Tujifunze kitu kwa misiba ya vigogo hawa na idadi ya watoto

Tujifunze kitu kwa misiba ya vigogo hawa na idadi ya watoto

Tahadhari kwa wazazi uzungu ukizidi sana ndio haya matokeo, ujasiri unaotoa wapi mtoto mdogo unamzika Baba yako uneongelea mziki wa Prof J, sisemi alie agalegale hapana ila sisi wa Africa wazazi tukipoteza ni pigo haijalishi wewe ni nani ila wenzetu naona mpaka tabia wanaiga za huko tuliona hata kwenye msiba wa Mafuru sijui labda ndio watoto wa kileo lakini mimi nilimzika mzazi wangu kwa uchungu hata kama sikulia hadharani lakini sura yangu sikuweza kuficha dhoruba.
Mkuu ukitambuka kuwa kifo ni sehemu ya maisha yetu huna haja ya kulia, kinachotuliza sisi masikini ni huduma, baba alikuwa ndio muhimili mkubwa wa familia, ametutoka je! Ni nani ataihudumia familia? Hapo kulia na kujigaragaza kunapoanza.
 
Mtu maskini akizaa mtoto anaongeza maskini mwingine duniani na kuipa serikali gharama kubwa sana ya kuhudumia umaskini wa kizazi chake.
Ni gharama ipi ambayo unaweza sema serikali za nchi za Africa zinaingia kwa ajili ya wananchi.

Maana serikali inaendeshwa kwa fedha za kodi zinazokusanywa toka kwa wananchi na wengi ni hao maskini.

Hao matajiri ndio wakwepaji kodi wakubwa na mpaka wanaajiri watu wa kuwashauri namna ya kukwepa kodi.
 
Ndio mkuu, huku mitaani watoto wamejaa tele wamekosa malezi
Ndandeki.
Mgawanyo wa majukumu wa kionezi sana huo. Yaan wengine ndiye wawe na haki ya kutiana na kuacha off-springs zao, huku wengine jukumu lao liwe kujenga uchumi na kulea hao wengine bila ya wao kuacha off-springs zao.
 
Usijidanganye..
.hao ni watoto waliojulikana,huko mitaaani anaeweza kuwa na watoto,Kuna mtu ndani ya ndoa alikuwa na watoto 2.kumbe inje ya ndoa anawatoto 4.
Usinambie nilijuaje!😂,
 
Nipo nacheki hapa msiba WA Ndugulile, kuacha watoto wawili tuu, pamoja alikuwa ana uwezo wa kipesa na cheo lakini kaishia kwenye watoto wawili, watoto wawili hawa naona kawakuza na kuwasomesha kwenye shule za gharama inawezekana nje ya nchi maana hata Kiswahili chao ni broken sana wanakuwa kama sio watanzania.

Lawrence Mafuru nae nadhani aliacha watoto wawili tuu.

Swali kwa makapuku wenzangu, hivi Sisi maskini tunazaa watoto wengi ili iweje? na utakuta pengne hata uwezo wa kuwahudumia tuu kikamilifu kwenye elimu na gharama za kila siku hatuwezi, nini maana ya hii?

Nahis NI vizuri kuzaa watoto kulingana na kipato chako, ambao utawamudu vizuri, utakaowapa elimu ya uhakika sio hii ya kuunga unga.

Sisi maskini tunawaza eti tukizaa watoto wengi ndio hao badae watatusaidia, wewe mzazi somesha mtoto, hudumia kwa kadiri ya uwezo wako maana ni jukumu lako, badae akipata maisha mazuri NI yeye sasa atajua atakusaidiaje, ndio ile utakuta wazazi wananunia wakwe zao wanaona kama wao ndio wanafanya wasipewe pesa na mtoto wao.

Tuzae Kwa mahesabu, utakuta mtu ana watoto wanne, halafu kapanga chumba na sebule, sasa jiulize hapo ndani wanaishije, tuwekeze nguvu kwenye kujenga uchumi Kwanza na kuzaa kwa akili.

View attachment 3167382
Mie nitachukua mfano wa tajiri namba moja duniani na wala sio wanasiasa.

Elon kafyatua 12 na anakwambia anaongezea
 
Nipo nacheki hapa msiba WA Ndugulile, kuacha watoto wawili tuu, pamoja alikuwa ana uwezo wa kipesa na cheo lakini kaishia kwenye watoto wawili, watoto wawili hawa naona kawakuza na kuwasomesha kwenye shule za gharama inawezekana nje ya nchi maana hata Kiswahili chao ni broken sana wanakuwa kama sio watanzania.

Lawrence Mafuru nae nadhani aliacha watoto wawili tuu.

Swali kwa makapuku wenzangu, hivi Sisi maskini tunazaa watoto wengi ili iweje? na utakuta pengne hata uwezo wa kuwahudumia tuu kikamilifu kwenye elimu na gharama za kila siku hatuwezi, nini maana ya hii?

Nahis NI vizuri kuzaa watoto kulingana na kipato chako, ambao utawamudu vizuri, utakaowapa elimu ya uhakika sio hii ya kuunga unga.

Sisi maskini tunawaza eti tukizaa watoto wengi ndio hao badae watatusaidia, wewe mzazi somesha mtoto, hudumia kwa kadiri ya uwezo wako maana ni jukumu lako, badae akipata maisha mazuri NI yeye sasa atajua atakusaidiaje, ndio ile utakuta wazazi wananunia wakwe zao wanaona kama wao ndio wanafanya wasipewe pesa na mtoto wao.

Tuzae Kwa mahesabu, utakuta mtu ana watoto wanne, halafu kapanga chumba na sebule, sasa jiulize hapo ndani wanaishije, tuwekeze nguvu kwenye kujenga uchumi Kwanza na kuzaa kwa akili.

View attachment 3167382
Hao ni wazembe tu, usilinganishe, je hana watoto wa pembeni?, sasa akina Jaffo mwenye wake wanne utasemaje, wewe zaa tu kila mtu ana mipango yake bwana
 
Ni gharama ipi ambayo unaweza sema serikali za nchi za Africa zinaingia kwa ajili ya wananchi.
Mikopo ya kugharimia maisha ya wananchi wengi maskini na matajiri wachache wakwepa kodi.

Hii ni gharama kubwa kwa serikali inayo zalisha madeni makubwa kwa serikali za Afrika.
Maana serikali inaendeshwa kwa fedha za kodi zinazokusanywa toka kwa wananchi na wengi ni hao maskini.
Serikali nyingi za Afrika zina endeshwa kwa mikopo na misaada ya wazungu.

Kwanza kwa Afrika watu wengi ni wakwepa kodi. Kwanzia maskini hadi matajiri.
.

Hao matajiri ndio wakwepaji kodi wakubwa na mpaka wanaajiri watu wa kuwashauri namna ya kukwepa kodi.
Afrika kila mtu ni mkwepa kodi.

Ni vile hao maskini hawajapata nafasi ya kuingia serikalini kupiga.

Ila mentality za waafrika wengi zimekaa kiwizi wizi.
 
Kosa kubwa alilofanya ni ile akili ya MTU mweusi ya kufanya Accumulation bila distribution

Yale maeneo potential yote aliyojimilikisha kigamboni Kama angeamua kutoa ghorofa lake moja akawapa wanafunzi wakaishi bure au akawa na programs maalumu za kuwalipia Ada wanafunzi hata wanafunzi 100 kila mwaka .

Tafsiri sahihi ya utajiri ya MTU mweusi huwa inafikirisha Sana .
Hii ndio shida ya Mwafrika. ..ubnafisi na Ulafi.

Wazungu wana hela sana. Wakishatimiza mahitaji yao muhumu pesa zinazobali wanatuletea Wafrika washenzi, miradi hii inayosaidia Wamama na Watoto na rai ni mingi
1. Malaria
2.TB
3.HiV
4. Afya ya Mama na Mtoto
5.Ukoma

Zote hizi ni pesa za wazungu wenye huruma kwa Binadamu wenzao.

Huku kwetu ni ufahari usio na faida yoyote hata kujenga kisima cha maji mtaani maskini wakapata maji hawajengi.

1.Magari ya kidahari
2.Nyumba za kifahari
3.Ardhi za kifahari
4. Ubaltasar mwingi

Mwisho wanakufa bila legasi yoyote waliyoacha
 
Mikopo ya kugharimia maisha ya wananchi wengi maskini na matajiri wachache wakwepa kodi.

Hii ni gharama kubwa kwa serikali inayo zalisha madeni makubwa kwa serikali za Afrika.

Serikali nyingi za Afrika zina endeshwa kwa mikopo na misaada ya wazungu.

Kwanza kwa Afrika watu wengi ni wakwepa kodi. Kwanzia maskini hadi matajiri.

Afrika kila mtu ni mkwepa kodi.

Ni vile hao maskini hawajapata nafasi ya kuingia serikalini kupiga.

Ila mentality za waafrika wengi zimekaa kiwizi wizi.
Mikopo na misaada ni uzembe wetu na hao tuliowapa dhamana.

Nchi Kama Singapore inategemea bandari zake na imetoboa.

Sisi tunachokosa ni uzalendo tu ila tuna kila kitu na bado maskini.
 
Binafsi huwa ni mwendo wa kufyatua, ilimradi Nina uwezo wa kuwalisha, kuwavisha na mazingira wezeshi kwaajili ya maisha Yao ya baadae nk... Huwa sijali chochote kile kisemwacho, watoto ni fahari kwangu. Nawafundisha wanangu kuhusu ubinadamu, wajue Kuna Leo na kesho kwenye maisha haya, wakipata wasiache kusaidia wenye tabu na shida, huu ndo wosia wangu kwao.
 
Tukianza kujilinganisha na Ndugulile na Mafuru utaona watu wengi hawàna sifa ya kuwa háta na nusu mtoto!
Siyo kweli kwamba hao wawili wanawakilisha wenye hela wote kuwa nà watoto wawili wawili.
Hao ni uzembe wao tuu mbona husemi waziri Jafo mwenye wake wanne na watoto lukuki?
Nchengerwa, Awesu, Hafidh nk wana hela na wana wake zaidi ya mmoja?
Unadhani hawa hawamjui Ndugulile, au Mafuru?
Jk,Mwinyi mzee,JkNyerere,Masabuli
 
Back
Top Bottom