Tufanye nini na hizi clip zinazopotosha Historia ya Tanzania?

Tufanye nini na hizi clip zinazopotosha Historia ya Tanzania?

Von...
Nimeeleza hapa mara nyingi kuwa hili si jambo la dini ila historia ya uhuru wa Tanganyika ilivurugwa kwa makusudi kupoteza mchango wa wazee wangu katika kupigania uhuru.

Nimekaa kitako nimeiandika na sasa ni historia mashuhuri.

Historia hii sikuiandika leo.

Nimeiandika nikiwa kijana sana katika umri wa miaka 30.

Hakika historia yetu imebebwa na udugu.

Nitakuwekea hapa picha kama ushahidi wa udugu huu na nitakuachia wewe kuweka caption ya picha hizo.

Hakika hapakuwa na hoja ya dini kwani lingekuwako suala la dini Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika katika miaka ya 1950 asingemuunga mkono Nyerere kuchukua uongozi wa TAA 1953 kisha uongozi wa TANU 1954.

Kwa kuhitimisha ningependa unieleze imekuwaje na nini kimetokea leo tuko katika hali hii?


Von...
Hapakuwa na sababu ya kunikejeli kuwa ''nazeeka vibaya.''

Wewe kijana lakini katika maandishi yako sikuona fikra pevu ila kejeli dhidi yangu.

Picha hizo hapo juu za historia ya maisha ya Julius Nyerere alivyoishi na wazee wetu.

Nakuachia wewe kutuweka maelezo ya picha hizo.
Ukishindwa sema mimi nitaweka maelezo.

Baadhi ya wazee hao mimi nimewafahamu nakua Dar es Salaam ya 1960s napata akili nawaona na wengine niliwadiriki katika uhai wao na nikazungumzanao wakati naandika historia ya uhuru.

Wote wazee hawa niliozungumzanao waliniombea dua njema nikamilishe historia yao katika kuligania uhuru wa Tanganyika.
Mzee wangu heshima yako, ninayo dhamira haswa ya kufanya mahojiano na wewe kwenye online tv. Nipo tayari kupokea maelekezo toka kwako.
 
We mzee kalale sasa, unajua nyie wavaa kobazi ni majuha kupindukia,
We kila muda unazungumzia vitabu vitabu, Udini udini, Sykes blaah blaah sijui nilikua Wapi na wapi wakati huko watu wapo kila siku.
Embu usilete upumbavu.
Mwl Julius Nyerere ni baba wa taifa hili.
Sasa hata heshima yako hapa inateketea kwa ajili ya mambo yako ya ajabu ajabu na Udini.
Na Chuki zako kwa dini zingine.
Im Pagan anyway
Babu...
Tatizo ni historia ya uhuru ilifutwa na mimi nikaandika kitabu kuisahihisha.

Historia Sykes haijawa blah, blah.

Mimi baada ya kuieleza sasa iko katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kufanya hivi si chuki.

Chuki unayo wewe ambaenl umenitukana.
 
Mzee sheikh Mohammed unazani kuna umuhimu wa familia za wapigania uhuru wa Tanzania ambao wengi ni waislam kupewa tuzo? Au wapewe zawadi yoyote kwa kuthamini mchango wao ni kuombwa samahani baada ya Nyerere kutowathamini? Au nini kifanyike maana kizazi cha sasa ndo kabisa hawajui hayo mambo na wanaenda kufutika kweli hao wadai wa uhuru OG
Massa,
Hayo si yangu mimi kuamua.

Nililofanya mimi nimesahihisha historia iliyokuwa na makosa na kuandika historia ya kweli.

Sidhani kama hili ni tatizo.
 
Dudu...
Historia ya uhuru wa Tanganyika na historia ya Nyerere katika harakati hizo ni changamoto kubwa kwa wasomi na wanahistoria wetu.

Siwalaumu.

Inahitaji mtu shujaa kweli kweli kueleza historia hii kwa ukweli wake unaostahili.

Unaelezaje mchango wa Waislam maarufu waliounda African Association 1929 lakini wamefutwa katika historia ya TANU?

Unaelezaje kupigwa marufuku na serikali EAMWS na kuundwa BAKWATA wakati ilikuwa inajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968?

Unajibu nini utakapoulizwa nini ilikuwa nafasi ya Julius Nyerere katika matatizo yote haya?

Nimeandika kitabu na yote haya nimeyaeleza kama yalivyostahili kuelezwa.

Kitabu hiki naamini unakijua au umepata kukisikia kimebadili si historia ya uhuru wa Tanganyika na TANU bali hata historia ya Julius Nyerere.

Kitabu kinakwenda toleo la tano toka kuchapwa mara ya kwanza 1989.

Haya si mambo ya maskhara, kejeli na kufanya utani.

Wewe ni mgonjwa wa akili,inferiority complex ndio inakusumbua,hii nchi wengi tu wametoa mchango wa uhuru,akiongoza mapambano JKNyerere,itabaki hivyo milele na milele. Poleni kwa sababu matarajio yenu yalifeli,Nyerere aliweka misingi imara sana ya umoja na amani katika nchi hii kwa kila jamii iliyopo hapa tz,hichi ndicho kinachowauma sana ulitamani hii nchi ivae hijabu na bharagashia.

Umepuuzwa na utaendelea kupuuzwa hata ujitutume vipi mzee ushafeli,hiyo historia utasoma wewe na wajukuu zako tu ila historia ya Tanganyika ilishaandikwa.
 
Babu...
Tatizo ni historia ya uhuru ilifutwa na mimi nikaandika kitabu kuisahihisha.

Historia Sykes haijawa blah, blah.

Mimi baada ya kuieleza sasa iko katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kufanya hivi si chuki.

Chuki unayo wewe ambaenl umenitukana.
Mzee mohd una busara sana ila hapo kwenye hiyo mantiki unakera.
Jaribu kutupa ilimu vijana wako bila kuingiza mambo ingine.
Tunalo la kujifunza toka kwako,
Lakini mtu akikusoma unazungumzia usilamu sijui nini na nini tunashangaa.
Kuna history nzuri tu huwa unaandika mbona mtu anasoma bila mawaa.
Wengine hatuna dini.
Sorry kwa kauli ingine huko juu
 
Massa,
Hayo si yangu mimi kuamua.

Nililofanya mimi nimesahihisha historia iliyokuwa na makosa na kuandika historia ya kweli.

Sidhani kama hili ni tatizo.

Sheikh Mohammed unazani vitabu vyako licha ya kutafasiliwa mara nne je vimesomwa na watu wengi? Hasa kwa watanganyika sisi. Na kama ni hapana unampango gani kuvifanya viwafikie watu wengi ili kuweza kujua history ya kweli ya uhuru wa tanganyika?
 
Mzee mohd una busara sana ila hapo kwenye hiyo mantiki unakera.
Jaribu kutupa ilimu vijana wako bila kuingiza mambo ingine.
Tunalo la kujifunza toka kwako,
Lakini mtu akikusoma unazungumzia usilamu sijui nini na nini tunashangaa.
Kuna history nzuri tu huwa unaandika mbona mtu anasoma bila mawaa.
Wengine hatuna dini.
Sorry kwa kauli ingine huko juu
Babu...
Kwanza si kweli kuwa huna dini.

Pili katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ukithubutu kutaka kukwepa Uislam tayari ushaipoteza historia yenyewe.
 
Wewe ni mgonjwa wa akili,inferiority complex ndio inakusumbua,hii nchi wengi tu wametoa mchango wa uhuru,akiongoza mapambano JKNyerere,itabaki hivyo milele na milele. Poleni kwa sababu matarajio yenu yalifeli,Nyerere aliweka misingi imara sana ya umoja na amani katika nchi hii kwa kila jamii iliyopo hapa tz,hichi ndicho kinachowauma sana ulitamani hii nchi ivae hijabu na bharagashia.

Umepuuzwa na utaendelea kupuuzwa hata ujitutume vipi mzee ushafeli,hiyo historia utasoma wewe na wajukuu zako tu ila historia ya Tanganyika ilishaandikwa.
Jiwe...
Tabu kupuuza kitabu chenye elimu mpya.

Hii ndiyo sababu nikatiwa katika Cambridge Journal of African History na Dictionary of African Biography (DAB) na nikatiwa katika miradi ya uandishi wa vitabu vya historia.

Halikadhalika nikapata pia fursa ya kuzungumza katika vyuo mbalimbali.
 
Babu...
Kwanza si kweli kuwa huna dini.

Pili katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ukithubutu kutakaku kukwepa Uislam tayari ushaipoteza historia yenyewe.
Hamna shida mzee wangu mwaga nondo hapahapa.
Sykes hawa wa mwisho si tushakaa nao sana socialy sijawai kuwaskia kuongelea dini wala kugusia mambo ya siasa.
Ni watu ambao hawana mambo hayo.
Mtaongea, kucheka na kutaniana hawajawai hata kutaja jina la baba yao
Wala politic, wala Nyerere, wala kitu chochote cha baba zao.
Ina maana hawajui?
No ni kwamba hawataki mambo mengi.
Vitabu vyako ni vizuri kusoma kujifunza
Ila ukiingiza Udini mtu anakosa interest hata kununua.
Hapo uwe Neutral.
Mtu akikutana na mawaidha yako huko kitabuni kashanunua atasoma au apite hizo kurasa.
Lakini haya mambo hapa sio mahali pake
Utakosa washabiki.
Ingawa kiukweli maandishi yako yanafundisha mengi tu.
 
Mzee sheikh Mohammed unazani kuna umuhimu wa familia za wapigania uhuru wa Tanzania ambao wengi ni waislam kupewa tuzo? Au wapewe zawadi yoyote kwa kuthamini mchango wao ni kuombwa samahani baada ya Nyerere kutowathamini? Au nini kifanyike maana kizazi cha sasa ndo kabisa hawajui hayo mambo na wanaenda kufutika kweli hao wadai wa uhuru OG
Hili swali ni zuri
 
Hamna shida mzee wangu mwaga nondo hapahapa.
Sykes hawa wa mwisho si tushakaa nao sana socialy sijawai kuwaskia kuongelea dini wala kugusia mambo ya siasa.
Ni watu ambao hawana mambo hayo.
Mtaongea, kucheka na kutaniana hawajawai hata kutaja jina la baba yao
Wala politic, wala Nyerere, wala kitu chochote cha baba zao.
Ina maana hawajui?
No ni kwamba hawataki mambo mengi.
Vitabu vyako ni vizuri kusoma kujifunza
Ila ukiingiza Udini mtu anakosa interest hata kununua.
Hapo uwe Neutral.
Mtu akikutana na mawaidha yako huko kitabuni kashanunua atasoma au apite hizo kurasa.
Lakini haya mambo hapa sio mahali pake
Utakosa washabiki.
Ingawa kiukweli maandishi yako yanafundisha mengi tu.
Babu...
Unawazungumza nani hao uliokaanao?

Watoto au wajukuu?
Miaka gani umekaa nao?

Hao unaowazungumza huenda ni wajukuu waliozaliwa miaka mingi sana baada ya babu zao kufariki wamekuta historia ya babu zao haipo tena katika historia ya Tanganyika.

Ishafutwa.

Picha ya pili chini imepigwa mwaka wa 1968 baadhi yetu katika picha hiyo ni kizazi cha kwanza cha wapigania uhuru.

Sote tukijua michango ya wazee wetu katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Suala la Uislam huwezi kulikwepa katika historia ya uhuru wa Tanganyika na kuiandika historia hii haliwezi kuwa suala la udini.

Kuwataja Wakikuyu na Mau Mau katika uhuru wa Kenya si suala la ukabila ni ukweli katika historia hiyo.

Kitabu hiki kina miaka 25 toka kichapwe mwaka wa 1989 na sasa tunakwenda toleo la tano.

Hakina shida ya wasomaji kimependwa sana na sababu yake ni kuwa kimeeleza historia ya wazalendo wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika ambao walifutwa katika historia.

Bahati mbaya kwako wengi wao ni Waislam na wengine ni masheikh.

Hapa ndipo lilipokuwa tatizo na kitabu cha Abdul Sykes imeliondoa tatizo hili.

Kila aliyehusika katika historia ya TANU katajwa katika kitabu hiki.

1680446574804.jpeg

Kushoto: Kleist Sykes, Miski Sykes, Mwandishi (ameshika Medali ya Mwenge wa Uhuru aliyopewa Abdul Sykes mwaka wa 2011 kwa ajili ya mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika) Aisha ''Daisy'' Sykes na Ilyaas Sykes.
Picha ya 2017

1680446819168.jpeg

Kushoto waliosimama: Abdallah Tambaza, Booby Bokhari, Kleist Sykes, Yusuf Zialor, Mwandishi,
Kushoto waliochutama: Kaisi, Wendo Mwapacha Abdul Mtemvu
Picha ya 1968.
 
Sheikh Mohammed unazani vitabu vyako licha ya kutafasiliwa mara nne je vimesomwa na watu wengi? Hasa kwa watanganyika sisi. Na kama ni hapana unampango gani kuvifanya viwafikie watu wengi ili kuweza kujua history ya kweli ya uhuru wa tanganyika?
Massa,
Mimi ni mwandishi.

Shughuli ya kusambaza kitabu ni ya publisher na wauzaji vitabu.

Kitabu ni mali ya publisher yeye ndiye aliyewekeza fedha zake kukichapa na ndiye mwenye fungu kubwa katika mauzo.

Kitabu kinafanya vyema kinakwenda toleo la tano.

1680447913418.jpeg
 
Massa,
Mimi ni mwandishi.
Shughuli ya kusambaza kitabu ni ya publisher na wauzaji vitabu.

Kitabu ni mali ya publisher yeye ndiye aliyewekeza fedha zake kukichapa na ndiye mwenye fungu kubwa katika mauzo.

Kitabu kinafanya vyema kinakwenda toleo la tano.

Kitabu kina kwenda vema kimauzo jambo zuri sana sheikh. Ila walengwa hasa wa kitabu ni wazungu au watanganyika? Ambao ndo inabidi tujue ukweli hasa wa jinsi uhuru ulivyopatikana. Kitabu kinapatina wapi na kwa bei gani. Usione vibaya kuwasaidia publisher kupush mauzo maana lazima unapata percentage kwa kila Kitabu kinachouzwa
 
Kitabu kina kwenda vema kimauzo jambo zuri sana sheikh. Ila walengwa hasa wa kitabu ni wazungu au watanganyika? Ambao ndo inabidi tujue ukweli hasa wa jinsi uhuru ulivyopatikana. Kitabu kinapatina wapi na kwa bei gani. Usione vibaya kuwasaidia publisher kupush mauzo maana lazima unapata percentage kwa kila Kitabu kinachouzwa
Massa,
Kitabu nimekiandika kwa Kiingereza Minerva Press London (1989)kikatafsiriwa na kuchapwa na Phoenix Publishers Nairobi (2002).

Hawa wana idara nzima ya masoko.

Kitabu kinapatikana IBM Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro, Msikiti wa Manyema na Msikiti wa Mtambani.

Bei shs: 10, 000.00.
 
Babu...
Kwanza si kweli kuwa huna dini.

Pili katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ukithubutu kutaka kukwepa Uislam tayari ushaipoteza historia yenyewe.
Siyo lazima utaje uislamu katika historia hiyo ni FALSE HYPOTHESIS!! Wataje tu akina Abdulwahid Sykes kama Watanganyiaka walioasisi mapambano ya uhuru, inatosha. Usiulazimishe UISLAMU. Hapo ndipo mzee Mohamed Said unaharibu.

Na kama huo ndiyo msingi wa vitabu vyako basi tambua umeandika trash kwa kuwa umewagawa Watanzania.

Jubu swali hili. Je Abdulwahid Sykes alisukumwa na Uislamu kugombania uhuru? Au alisukumwa na exposure aliyoiona baada ya kuwa askari wa jeshi la mkoloni kwenye World War 1 & 2?
 
Siyo lazima utaje uislamu katika historia hiyo ni FALSE HYPOTHESIS!! Wataje tu akina Abdulwahid Sykes kama Watanganyiaka walioasisi mapambano ya uhuru, inatosha. Usiulazimishe UISLAMU. Hapo ndipo mzee Mohamed Said unaharibu.

Na kama huo ndiyo msingi wa vitabu vyako basi tambua umeandika trash kwa kuwa umewagawa Watanzania.

Jubu swali hili. Je Abdulwahid Sykes alisukumwa na Uislamu kugombania uhuru? Au alisukumwa na exposure aliyoiona baada ya kuwa askari wa jeshi la mkoloni kwenye World War 1 & 2?
Stux...
Uislamu umewatisha wengi katika uandishi wa historia ya uhuru wa Tanganyika.

Katika kitabu alichohariri John Iliffe kuna sura kaandika: Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114.

Katika kitabu hiki Kleist Sykes ananukuliwa akisema katika historia ya maisha yake na ndiyo historia ya kuundwa kwa African Association 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika !933 kuwa waasisi wangi wa AA walikuwa Waislam kwa kuwa Wakristo walikuwa wakionywa na kanisa wasijihusishe na siasa.

Unaniuliza kama Abdul Sykes alisukumwa na Uislam kugombania uhuru wa Tanganyika.

Swali lako lingekuwa hivi: ''Je, baba yake Abdul, Mzee Kleist alisukumwa na Uislam kuasisi AA na kisha Al Jamiatul Islamiyya?''

Wakati wazalendo wa Southern Province Suleiman Masudi Mnonji, Salum Mpunga na Yusuf Chembera wanaunda TANU Lindi wakajikuta wako Waislam watupu kwa sababu Wamishionari kutoka Peramiho walikuwa wanawatisha waumini wao kujiweka mbali na TANU wakidai kuwa TANU ilikuwa inatayarisha vita vingine vya Maji Maji dhidi ya Waingereza.

Hiki ni kisa cha kusisimua nimekieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Si mimi niliyelazimisha Uislam uwe mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa nini kiongozi wa juu kabisa wa Waislam Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru akiuza kadi za TANU misikitini wakati Kadinali Rugambwa hakuonekana popote katika harakati hizi?

Hizi ni changamoto za ukoloni.

Yapo mengi katika ''Islam as a field of enquiry'' tunayoweza kujadili.

Hapo ndipo nilipochukua ukurasa mmoja na kufanya utafiti kutaka kujua kwa nini ilikuwa hivi?

Hivi ndivyo nilivyojua kwa nini Uislam unawatisha watafiti wengi katika historia ya Tanganyika.

Wewe ukiwa mmoja wa hao.

1680465036102.jpeg
 
Back
Top Bottom