Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 7,799
- 14,215
- Thread starter
-
- #121
😀😂😂😂Pole sana,
Nimesikitishwa sana na taarrifa hizi, nimefedheheshwa sana na askari wetu kwa hatua walizochukua dhidi ya raia huko kawe.
Naomba utulivu na subiira kidogo ili kujiridhisha na hatimae, niwahakikishie, hatua kali stahiki za kijeshi zitachukuliwa dhidi ya wote watakao thibitika kushiriki aibu hii...
Kweli kbs mkuu.Naunga mkono hoja hii kila mmoja asimame kwenye nafasi yake.
Hakuna nafsi inapenda kuonewa
I think ndio yeye. Maana afisa alieuwawa, kiasili anatokea mkoa wa Singida.Au ndiye yule tumeona wanamzika Manyoni, wanasema kaua Dar , Afisa wa Jeshi?
R.I.P Afisa
Machafuko hayo yatawaumza zaidi hao raia watakaofanya upumbavu huo.Wakiendeleza kupiga raia ovyo machafuko yatatokea tu.
Watu wakianza kuwategea mabomu ya kutengenezea majumbani mtaelewa tunacho onya sasa.
Cha mkunjo ndio nini?Afisa ameuwawa baada ya kuleta utemi wa kishamba.
Kaziba barabara, dogo akamuomba kistarab tu afisa huyo apaki gari yake vizuri ili dogo apate njia ya kupita na bajaj yake. Ofisa kuona macho ya watu akaona kadharauliwa na kutembeza makofi kwa dogo.
Dogo nae hakupenda unyonge uendelee, ndo akachomoa cha mkunjo na kulenga sehemu husika iliyomuangusha ofisa na kupelekea kupotez maisha.
Just imagine wakikuta mzee anatoka kutafuta riziki ya watoto wake wanakula ugoko.Mbaya zaidi wanalipa kisasi kwa kila aliyeko mbele yao, ina maana hata wangekutana na dingi yako anatoka misele wangekata funua tu. 🤣 🤣 🤣
Sasa tumeelewana!
Kweli mkuu, na sio wahusika kuchukuliwa hatua tu, bali pia wawaombe radhi waathirika wote wa tukio lile kwa kipigo na unyama waliowafanyia.Ni heri wachukuliwa hatua Hata kijeshi , ikiwezekana waachishwe kazi mana wamekosa nidhamu na wako above the law, kwa walichokifanya inaweza chochea kwa chuki mtaani na kuwindana
Daaah anyway mwamba ninamfahamu hakuwa na makuu likizo alikuwa Singida Manyoni, kwao ni Jirani na Makazi yangu ya zamani.I think ndio yeye. Maana afisa alieuwawa, kiasili anatokea mkoa wa Singida.
Mimi sio daktari aliefanyia uchunguzi mwili wa marehem.Alimchoma kisu sehemu gani?
Kwahiyo mfano mzazi wako au wewe mwenyewe ungekuwa unatoka zako town haujui hili wala lile unashuka tu kwenye basi unakumbana na jamaa wanaanza kukupiga huku na kule bila sababu wala kukuuliza chochote ungekaa kimya et kwa sababu hili sio swala la kisiasa?Kaeni.kimya acheni kuchochea msivyojua,haya mambo humalizwa kimya kimya bila kelele za media!!
Msifikiri Kila jambo huwa ni la kisiasa eti lazima watu wasikie!!
Tutulie!
Asante mkuu..Ahsante Kwa kupaza sauti....
Kweli kabisa mkuu.Kuna siku raia watavurugwa, hatatoka mwanajeshi mtaani..
Umemjibu vizuri san mkuu.Raia alimkuta mwanajeshi anafanya yake akamvamia tu bila sababu?
Raia alikuwa anajilinda sababu anayepaswa kumlinda ndiyo kamshambulia.
Hiyo kambi ya kawe ihamishwe iende Mbali na makazi ya watu!Kwahiyo mfano mzazi wako au wewe mwenyewe ungekuwa unatoka zako town haujui hili wala lile unashuka tu kwenye basi unakumbana na jamaa wanaanza kukupiga huku na kule bila sababu wala kukuuliza chochote ungekaa kimya et kwa sababu hili sio swala la kisiasa?
Kila binadamu nchini au duniani ana haki zake za kuishi kwa amani na usalama. Haiwezekani mtu haujui kilichotokea na wala haukuwepo eneo la tukio, ghafla tu unavamiwa na kuanza kupigwa hovyo kichwani miguuni na sehem zingine mbali mbali za mwili bila kuulizwa chochote. Na hata ukiulizwa kama jambo haulijua na haukuwepo kwenye eneo la tukio, humjui muuaji wala alieuwawa unafikiri utajibu nini?
Hapana mkuu sababu iliyosababisha kifo chake haikuwa mpira, bali ni kaubabe fulani, si unajua jeshi ni jeshi tu hata awe mpole vipi, lkn anakuwa na karoho fulan ka tofauti ni sisi raia wa kawaida.Daaah anyway mwamba ninamfahamu hakuwa na makuu likizo alikuwa Singida Manyoni, kwao ni Jirani na Makazi yangu ya zamani.
Pumzika Afisa , ukweli wa Jambo anaujua Mungu tu.
Yanayosemwa huku kuwa yalikuwa mabishano ya mpira eti?
Usingeandika huu ujinga wako kama hao wajinga wangevamia kwenu ,wakaanza kumpa kisago baba yako na mama yako na kuwajeruhi na wewe wakakupasua bila kosa lolote mlilofanya .Afrika siyo sehemu ya kuendekeza saaana kufuata Sheria.....Ni kipigo tuu....Sasa wewe mwanao mnyime kipigo ufuate sheria.
Raia za Afrika wakati mwingine wanaelewa kwa kipigo
Ushauri uliotoa ni mzuri sana mkuu. Lakini nafikiri ni vigumu mno kuhamisha kambi. Maana hii kambi ni ya muda mrefu sana.Hiyo kambi ya kawe ihamishwe iende Mbali na makazi ya watu!
Ndio msaada pekee!
Saikolojia ya wanajeshi sio sawa kwa raia!
Huo unaouona na hiyo Hali waliyonayo ndio inatufanya tuwe na amani hadi leo mkuu!!
Hao jamaa watengewe makazi yao nje ya mji kabisa!!
State of mind ya mjeda ni tofauti sana na hiyo uliyonayo!
Hivyo tu na Tena kama wamefiwa na mtu wao ndio kabisaa nawashauri Wana kawe wahamie huku mikoani kwa muda!!