Tuhuma za Madawa ya Kulevya: Kamishna Jenerali wa DCEA akosoa utaratibu alioutumia Makonda

Tuhuma za Madawa ya Kulevya: Kamishna Jenerali wa DCEA akosoa utaratibu alioutumia Makonda

Swala la kuwataja washukiwa ni kinyume na kanuni za kimaadili, ila ukweli wa kuhusika kwa waliotajwa nalo ni jingine.
Marekani na baadhi ya nchi za dunia ya kwanza kama wanavyojiita wao, uwataja washukiwa wote wanao shiriki biashara za madawa ya kulevya, bila hata kufikishwa mahakamani. Mahakama haipo kukutuhumu, bali unaweza kupewa tuhuma kisha mahakama ndo itaamua kama tuhuma hizo ni kweli au si kweli.

Kwa sheria zote za jinai Tanzania wanaofikishwa mahakamani uwa ni watuhumiwa si wakosaji. Watakuwa wakosaji mara mahakama inapothibitisha. Ni mara ngapi majambazi wamekamatwa kwa kushukiwa kufanya tukio la ujambazi?

Au ni mara ngapi watu wamekamatwa kwa kushukiwa tu kuuwa?

Uwezi subiri umshike mfanya biashara wa madawa kwa kumkuta na madawa. Huyu kamishina anatetea baadhi ya vigogo maarufu wafanyao hiyo biashara. Kwa mwendo huu tusahau vita dhidi ya madawa ya kulevya. Ni ubabaishaji tu! Hata Rais mwenyewe yupo kimya simsikii kakemea au kuongelea.
 
Jana katika kipindi cha Dk 45 ITV walikuwa na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ambaye alipinga vikali utaratibu uliyokuwa unatumiwa na aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa DSM Ndug Paul Makonda wa kuwataja hadharani watu aliokuwa akiwatuhumu au wakidhaniwa kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya.

Alienda mbali na kusema wao kama serikali hawawezi kukutaja hadaharani hivyo bila kuwa na uthibitisho na wala kutiwa hatiani na Mahakama.

Namnukuu pia "Si kila anayetajwa anahusika na dawa za kulevya, mtu mwingine naweza nkakutaja kwa visa tu"
-Gerald Kusaya - Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya.


Makonda kipindi hiki cha Kamishna Lyimo sijui kama atadhubutu kuchezea hii mamlaka inayotusaidia kudhibiti mawada.
 
Back
Top Bottom