tanganyika anaependa kusomesha historia hii kwa kuanza na Nyerere.

Sasa ni miaka 25 ishapita kitabu cha Abdul Sykes bado kipo midomoni mwa wasomaji wakiuliza hili na lile.

Wako kama wewe wanachomwa nyoyo kusoma historia mpya ya TANU iliyokuwa mbali sana na historia rasmi ya TANU iliyoandikwa na ChuoChaCCMKivukoni.

Kuhusu Wamanyema katika historia hii huwaeleza pamoja na Wazulu na Wanubi walioingia Germany Ostafrika na Hermann von Wissmann kama askari mamluki kuimarisha jeshi la Wajerumani.

Babu yangu mkuu Mwekapopo Muyukwa ni mmoja katika askari hawa.

Hapa wanafunzi wangu wanamsoma Mbuwane Sykes babu yake Abdul Sykes aliyekuja kupigana na Abushiri bin Salim na Mkwawa.

1680517568079.jpeg

Kushoto Iddi Faiz Mafungo (Mmanyema), Sheikh Mohamed Ramia (Mmanyema), Julius Nyerere (Mzanaki) Saadan Abdu Kandoro (Mmanyema) Haruna Iddi Taratibu (Mmanyema) Dodoma Railway Station 1955/56.​

Hao wazalendo hapo juu wote wana sifa za kutukuka.

Iddi Faiz Mafungo alikuwa Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na ndiye aliyekuwa mkusanyaji wa fedha za safari ya kwanza ya Nyerere UNO.

Sheikh Mohamed Ramia ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa TANU Bagamoyo na Khalifa wa Qadiriyya.

Saadan Abdul mwanasiasa mkubwa Kanda ya Ziwa na ni katika wazalendo 17 walioasisi TANU 1954.

Haruna Iddi Taratibu muasisi wa TANU Central Province.
 
wacha kumfananisha kadinali Rugambwa na wazee wako wacheza bao wasio na elimu.Rugambwa ni habari nyingine.
Lukubuzo,
Kawaida ninapohisi mtu kaghadhibika humshauri tusimamishe mjadala.

Nakuona hapa unawatukana watu wazima wenye heshima kubwa katika historia ya Mwalimu Nyerere mwenyewe.

Nakushauri hivi kuzuia matusi.
 
Lukubuzo...
Unaandika hasira zimepanda.
Hasira zinazuia ubongo kufikiri vyema.

Sijapata kumdogosha Mwalimu na laiti ningeandika kitabu changu na lujaribu kushusha heshima ya Nyerere leo kitabu changu kingekuwa hakipo sokoni na wewe na mimi tusingekuwa hapa tunajadili historia ya uhuru wa Tanganyika.

Hakuna anaepinga kuwa Nyerere ni baba wa taifa.

Wala haitakuja ikawa Abdul Sykes aitwe baba wa chochote.

Historia ya Abdul Sykes na ya baba yake Kleist ni nyingine kabisa.

Kleist Sykes aliasisi African Association 1929 baada ya kukutana na Dr. Kwegyir Aggrey kutoka Achimota College Ghana.

Hivi ndivyo mimi ninavyosomesha historia ya uhuru wa Tanganyika.

Huanza kwa kuwaambia wanafunzi wangu waanze kwa kumsoma Kleist katika Dictionary of African Biography (DAB) kisha katika kamusi hilo hilo huwaambia wafunue ukurasa wenye historia ya Dr. Aggrey wamsome.

Baada ya hapo wakiwa washawajua wazalendo hawa ndiyo nakuja kwa Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Chief David Kidaha Makwaia na Julius Nyerere.

Nimefanikiwa hata kuwasisimua walimu wa miaka mingi wa historia ya Tanganyika.

Hakuna leo mwalimu wa historia ya uhuru wa Tanganyika anaependa kusomesha historia hii kwa kuanza na Nyerere.

Sasa ni miaka 25 ishapita kitabu cha Abdul Sykes bado kipo midomoni mwa wasomaji wakiuliza hili na lile.

Wako kama wewe wanachomwa nyoyo kusoma historia mpya ya TANU iliyokuwa mbali sana na historia rasmi ya TANU.

Kuhusu Wamanyema katika historia hii huwaekeza pamoja na Wazulu na Wanubi walioingia Germany Ostafrika na Hermann von Wissmann kama askari mamluki.

Hapa wanafunzi wangu wanamsoma Mbuwane Sykes babu yake Abdul Sykes aliyekuja kupigana na Abushiri bin Salim na Mkwawa..
Nimebahatika kukutana na wazee ambayo wanaifahamu historia vema ya Tanganyika. Naungana na wewe Kwa kuandika vema na vile ambavyo nimekuwa na simuliwa historia ya Tanganyika.

Sehemu ambayo umeenda tofauti ni kukumuisha Imani katika historia hii. Hili linaleta ukakasi, unaonekana unauhubili kufichwa historia Kwa misingi ya dini. Jambo ambalo linaweza kuwa ni mapungufu ya waandishi. Vinginevyo nimependa jinsi ulivyoandika. Nitavitafuta vitabu hivyo nivisome Kiongozi.
 
[/QUOTE]
Nimebahatika kukutana na wazee ambayo wanaifahamu historia vema ya Tanganyika. Naungana na wewe Kwa kuandika vema na vile ambavyo nimekuwa na simuliwa historia ya Tanganyika.

Sehemu ambayo umeenda tofauti ni kukumuisha Imani katika historia hii. Hili linaleta ukakasi, unaonekana unauhubili kufichwa historia Kwa misingi ya dini. Jambo ambalo linaweza kuwa ni mapungufu ya waandishi. Vinginevyo nimependa jinsi ulivyoandika. Nitavitafuta vitabu hivyo nivisome Kiongozi.
Mwana...
Unadhani kwa nini historia hii ilifutwa?
 
wacha kumfananisha kadinali Rugambwa na wazee wako wacheza bao wasio na elimu.Rugambwa ni habari nyingine.
Luku...
Sina ujasiri wa kumfananisha Kadinali Rugambwa na kitu chochote kile sembuse na wazee wangu waliosimama na Nyerere kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kadinali Rugambwa yeye hakuwapo.

Vipi ataingizwa na kuenea kati ya wazalendo hawa mfano wa Sheikh Mohamed Yusuf Badi aliyempokea Nyerere Lindi kwa zafa na dufu?

Au nimfananishe na Sheikh Abdallah Rashid Sembe aliyefanya dua Mnyanjani pamoja na Nyerere na masheikh wengine kuomba TANU ivuke mgogoro wa Kura Tatu?"

1680519807082.jpeg
1680519935098.jpeg

Sheikh Abdallah Rashid Sembe



 
nyerere toka afariki ni muda gani?

EAMWS bado ipo?

kama ipo kwanini msijiunge mjenge hivyo vyuo?

umebaki kupiga soga mapipa basi kwenye vijiwe vya kahawa!

unajifaragua unajualikana duniani huko, umeleta juhudi gani kujenga hata chuo cha kufuguia u?
Luku...
Nasikitika kuwa umeamua kuleta matusi badala ya hoja.

Katika miaka ya 1970 Organisation of Islamic Conference (OIC) ilitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Serikali ilikataa kutoa kibali na chuo hicho kikajengwa Mbale, Uganda.

Mwaka wa 1997 Darul Imam kutoka Saudi Arabia ilitaka kujenga Chuo Cha Ufundi Kibaha.

Baada ya kila kitu kukamilika ikazuka vurugu kubwa Darul Iman ikaondoka kwa nia ya kupeleka mradi ule nchi nyingine ya Kiafrika iliyo tayari kupokea msaada ule.

Aboud Jumbe aliingia kati kwa hoja kuwa ikiwa Tanganyika haiwezi kupokea msaada ule basi uletwe Zanzibar.

Hili lilifanikiwa na ndiyo kikajengwa Chuo Kikuu Tunguu badala ya Shule ya Ufundi iliyokusudiwa Kibaha.
 
Nafikiri labda wangesema kisukuma ni lugha mojawapo badala ya kiarabu
 
Back
Top Bottom